siasa za jimbo la Arusha mjini: 2010 mpaka 2015.

Stroke

JF-Expert Member
Feb 17, 2012
34,679
40,931
nakumbuka mwaka 2010, oktoba tulifanya uchaguzi mkuu.

jimbo la arusha mjini ambalo mimi nilikua mmoja wa wapiga kura, wagombea kwa nafasi ya ubunge walikua Lema kwa cdm na batilda kwa ccm, mchuano ulikua mkali haswa.

baada ya kufanya uchaguzi tukawa tunasubiri matokeo yatangazwe lakini ghafla zikaja habari kwamba chama flani shiriki kilitaka kuiba kura baada ya mgombea wake kushindwa, watu kwa maelfu wakakusanyika nje ya ofisi za manispaa ya mji kusubiri matokeo.

binafsi nilikuwa mmoja wa wale waliokua wanasubiri matokeo kwa hamu. ili kunasa matukio vizuri nilipanda juu ya mti kama zakayo ili nipate kuona vyema.

umati na tense ilikua kubwa kuwahi kutokea.

ghafla tukasikia kua mtu fulani maarufu toka chama flani kafika pale ili kuokoa jahazi la chama chake; kusikia hivyo umati ulilipuka kwa vurugu ambazo maji ya kuwasha yalitumika kutawanya umati.

baadae matokeo yalitangazwa na mshindi akapatikana: ambapo yule mtu maarufu alikuja baadae kugombea moja ya nafasi za juu kabisa nchini.

baada ya tafakuri nikahitimisha kua siasa hasa za tz sio hasa.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom