JMP Mchungu
Member
- Jun 30, 2015
- 49
- 127
Hizi story za kahawa na kashata.Wengi wetu tunajua kuwa mataifa yenye nguvu na teknolojia za kijeshi na kivita ni Marekani,Urusi na China! ila ukweli wengi mtakubaliana nami kuwa taifa lenye teknolojia kubwa zaidi duniani ni Israel! hili ni taifa ambalo lipo kimya sana lakini hakuna awezaye kujikanyaga! wengi mtakubali kuwa Marekani anategemea teknolojia za vita kutoka Israel ndo kinachompa nguvu na jeuri kubwa!
Ushahid wa unayo ongea?Wengi wetu tunajua kuwa mataifa yenye nguvu na teknolojia za kijeshi na kivita ni Marekani,Urusi na China! ila ukweli wengi mtakubaliana nami kuwa taifa lenye teknolojia kubwa zaidi duniani ni Israel! hili ni taifa ambalo lipo kimya sana lakini hakuna awezaye kujikanyaga! wengi mtakubali kuwa Marekani anategemea teknolojia za vita kutoka Israel ndo kinachompa nguvu na jeuri kubwa!
Mkuu hivi kweli hapo hujatupiga chai mkuu?Huyo Israel mpaka leo hii ukisema Ulaya na Usa wakisema wasimpe msaada wowote yaani abaki yeye kama yeye halafu jeshi la Hezbollah lipewe silaha kamili mbona atapakimbia hapo mashariki ya kati kumbuka Anwar El Saadat alisema hakuna haja ya kupigana na Israel maana kila majeshi yao yalivyokuwa yakizidi kusonga mbele walikuwa wanakutana na Majeshi ya ITALY GERMANY FRANCE UK USA CANADA akaona bora tu itumike Diplomasia kumaliza mgogoro baina ya Israel na Misri kilichofuata ikaonekana Anwar kawasaliti wenzake
Umetoka kuvuta bangi ukaingia Google unaona tu mambo yapo kinyumenyume
Upo sahihi kabisa mkuu.Hizi story za kahawa na kashata.
Marekani kila mara anampa msaada Israel wa vifaa vya kijeshi ambapo Israel anavitumia hivyo hivyo au anavimodify.
Eti Israel iko kimya, sasa kama iko kimya wewe umejuaje kuhusu uwezo wake?
Ebu tutajie hizo teknolojia ambazo Marekani anategemea?
Najua utaanza taja wayahudi walioko Marekani ambao wameshiriki au kugundua vitu wakiwa kama raia wa Marekani.
Usisahau Marekani imejumuisha watu wa mataifa mbalimbali pia kuna wanasayansi kule ambao wamegundua vitu vingi chimbuko lao ni china, india, germany, africa, russia etc
Israel ndiyo nchi inayo ongoza kuwa na tecn kubwa dunia kuizidi nchi yeyote,Na kwa kuongeza jeshi la anga la Israel limejaza ndege za kivita za Kimarekani zifuatazo
F-15, F-15E and F-16 na mwaka jana wameongeza ndege za kivita jumla ya 15 aina ya F-35 II ambazo zina telnolojia ya hali ya juu toka Marekani.
Mkuu hizo story tu! mtu ukiwa na technology yako gharama za kutengeneza kitu zinaweza kuwa ndogo zaidi hamna taifa lisilohitaji kuwa na uwezo wake binafsi--kama wangekuwa na uwezo wa kugundua technologia mbalimbali wangetumia uwezo huo toka miaka hiyo kutengeneza vitu vyao wenyeweIsrael ndiyo nchi inayo ongoza kuwa na tecn kubwa dunia kuizidi nchi yeyote,
Israel uchumi wake hauwezi kumwezesha kutengeneza ndege au vifaa vya kijeshi vinavyo hitaji bajeti kubwa, akivumbua techn mpya ya kijeshi anamuuzia marekani, mfano hizo ndege ulizo ziorodhesha hapo juu, ni techn ya Israel, Marekan anainunu wanatengeneza kwa hela zake halafu wanakuja kumuuzia Israel,
Hizo ndege kama hiyo F-15, ikisha fika Israel itaenda kubadilishwa techn yote, mfumo mzima unabadilishwa na kuiboresha, F-15 iliyopo israel na f-15 hiyo hiyo ikiwa Marekani hazifanani kitechnologia
ulisha wahi kujiuliza kwanini Marekani anailinda Israel kuliko kitu chochote?
Bila Israel hakuna Marekani, Marekani inaendeshwa na Waisrael, Marekani anamuhitaji Israel kuliko Israel anavyo muhitaji Marekani...
Hahahaha! Jamaa anatuletea stori za vijiwe vya kahawaMkuu hivi kweli hapo hujatupiga chai mkuu?
Ile vita waarabu walishindwa kwa uzembe wao wenyewe na kutokuwa na umoja otherwise wangeshinda ile vita maana siku za mwanzo waisrael walikuwa washadundwa vibaya kabisa.
Nimeona documentary ya hii vita aljazeera not more than a month ago na makanda na wanajeshi walio hai wa kila upande walikuwa wanafanyiwa interview wanatoa story ya kilichotokea na hakuna aliyesema kukutana na wanajeshi wa canada wala ufaransa wala germany et el