Kiranja wa jamii
JF-Expert Member
- Jan 2, 2023
- 963
- 2,195
Tanzania na nchi nyingi za ulimwengu huu zinategemea vyama vya siasa kuzalisha viongozi wa kitaifa
Vyama vya siasa vina siasa ndani ya chama na vina siasa dhidi ya vyama vingine shindani hivyo kuna wakati kwao kipaumbele ni kuyapata madaraka pasipo kujali sana hulka, mitazamo, nguvu, wala uwezo wa huyo atakayeshika hayo madaraka
Kuna wakati kipimo chao huwa ni "nani anakubalika" zaidi kuliko wengine bila kujiuliza sana kwanini mtu huyo anakubalika na ametumia njia zipi hadi yeye kukubalika
Ndiomaa kesi za rushwa, hongo na kila aina ya ushawishi hutumika sana ndani ya vyama na hadi leo vimekosa mwarobaini kwasababu watu hutumia njia mbalimbali ili wakubalike
Jamii isiyo makini inayoendekeza siasa za vyama matokeo yake jamii hiyo itaendelea "kuletewa" viongozi waliokubalika ndani ya vyama vyao bila kujali wamefanya nini kwenye jamii, watafanya nini , wana uwezo gani wa kushughulika na matatizo ya jamii wala kupima uzalendo wao kwa Taifa lao
Najaribu kumfikiria nguli kama Prof. Mark Mwandosya, halafu namuangazia Dr. Salim Ahmed Salim kisha nawalinganisha hawa na Mh. Jakaya Mrisho Kikwete, kamanda na mtumishi wa JWTZ kisha narudi kwenye tafakuri ya nani hasa alistahili "kupewa" u Rais kwa wakati huo ndani ya hao manguli?
Tangu enzi na enzi tumekuwa tukisikia kuwa kuna kitu kinaitwa "vetting".
Kwamba viongozi wakubwa wakubwa wa nchi na taasisi mbalimbali hawawezi kuwa viongozi mpaka wawe "approved" na dawati la vetting lililojaa wakusanya taarifa za nyuma toka utotoni, za sasa na wafanya tathimini wabobezi wa uwezo wa muhusika kulingana na madaraka anayotakiwa kupewa na wabobezi wa ku "project" performance ya muhusika
Tukirejea kwenye simulizi za Mh. Balozi Polepole za hivi karibuni kabla hajatwaliwa zilizomuhusisha Mh. Mstaafu na kundi lake likiongozwa na Ndugu Azizi na tuhuma zote alizokuwa anazitoa ambazo zilipelekea ndugu Azizi kuja hadharani kuzisemea
Iliwezekanaje dawati la vetting liliweza kusema huyu ndiye mbele ya hao wengine?
Ukiniuliza mimi nitasema kuwa pengine hili dawati halina nguvu ya kuingilia siasa za vyama vya siasa vya nchi hii ndiomaana nasema vyama vina vigezo vyao ambavyo hili dawati haliruhusiwi kuvitengua?
Nadhani ni wakati sasa ili jamii ipate viongozi bora, dawati liwe na nguvu kuliko siasa za vyama
Vyama vibaki na wanachama lakini linapokuja swala la kunyofoa viongozi ndani ya hivyo vyama dawati lipewe nafasi kubwa ili kuendelea kulinda nguvu zao
Vyama vikiendelea kubaki na nguvu hizi zilizonavyo lazima vitaitawala dola. Vyama vibaki kuwa chini ya dola ili dola ibaki kuwa na nguvu ya kuvisimamia na kuviongoza kufuata mwelekeo wa nchi
Nimewakumbuka sana Prof. Mark Mwandosya na Dr. Salim Ahmed Salim
Vyama vya siasa vina siasa ndani ya chama na vina siasa dhidi ya vyama vingine shindani hivyo kuna wakati kwao kipaumbele ni kuyapata madaraka pasipo kujali sana hulka, mitazamo, nguvu, wala uwezo wa huyo atakayeshika hayo madaraka
Kuna wakati kipimo chao huwa ni "nani anakubalika" zaidi kuliko wengine bila kujiuliza sana kwanini mtu huyo anakubalika na ametumia njia zipi hadi yeye kukubalika
Ndiomaa kesi za rushwa, hongo na kila aina ya ushawishi hutumika sana ndani ya vyama na hadi leo vimekosa mwarobaini kwasababu watu hutumia njia mbalimbali ili wakubalike
Jamii isiyo makini inayoendekeza siasa za vyama matokeo yake jamii hiyo itaendelea "kuletewa" viongozi waliokubalika ndani ya vyama vyao bila kujali wamefanya nini kwenye jamii, watafanya nini , wana uwezo gani wa kushughulika na matatizo ya jamii wala kupima uzalendo wao kwa Taifa lao
Najaribu kumfikiria nguli kama Prof. Mark Mwandosya, halafu namuangazia Dr. Salim Ahmed Salim kisha nawalinganisha hawa na Mh. Jakaya Mrisho Kikwete, kamanda na mtumishi wa JWTZ kisha narudi kwenye tafakuri ya nani hasa alistahili "kupewa" u Rais kwa wakati huo ndani ya hao manguli?
Tangu enzi na enzi tumekuwa tukisikia kuwa kuna kitu kinaitwa "vetting".
Kwamba viongozi wakubwa wakubwa wa nchi na taasisi mbalimbali hawawezi kuwa viongozi mpaka wawe "approved" na dawati la vetting lililojaa wakusanya taarifa za nyuma toka utotoni, za sasa na wafanya tathimini wabobezi wa uwezo wa muhusika kulingana na madaraka anayotakiwa kupewa na wabobezi wa ku "project" performance ya muhusika
Tukirejea kwenye simulizi za Mh. Balozi Polepole za hivi karibuni kabla hajatwaliwa zilizomuhusisha Mh. Mstaafu na kundi lake likiongozwa na Ndugu Azizi na tuhuma zote alizokuwa anazitoa ambazo zilipelekea ndugu Azizi kuja hadharani kuzisemea
Iliwezekanaje dawati la vetting liliweza kusema huyu ndiye mbele ya hao wengine?
Ukiniuliza mimi nitasema kuwa pengine hili dawati halina nguvu ya kuingilia siasa za vyama vya siasa vya nchi hii ndiomaana nasema vyama vina vigezo vyao ambavyo hili dawati haliruhusiwi kuvitengua?
Nadhani ni wakati sasa ili jamii ipate viongozi bora, dawati liwe na nguvu kuliko siasa za vyama
Vyama vibaki na wanachama lakini linapokuja swala la kunyofoa viongozi ndani ya hivyo vyama dawati lipewe nafasi kubwa ili kuendelea kulinda nguvu zao
Vyama vikiendelea kubaki na nguvu hizi zilizonavyo lazima vitaitawala dola. Vyama vibaki kuwa chini ya dola ili dola ibaki kuwa na nguvu ya kuvisimamia na kuviongoza kufuata mwelekeo wa nchi
Nimewakumbuka sana Prof. Mark Mwandosya na Dr. Salim Ahmed Salim