Lekachonka
Member
- Dec 17, 2016
- 35
- 17
Kila mtu amekuwa akitoa maoni yake kulingana na mtazamo wake kisiasa kuhusu Zimbabwe ya Mugabe na hapa kwetu Tanzania.
Kuna wanaohusisha moja kwa moja ZANU-PF na CCM na wapo pia wanaomlinganisha Rais Mugabe na Rais Magufuli,lakini pia wapo wanaolinganisha hayo mambo ya Rais Mugabe na mwenyekiti wa CHADEMA, Mh. Mbowe.
Ukisoma na kusikiliza hoja za pande zote,unaona zimejaa ushabiki tu wa kisiasa na hamna hoja ya maana waliyonayo. Hii inaonesha kwa kiasi gani tulivyo wavivu wa kusoma na kufuatilia kwa makini matukio makubwa yanayoendela duniani.
Ya Zimbabwe tuwaachie wazimbabwe, japo yametuachia cha kujifunza kama vyama,serikali na Taifa kwa ujumla.
Ukifuatilia watu makini,unamwona Rais Museveni tayari keshachukua hatua katika serikali yake kufuatia mkasa huu wa Zimbabwe. Na naamini vyama vingi hasa vikongwe Barani Afrika vitazidi kuchukua hatua sahihi kuhusu hili sakata.
AFRIKA NI MOJA,TUZIDI IOMBEA ZIMBABWE IPITE SALAMA KATIKA KIPINDI HIKI.
Kuna wanaohusisha moja kwa moja ZANU-PF na CCM na wapo pia wanaomlinganisha Rais Mugabe na Rais Magufuli,lakini pia wapo wanaolinganisha hayo mambo ya Rais Mugabe na mwenyekiti wa CHADEMA, Mh. Mbowe.
Ukisoma na kusikiliza hoja za pande zote,unaona zimejaa ushabiki tu wa kisiasa na hamna hoja ya maana waliyonayo. Hii inaonesha kwa kiasi gani tulivyo wavivu wa kusoma na kufuatilia kwa makini matukio makubwa yanayoendela duniani.
Ya Zimbabwe tuwaachie wazimbabwe, japo yametuachia cha kujifunza kama vyama,serikali na Taifa kwa ujumla.
Ukifuatilia watu makini,unamwona Rais Museveni tayari keshachukua hatua katika serikali yake kufuatia mkasa huu wa Zimbabwe. Na naamini vyama vingi hasa vikongwe Barani Afrika vitazidi kuchukua hatua sahihi kuhusu hili sakata.
AFRIKA NI MOJA,TUZIDI IOMBEA ZIMBABWE IPITE SALAMA KATIKA KIPINDI HIKI.