SIKITIKO LANGU! Tanzania itabadilishwa na Watanzania wanaothubutu mabadiliko!

Ras

Senior Member
Mar 16, 2007
126
6
Ndugu zangu Watanzania, nawasalimu sana. Niandikapo thread hii najisikia uchungu sana moyoni. Hapo awali kabla sijatoka Tanzania na kutembelea nchi zingine niliona maisha yapo sawa tu kwa hapo Tanzania.

Lakini kwa sasa nipo nje ya nchi kwa kweli maisha ninayoona wanaishi wenzetu huku ni yale ambayo wengi wetu hapo nyumbani na tunaoamini dini twajipa moyo kuwa tutajaishi tukifa huko Paradiso!! I WAS VERY WRONG THINKING THAT GOOD LIFE CAN BE FOUND ONLY IN PARADISE!! PARADISE twaweza itengeneza sisi wenyewe kwa kuwa na MAAMUZI YENYE BUSARA KWA WAKATI MUAFAKA.

Tuachane na zile fikra kuwa pengine chama fulani kisipokuwa tawala kutatokea vita na amani haitokuwepo, NINI MAANA YA AMANI IWAPO WATU WANAKUFA KWA NJAA HUKO VIJIJINI?? Hospitali huduma hafifu!! Ujambazi unashamiri!! Nadhani ni wakati muafaka sasa wa kubadili mfumo! Hebu tuthubutu na tuone, uzuri ni kuwa miaka mitano tunafanya tena uchaguzi,

Tuchague na viongozi toka vyama vingine tuone mabadiliko! kama hayapo then uchaguzi mwingine tunachagua mwenye sera nzuri na zinazotekelezeka tukumbuke usemi kuwa "HE WHO DARE TO RISK SUCCEEDS" Wenztu huku hawaangalii sera za kusadikika! wanaangalia sera zenye kujenga uchumi wa Taifa!!

Hebu angalia thamani ya pesa ya Tanzania inavyoporoka kila kukicha!!! ni dalili mbaya. Kwa kweli ukiangalia wenzetu huku nje(Nipo bara la Asia) wanavyo-manage kodi zao na kuzitumia katika mambo ya maendeleo yanayoonekana, inatia uchungu sana sisi kwa nini tushindwe!! Si kwamba hakuna viongozi ambao ni Wazalendo wanaoweza kutufisha hapo lah! ni vile tu hatuthubutu kuwachagua.


WITO WANGU! TUBADILIKE, TUCHAGUE MTU AMBAYE ANA UWEZO NA UZALENDO PIA, TUJARIBU KUWAPA AU KUKIPA CHAMA KINGINE HATAMU TUONE MAMBO YATAENDAJE, WAKISHINDWA UCHAGUZI MWINGINE HATUWAPI TENA. KWA NJIA HII TUTAENDELEA. INASIKITISHA KUITWA NCHI MASKINI WAKATI TUNA KILA KITU ISIPOUWA TWAKUMBATIA MFUMO NA VIONGOZI WABOVU NA WEVI!

Samahani kama ntakuwa nimemkwaza yeyote ila huo ni uchungu wangu kama mzalendo! Laiti kama kila Mtanzania angeweza pata fursa ya kutoka na kuona nchi za Wenzetu zilivyopiga hatua! LAITI KAMA...nadhani tungefumbuka macho.
 
Ras you have spoken well! unadhani basi kuna haja ya kila Mtanzania kutoka nje ya hapa ili kuona hayo uyasemayo! la siku hizi kwa maendeleo haya ya teknolojia watanzania tunayaona hayo usemayo kwenye Runinga na siku hizi kupitia tovuti/wavuti. Tatizo tulilonalo ni udumavu wa kufikiri, uwoga wa kuthubutu na ujinga wa kupandikizwa kuwa bila CCM nchi haitawaliki! jana nilimsikia mgombe a mmoja wa Ubunge jimbo la Arusha alinena vyema sana, kuwa moja ya sera zake ni kuamsha uwezo wa kufikiri wa waTanzania, atafanyaje sijajua, lakini nilifarijika kusikia tu kuwa ameliona tatizo la msingi hapa ni uelewa duni na uwezo wa kuthubutu tulionao. lakioni usijali sana mapambano ndio yameanza sasa, hatudanganyiki tena na kama haitakuwa leo basi kesho yaani Ras ninachosema hapa ni Mdogomdogo hadi Ikulu!
 
Ras you have spoken well! unadhani basi kuna haja ya kila Mtanzania kutoka nje ya hapa ili kuona hayo uyasemayo! la siku hizi kwa maendeleo haya ya teknolojia watanzania tunayaona hayo usemayo kwenye Runinga na siku hizi kupitia tovuti/wavuti. Tatizo tulilonalo ni udumavu wa kufikiri, uwoga wa kuthubutu na ujinga wa kupandikizwa kuwa bila CCM nchi haitawaliki! jana nilimsikia mgombe a mmoja wa Ubunge jimbo la Arusha alinena vyema sana, kuwa moja ya sera zake ni kuamsha uwezo wa kufikiri wa waTanzania, atafanyaje sijajua, lakini nilifarijika kusikia tu kuwa ameliona tatizo la msingi hapa ni uelewa duni na uwezo wa kuthubutu tulionao. lakioni usijali sana mapambano ndio yameanza sasa, hatudanganyiki tena na kama haitakuwa leo basi kesho yaani Ras ninachosema hapa ni Mdogomdogo hadi Ikulu![/QUO

Kwa kweli inasikitisha sana Mkuu, mimi nimeliongea hili kwa uchungu mkuu. Ni kweli kabisa twahitaji kujikomboa katika hii fikra ya bila CCM nchi haina amani wala haitawaliki! twatakiwa kuchagua viongozi ambao wana uthubutu wa kutuletea maendeleo na si ahadi nzurinzuri tu. Kimsingi kwa Watanzania waliopo mijini naanza kuona mwamko lakini vijijini hali ni mbaya!! utakuta mtu masikini wa kutupa lakini yupo tu na ccm yake.,hawa kazi ipo sababu hawana TV, Internate na wachache wana Redio ambazo hazitoi picha. I la Inshallah naamini kama usemavyo tutafika, na twatakiwa kuanza sasa. Wenzetu wanafanya vitu hadi unafurahi ati!! barabara lami nchi nzima hadi vijijini, soko la mazao ya wakulima la uhakika, Mazingira safi, Usalama wa raia na mali zao wa kutosha. Kimsingi naamini kuwa iwapo tutakuwa na uongozi bora wa Kizalendo na kusimamia mapato yetu bila hiana hata hao vibaka na wezi hapo Dar. wanaotishia maisha ya wtu watapungua kaisa kama siyo kuisha sababu hata huyo kibaka anapenda kuwa na familia akaitwa Baba na kuilea familia yake sema tu hali halisi ya utawala ndiyo imempelekea hapo alipo! TUAMKE JAMANI! WAKATI NDIYO HUU. CHAGUA KIONGOZI AMBAYE NI MZALENDO, TUWAPE NA VYAMA VINGINE TUONE! JUST FIVE OR TEN YEARS!
 
Back
Top Bottom