Siasa Chafu Tanzania Inadidimiza Taifa!

Siasa Chafu Tanzania Inadidimiza Taifa!

Mangisandy

JF-Expert Member
Joined
Apr 23, 2012
Posts
2,644
Reaction score
2,273
Nasikitishwa sana na taifa langu, kwa sababu ya utamaduni wetu wa kujisafisha kwa kuonesha uchafu wa tunao shindana nao! Badala ya kukubali kosa na kujirekebisha, unamwonyesha kosa lake pia!

Uozo wa chama fulani au mwanasiasa fulani hautakatishi uchafu wa mpinzani wake, kwanini tunakimbilia kulinganisha maovu yetu?? Kwanini tunawekeana 'hakiba' ya rekodi mbaya na kusubiri kulipuana??

Mikakati hii michafu inatuchelewesha kufikia taifa bora tunalotaka.

Naiombea Tanzania, Mungu ibariki Tanzani, utufungue macho kuona hizi layers za uchafu, na kupambana nao.

Tanzania safi inawezekana, change ni wewe, amka Mtanzania.
 
Si wote ndani ya jukwaa hili tu kwa ajili ya kutimiza ushabiki bali tupo kutafiti na kujifunza. Tunataraji ktk hili kukutana na fikra zilizopevu. Kwa kiwango kikubwa unakuta mtu ktk upevu wake anakazana kuzungumuzia uzinzi, sura, tabasamu, mapenzi, nk, vya mtu fulani. Habari binafsi za fulani. Unajiuliza ni kwa kiwango gani mtanzania wa kawaida kwa hayo anatetewa? Unajiuliza ni nn madhumuni, malengo ya huyu bwana? Unashindwa kupata anafananisha na malaika gani ambao sio kama hao? Ni kuwa alitaka nafasi hiyo iwe ya kwake? Babake? Mjombake? Au nani? Mbona hawatutajii tukawalinganisha na hao wanao watuhumu? Hayo ndio wanaona kuwa ndio fikra pevu? Sisi humu hatutoi cv zetu, mnadhani tunapimanaje akili, elimu na uwezo km si kwa jinsi tunavyochangia? Kwa nn wasomaji wawe na mawazo kuwa ww ni kilaza wakati una elimu nzuri. Umezaliwa na kulelewa vizuri bali unaharibiwa tu kw sababu uzijuazo ww. Yaani unakuwa huna dira na dhima. Ninaomba mtaje matarajio yenu kwa kila mtakachopanga kuwakilisha hapa. Nawakilisha.
 
nimekuwa mara kwa mara nafuatilia vyombo mbalimbali vya habar pamoja maongez ya mitaani ya wananchi kikubwa zaid nimegundua watanzania wengi wanapenda kuendeshwa na matukio ya kila siku leo mazungumzo ya mtaani ni juu yazitto na chadema na kesho akija Obama zitaanza hadithi za ndege ya Obama na ulinzi.tukumbuke jaman kuna mambo yamsing kama baadhi ya watoto wetu wamechaguliwa kidato cha kwanza na hakuna vyumba vya madarasa.hebu ndugu zangu tuachane na kuendeshwa na matukio yasiyo natija kwa taifa kama haya ya akina zitto
 
ni stage tu kuelektea huko unako tamani...cwajua maendeleo ni hatua? watoto wa wajukuu wetu watakuwa wameuona huo mwanga...sisi tupo kwenye stage ya ujima bado....hatuna muda wa kutafakari mambo kiundani....
 
Tatizo letu ss watz kwanza kabisa tuna tatizo la elim ya vieti na sio ya kujitambua ndio maana tunafanya vitu kwa mataarajio na sio uharisia wa mambo. Kuna kundi kubwa la watu wanajiita wasomi na wengine kwa uwezo wao au kwa kusaidiwa wanakabidhiwa majukum ambayo hawaendani nayo wala hawalingani nayo kwakila kitu matokeo yake ndio hapa tulipo fika sasa. Mfano wewe ni Tabibu ambae huna sifa wala vigezo vya kua Tabibu ukapewa majukum wakati huo niwazi kua kama huna sifa wala vigezo hutoweza kutimiza wajibu ulio pewa je muathirika wa huo upuuuzi wako ni nani? Je ww Tabibu usie na vigezo wala sifa utatumikia kwa kipindi gani? Na nani mwenye kukuwajibisha?
 
Ni muda mrefu kidogo nimekuwa nje ya jukwaa hili ila kwa sasa nimeamua kuingia tena rasmi na kusema yaliyo moyoni

Kwa Leo niongelee watanzania wengi kuendesha mambo yao kishabiki na kutokuelewa nyakati za kufanya hivyo .ushabiki huu unachangiwa sana na vyombo vya habari either kwa kuwa na wahariri wasioelewa mchango na madhara ya uandishi wai au kwa kutokujua role yao katika jamii

Wakati nchi ilipokuwa kwenye sakata la kuilipa richmond mabilioni ya pesa kwa amri ya mahakama,huku waziri mkuu akitoa kauli kuwa haikwepeki kuilipa richmondi alizuka babu wa loliondo vyombo vya habari vikampa umaarufu mkubwa na kutupozea dira wote tukahamia loliondo la richmond likapita mpaka Leo wengi hatujui kuwa walilipwa au hawakulipwa ila sasa gharama za umeme ni mwiba mzito kwa kila mtanzani.

Huo ni mfano mmoja Tu ipo mingi sana tena sana. Sasa hivi rasimu ya pili ya katiba imetoka ambayo ina maslahi kubwa kwa kila mtanzania ila vyombo vya habari vinampango uleule vimehamia kwa chadema na zito kabwe

hivi mgogoro wa hawa mabwana chadema Vs zito una maslahi gani kwa tanzania ili upewe kipaumbele hivyo na kuacha masuala ya msingi yanayobeba maslahi ya taifa?
 
Chadema wanaendesha mtafaluku katika chama unao potosha wengi vijiweni na wapenzi wachama ...ukiangalia wanazidi kutugawagawa kwa maneno ...na habari za katika jamii forum kujaa nyingi zao ....twawezaq
 
Watanzania kwasasa wale wapenzi wa chama cha chadema..mjisii kuwa ugomvi wa viongozi usije leta ugomvi ya wananchi...mfano kwa sasa ukiangalia ktka jamii forum utaona page ya siasa utaona stori za chadema zimejaa ...sawa lakini tufuate mambo mazuri ya viongozi na sio maneno mabaya yanayo leta ugomvi kwa wanachama...Na viongozi vyama vyetu ni vidogo kama pilitoni lakini wanataka vioongozwe kama vipo ka ndege ...pesa zauendeshaji vyama ni ndogo kuliko tunavyozitumia ...hasa viongozi wajisii wafanyalo...
 
Watanzania kwasasa wale wapenzi wa chama cha chadema..mjisii kuwa ugomvi wa viongozi usije leta ugomvi ya wananchi...mfano kwa sasa ukiangalia ktka jamii forum utaona page ya siasa utaona stori za chadema zimejaa ...sawa lakini tufuate mambo mazuri ya viongozi na sio maneno mabaya yanayo leta ugomvi kwa wanachama...Na viongozi vyama vyetu ni vidogo kama pilitoni lakini wanataka vioongozwe kama vipo ka ndege ...pesa zauendeshaji vyama ni ndogo kuliko tunavyozitumia ...hasa viongozi wajisii wafanyalo...

wazo zuri ufikishaji mbovu,ki ukweli tumekuwa washabiki zaidi kwenye vyama kuliko kwenye dini zetu,hii yote ni kwa sababu mfumo wa vyama vingi ni mgeni kwetu,watu wana chuki na ccm na wanaaminishwa vyama ndio vinawaletea mateso au uokovu,kuondoka kwa ccm hakutabadili maisha ya mtu kama mtu huyo ana fikra mgando hachakariki.Ajabu viongozi wa siasa ni marafiki washabiki ni maadui wanaoombeana majanga na vifo bila kuguswa na utu.
 
kwanini mnapenda kuhamisha mada kwenye migogoro ya cdm,ni lazima migogoro ijadiliwe kwa kina mbona ya ccm mnaifurahia sana.Bunge la katiba litakuwa na wabunge waliopo na watakaoteuliwa na rais wewe utahusika kwenye kura ya maoni,tuache sisi tujadili migogoro ya vyama kwa ustawi wa kisiasa maana pumba na mchele vitajulikana
 
Watu wazima, wasomi kabisa
na watu wanaoonekana kuwa
na busara, wanashinda kutwa
nzima wakihangaika namna ya
kuwazushia wengine tuhuma
za kipuuzi na kujiapiza namna
watakavyoizika CHADEMA.
Nacheka kwa uchungu kila
ninapowaza aina ya viongozi
na wanasiasa sasa hawana
muda wa kutafuta mbinu za
kuinua uchumi wa taifa letu,
njia za kuwafanya Watanzania
waondokane na umaskini,
kuokoa rasilimali za nchi
zinazoporwa usiku na
mchana, badala yake kama
mazuzu wanahangaika na
vyama vya upinzani na
kuendesha siasa za
kuchafuana!
 
The country have short minds leaders. Bahati mbaya mfumo uliotufikisha hapa ni ujamaa. Mambo yanaenda kwa kubebwabebwa tu hata km huna qualities za kuwa kiongozi lakini unakuwa kiongozi wa wenye qualities za kuwa kiongozi. Hii ni ajabu na kweli. Ingekuwa tume practice mfumo wa "you have to qualify in order to earn" yaani capitalism hawa viongozi wapuuzi tusingekuwa nayo
 
Wao adui wao mkuu sio ujinga, rushwa na mengineyo Bali ni CHADEMA...
 
Kwa hali ilivyo sasa, taifa zima na wananchi wake wanahitaji wawe na strong antivirus software kwenye kila sekta; maana hv ninavyoandika hapa leo ama kesho nikipata opportunity ya kuwa kiongozi i will do the same kama wao walivyofanya ama mm nitafanya zaidi yao. Kwann? Kwa sababu nafsi yangu imeshejengewa hvyo na hawa walioniongoza miaka yote walioniongoza. Sio kosa langu, ni la walezi(viongozi) mm ningejuaje ufisadi km sio wao!
 
Back
Top Bottom