Demokrasia na Uhuru wetu Vs Uzalendo na Wajibu Wetu

Azizi Mussa

JF-Expert Member
May 9, 2012
9,172
7,428
"Binadamu tunajua mengi. Asiyejua hili anajua lile. Hata hivyo kama kila anayejua atakuwa akikisema kila anachokijua kumuambia yeyote, mahali popote kwa madhumuni yeyote yale hata kama ni mazuri, tutajishusha katika hadhi duni mno kana kwamba hatukupewa akili hata kidogo".

Demokrasia na uhuru wa mwanadamu kwa ujumla wake una misingi yake.Hilo ni jambo linalofahamika dunia nzima na kuzingatiwa na jamii ya watu wote waliostaarabika. Kadhalika wanadamu tumepewa akili ili tuweze kutathmini mambo kulingana na wakati na mazingira.Kufikiri kwamba kwa sababu ya demokrasia na uhuru wa mtu, basi anaweza kufanya au kusema chochote kwa yoyote na mahali popote na kufikiri kuwa huo ndio utarajibu unaoweza kuleta tija kwa mtu binafsi au kwa taifa ni kukosa uzalendo na kuamua kutokuwajibika.

Unaweza ukawa unaongea ukweli au unatoa ushauri wa maana lakini kama utautoa kwa hadhira isiyostahili, au kwa namna isiyostahili, jambo unalolifanya haliwezi kuwa na maana yeyote. Kwa mfano: kama wewe ni mwanamke na mumeo haogi wiki nzima, unafikiri ni kila mtu anapaswa kulijua hilo kwa kuwa una uhuru wa kuongea na kutoa habari na kwa sababu hiyo unatakiwa umuenye kupitia media? unafikiri utakuwa umeisaidia familia!

Hivi ni mantiki gani inayofanya isikubalike kutoa mambo ya ndani nje ya nyumba au mambo ya kikao chochote nje ya kikao n.k?Nafikiri mantiki ni kwamba ni kwa kuwa si kila ambacho mtu anakijua ni lazima akiseme na si kila mtu anayepaswa kuambiwa kila kitu , popote na wakati wote! au sio?.

Katika level , ya nchi ni vivyo hivyo kwamba pamoja na demokrasia na uhuru wetu, ni lazima Watanzania tuangalie kama tunayoyasema yana umuhimu wa kusema, tunasemea sehemu sahihi, na tunaowaambia ndio tunaotakiwa tuwaambie? vinginevyo tunaweza kujikuta tunawalaumu wengine kwa kutokutimiza wajibu wakati nasi ni sehemu ya wasiotimiza wajibu.Nafikiri kuna aina ya mambo hayahitaji siasa.Hata kama una hitilafu na Mumeo au mkeo, si kila kitu cha familia unatakiwa kuelezea wanakijiji hata kama unajua mengi (ya sebuleni hadi chumbani).Na wala haupaswi kusema kwa kuwa tu una fursa au mdomo wa kusemea bali kwa kuwa ufanyavyo ndiyo ikupasavyo kufanya.

Demokrasia na Uhuru wetu ni lazima uendane na Uzalendo na wajibu wetu na muda kidogo wa kufikiri kabla ya kutenda jambo ni bora kuliko kufanya fatiki ya mwaka mzima.Kama watanzania tunataka maendeleo ya maana, ni lazima tujijengee utamaduni wa kuchukua hatua sahihi, wakati sahihi, mahali sahihi na kwa watu sahihi.Kinyume chake hakuna kitu.
 
kama lengo la Msingi la ACT ni kuirudisha misingi iliyoliasisi taifa (ya Nyerere) ikiwemo uzalendo, uchapaji kazi, uwajibikaji, kujitegemea na kuepuka ubadhirifu wa mali ya umma,haipo sababu ya ACT kuendelea kubaki peke yake peke yake. Ni bora ACT ikatangaza rasmi kuiunga mkono CCM ya magufuli kwa sababu Anachokifanya Rais Magufuli ndicho walichokuwa wanakihubiri ACT wakati wa kuanzishwa kwake. Vinginevyo watawajibika kubadili gia angani ili waweze kujigeuka wenyewe.
 
kama lengo la Msingi la ACT ni kuirudisha misingi iliyoliasisi taifa (ya Nyerere) ikiwemo uzalendo, uchapaji kazi, uwajibikaji, kujitegemea na kuepuka ubadhirifu wa mali ya umma,haipo sababu ya ACT kuendelea kubaki peke yake peke yake. Ni bora ACT ikatangaza rasmi kuiunga mkono CCM ya magufuli kwa sababu Anachokifanya Rais Magufuli ndicho walichokuwa wanakihubiri ACT wakati wa kuanzishwa kwake. Vinginevyo watawajibika kubadili gia angani ili waweze kujigeuka wenyewe.

Kwanza karibu jukwaani, ulipotea sana kaka, Je hiyo ACT inakubaliana kwa asilimia ngapi na kile anachokifanya Magufuli? Je hicho anachokifanya Magufuli kinaungwa mkono kwa dhati na wanaccm wenzake au watu wanaunga mkono hadharani lakini moyoni wanaumia? Nadhani kuna mambo ambayo hao ACT wameshatangaza kumuunga mkono Magufuli lakini sio kila kitu kwani kuna hatari ya wao kupotea kabisa, kumbuka ndio kwanza kilikuwa kinakuwa, sasa kikianza kujichanganya kikiacha kusimama kama chenyewe huenda kikafutika kabisa jambo ambalo sidhani kama lilikuwa lengo lake. Na iwapo ACT itaamua kuingo mkono ccm kwa kila jambo ni baadhi tu ya viongozi wake watapata nafasi ya upendeleo toka ccm, na iwapo Magufuli ataondoka madarakani ni lazima mambo yatabadilika, je ACT itakuwa kwenye hali gani, ama itatafuta mbia mwingine? Na iwapo hali hiyo itatokea itakaa itoboe kweli? Wewe kama wewe sishangai kwa ushauri huu kwani kama ni vyama umeenda vingi hivyo ushauri kama huu kwa ACT siioni kama ni shida ukitoka kwako. Je wana ACT wengine watakubali?
 
kama lengo la Msingi la ACT ni kuirudisha misingi iliyoliasisi taifa (ya Nyerere) ikiwemo uzalendo, uchapaji kazi, uwajibikaji, kujitegemea na kuepuka ubadhirifu wa mali ya umma,haipo sababu ya ACT kuendelea kubaki peke yake peke yake. Ni bora ACT ikatangaza rasmi kuiunga mkono CCM ya magufuli kwa sababu Anachokifanya Rais Magufuli ndicho walichokuwa wanakihubiri ACT wakati wa kuanzishwa kwake. Vinginevyo watawajibika kubadili gia angani ili waweze kujigeuka wenyewe.
Dah ..habari za masiku mkuu ...
 
Watanzania tumekuwa na utaratibu wa ajabu sana. Utaratibu wa mtu au kundi linapoona mtu au kundi lingine linadhulumiwa, tena dhulma za wazi kabisa, basi mtu au kundi ambalo haliguswi moja kwa moja na dhulma hiyo kwa wakati huo, si tu kwamba halimtetei anayedhulumiwa kwa namna yeyote bali hata halifanyi jitihada zozote za kukemea dhulma husika na pengine linaweza kushabikia.

Kwa mfano; kumekuwa na kautaratibu kwa watu wanaona kwa mfano mtu anaibiwa wanaangalia tu, watu wanawekwa ndani kwa dhulma za wazi wengine kimya, watu wanadhulumiwa haki zao mbalimbali wengine kimya. na mifano mingine isiyo na idadi ambayo sipendi kuitaja humu.

Wale wasiochukua hatua yeyote au wanaoshangilia wakati wengine wanadhulumiwa ukiwauliza jibu lao rahisi sana " Kwani Mimi/sisi inatuhusu nini?"

Wewe kaa kimya wakati mwenzako anadhulumiwa, tena dhuluma za wazi kabisa ila tu ujue nawe ikifika siku yako ya kudhulumiwa, na wengine nao watabaki kimya vile vile. Utapiga kelele kuomba msaada lakini hakuna atakayekusaidia.Sana sana wataibuka wanaokukejeli, kushabikia au kuunga mkono jinsi unavyodhulumiwa kama ambavyo nawe ulikuwa unafanya.

Watanzania tujengeni tabia ya kuwa wakweli na kutetea haki hata kama anayedhulumiwa ni mtu wa tatu. "Usiseme tu wanaodhulumiwa au kubaguliwa si wale, mimi si miongoni mwao" hiyo ni dhambi ambayo "Karma" yake ni mbaya sana na itamfika kila mtu kwa wakati wake na katika namna na mazingira ambayo hukuwahi kuyafikiria.
 
Hili ndio jambo bays kabisa ambalo Nyerere alituachia,kukosekana kwa sauti ya pamoja na nguvu ya umma.wengine wanabaki kulalamikia kina Mbowe au Zitto mbona hawasemi juu ya jambo fulani,lakini hawajui kama nguvu na sauti ipo mikononi mwao na wao ndio walioiweka serikali madarakani.tz ni kama kisiwa,hawajifunzi brazil, SA au hata Kenya tu.
 
"Kwanza walikuja kuwadhuru wajamaa, sikusema kitu kwa sababu sikuwa mjaama"

"Kisha walikuja kuwadhuru Wanaharakati na sikusema kitu, kwa sababu sikuwa Mwanaharakati"

"Halafu wakaja kwa Wayahudi na sikusema kitu, kwa sababu sikuwa Myahudi"

"Na hatimaye walinijia mimi na hakukuwa tena na mtu aliyesalia wa kusema kwa ajili yangu"

-Martin Niemoller-

Hatutakiwi kukaa kimya pale tunapoona kuwa kuna jambo haliendi sawa eti kisa tu halituhusu Bali tuseme kadri ya uwezo wetu kwa niaba ya wengine ili siku moja nao waseme kwa ajili yetu.
 
Hali hii imetufikisha kubaya ktk hali ya kufurahiya tunapoona wenzetu wanadhurumiwa.
Hali hii sanasana imeletwa na utawala wa sasa ambapo wananchi wameaminishwa kuwa wafanyakazi wote wa umma ni wezi kiasi ya kwamba wananchi huona umaskini wao umesababishwa na wafanyakazi wa umma kiasi ya kwamba wanachi wakawaida wamejenga wivu dhidi ya wafanyakazi hao.
Leo mfanyakazi akiwa na gari au nyumba wananchi wanaona kuwa ni mwizi, hivyo basi wakisikia mfanyakazi amefukuzwa wao hushangilia bila kujua uharali wa amri hiyo ya kufukuzwa, jambo ambalo ni baya sana na limetutenganisha na kutuondolea umoja.
Serikali inatumia mbimu hii ili kuendelea kututawala. DIVIDE AND RULE
 
DIVIDE AND RULE
mkuu kuna shida kubwa sana na nafikiri ni shida ya kifikra zaidi, kwa mfano wanaolalamikia ajira ni wasio na ajira na wanalalamika peke yao, wanaolalamikia elimu ni wanafunzi nao peke yao,n.k n.k yaani wengine ni kama hawapo vile. Lakini pia kwa mfano wanafunzi wa chuo, nao wanadai ndio wasomi ila nao ukiwaona wanalalamika ujue hawajapata boom lao. wakishapata kimyaa kana kwamba hakuna matatizo mengine ya kijamii ambayo wanatakiwa kuyaadress (kama wasomi?) lakini nao wakililia hilo boom ambalo ni haki yao mwishowe hujikuta wakilia peke yao n.k
 
  • Thanks
Reactions: bne
Ila mbona hatutupani sana, kwa mfano Kamanda wetu Godbless Lema alivyokuwa mahabusu Kisongo, namshukuru Mungu wanachama wote hasa viongozi wa ngazi za juu wa CHADEMA wako naye bega kwa bega hawajamucha muda wote wako Arusha
 
Back
Top Bottom