Sifa za mshabiki wa UKAWA

Sifa za mshabiki wa UKAWA

Jifunze kuheshimu mawazo ya wengine, na ujifunze kuwa sikila asiyekubaliana na lowassa ni ccm, kama serikali ingekuwa na mawazo kama yako leo ingekuwa hakuna upinzani, wewe kama unaona sawa kwa hilo ni juu yako, lakini huwezi kulazimisha kila mtu afanane mawazo na wewe

Nilidhani utakuja Na sifa za shabiki wa CCM.
 
Wako Tayari kubadirika na kusahau
Wana Amini yeyote anaye jiunga na Ukawa basi sio fisadi Tena
Wana Amini Fisadi ni Ccm pekee
Wana Amini Mabadiriko yanaletwa na mwana ccm aliye bobea
Wana Amini mtoto wa nyoka hang'ati

Na ndiyo sababu wenye akili sana(walioiba mitihani ya sekondari) wakaamua kucopy na kupaste nembo yao ya M4C
 
Jifunze kuheshimu mawazo ya wengine, na ujifunze kuwa sikila asiyekubaliana na lowassa ni ccm, kama serikali ingekuwa na mawazo kama yako leo ingekuwa hakuna upinzani, wewe kama unaona sawa kwa hilo ni juu yako, lakini huwezi kulazimisha kila mtu afanane mawazo na wewe

Sawa mkuu nimekuelewa vizuri kabisa, naheshimu hisia zako. Shida kuna wengine huku tumepata taabu sana kutokana na serikali ya hawa watu ndo maana tunahisia mbaya sana dhidi yao. Lakini nimekuelewa na ninaheshimu maamzi yako
 
Usipokubali wewe mke wako au watoto au ndg zako watakubaliana na mabadiliko kupitia Lowassa
Khaa!! Na hii ndiyo sifa kuu juu ya Imani ya mwanaukawa. Utadhania anawajua hao ndugu zako :glasses-nerdy:
 
Tujiandae kupiga kura october 25 kila.mwenye harufu ya ufisadi,kashfa,anyimwe tu,na apigwe tu kwani usafi,wajibikaji iwe ndicho kipimo cha mgimbea bora siyo ushabiki bila kujiuliza yeye ni nan alifanya nini kwa nini
 
14. Wana uwezo mzuri wa kufikiri, lakini wanapenda kufikiriwa na Viongozi wao.
15. Hodari wa kula MATAPISHI YAO.ao
16. Wasomi ambao wanadanganyika kirahisi.
17. Wanauwezo kuwafichua Mafisadi wa vyama vingine, lakini wao wanaunga mkono kuongozwa na Mfalme wa mafisadi.

15 sifa nyingne ukiongelea na kuponda kiongozi fisadi hata kama hauna chama jiandae kutukanwa
 
Khaa!! Na hii ndiyo sifa kuu juu ya Imani ya mwanaukawa. Utadhania anawajua hao ndugu zako :glasses-nerdy:

Siamini kama ndg zako wote wanaweza kukengeuka kiasi hicho hadi kuanza kushabikia ccm kwa sasa. Kama utaweza kafanye random sampling ya watu kumi au panda Hiace hoji au katika familia zenu huko utagundua kwamba yawezekana wewe pia ni kikwazo hata kwa wengine katika mabadiliko ya kweli.
 
Lowassa ndio tumaini pekee la watanzania. Lazima tumkabidhi nchi. Hatuna namna nyingine.
 
Mkuu kupitia post hii utapata sifa kibao za wana ukawa ambazo ujazitaja subiriii... .......
 
Sijawahi kumkubali magufuli wala lowassa, ccm ni katika shetani nalotamani lifutike duniani kabisa, nachopingana nacho kwa sasa, kuwatumia wale wale waliotusababishia matatizo hayo hayo,

Halafu wanakuja kwa ulaghai kwamba wao ndo wenye mabadiliko bora walikuwa wapi siku zote hata sasa waje na meneno matamu.
 
Siamini kama ndg zako wote wanaweza kukengeuka kiasi hicho hadi kuanza kushabikia ccm kwa sasa. Kama utaweza kafanye random sampling ya watu kumi au panda Hiace hoji au katika familia zenu huko utagundua kwamba yawezekana wewe pia ni kikwazo hata kwa wengine katika mabadiliko ya kweli.
Khaa!! Kila mtu anataka mabadiliko mazuri kila siku. Lakini anataka mabadiliko positive na si mabadiliko hayo ambayo hadi leo mimi na wewe hatujui kesho itakuwaje. Jitendee haki na kisha tumia akili kidogo KUPENDA MABADILIKO SI KUPENDA UKAWA/LOWASSA :glasses-nerdy:
 
Yote umesema sawa kabisa, lakini kwa kutaka mabadiliko kwa kupitia kwa lowassa hilo ndio nakataa kabisa, Lowassa ndio mmoja wa waliyoyatengeneza hayo matatizo, eti Leo ndio awe tiba?
Sikubali kabisa hilo

Ni kweli Lowassa ndio alioyatengeneza hayo matatizo yote, ni hatua gani mmemchukulia mpaka leo?
 
Khaa!! Kila mtu anataka mabadiliko mazuri kila siku. Lakini anataka mabadiliko positive na si mabadiliko hayo ambayo hadi leo mimi na wewe hatujui kesho itakuwaje. Jitendee haki na kisha tumia akili kidogo KUPENDA MABADILIKO SI KUPENDA UKAWA/LOWASSA :glasses-nerdy:

CCM mlibaki kwenye bunge la katiba, ile ilikuwa ni nafasi ya pekee kutunga katiba yenye kubeba mabadiliko wayatakayo wananchi, lakini kwa kutumia wingi wenu vibaya mkatengeneza katiba itakayohakikisha mnabaki kuitawala nchi hii. Sasa sisi wananchi tunataka tufanye mabadiliko yetu kwa njia ya box la kura mnajifanya kutujia na nyimbo zisizo na kichwa wala miguu. Kaeni pembeni mmechoka na hamjui wananchi wanataka mabadiliko ya aina gani mmebaki kuiga ya wapinzani tu.
 
Back
Top Bottom