Siasa na mbinu zake chafu

Masika

JF-Expert Member
Sep 18, 2009
723
30
Habari wadau!

Hivi ni nani atakae tunga sheria ambayo itamkandamiza mwenyewe?
Ni swali nnalojiuliza baada ya kuona malumbano ya chadema na ccm kuhusu mchakato wa kuandaa katiba!
Kwa hali ya kibinadamu lazima katiba inayoandaliwa iwe na upendeleo kwa ccm hata kama wananchi watashirikishwa kwa sababu naamini hakuna atakaeanda taratibu au sheria ya kumbana mhusika kwa hiyo ni halali
kuwa na mtafaruku kwenye mchakato huo,mwenye nguvu mpishe lakini ni hatari sana!

Pia, fairness haitakuwepo mpaka pale mkuu wa nchi atakapokua chini ya sheria na si juu kama ilivyo sasa,angalau ashtakiwe baada ya kumaliza kipindi cha uongozi wake!
Naamini katiba itakayoundwa itazingatia mambo mengi mazuri lakini ni vigumu kuepuka upendeleo wa serikali inayosimamia uundwaji wake,as per human perspective.

Na pia ukishapata uraisi kwa kipindi kimoja tu usiruhusiwe kugombea tena,hii itapunguza uundwaji wa makundi au uongozi wa kupeana/kifalme

huu ni mtizamo wangu tuu sijui mnasemaje karibuni tuchangie
 
Back
Top Bottom