Shule ya Mt. Kibo Yathibitisha Wanawake Wanaweza!, Hawahitaji Upendeleo Wala Viti Maalum!

Pascal Mayalla

Platinum Member
Sep 22, 2008
50,582
113,781
IMG-20170123-WA0008.jpg
Wanawake, wanauwezo wa kushinda chaguzi kuliko wanaume, hivyo hawahitaji tena upendeleo au kutengewa viti maalum!.

Imethibitishwa kuwa wanawake wakijengewa uwezo wa kujiamini, wanauwezo wa kushinda katika chaguzi mbalimbali bila kuhitajika hitaji la upendeleo wa kutengewa viti maalum, kwa sababu wanawake wana uwezo sawa na wanaume na hata kuwazidi wanaume kwenye kila kitu, ikiwemo kwenye siasa na kwenye uongozi.

Uthibitisho huo, umethibitishwa katika uchaguzi wa viongozi wa wanafunzi wa Shule ya Msingi ya Mt. Kibo iliyopo Mbezi Juu jijini Dar es Salaam, ambayo ni shule mchanyiko wa wavulana na wasichana, lakini katika uchaguzi wa viongozi wa wanafunzi wa shule hiyo, uliofanyika mwishoni mwa wiki, nafasi zote za uongozi wa juu, zimeshikwa na wanafunzi wa kike waliochaguliwa kidemokrasia baada ya kuwabwaga wapinzani wao ambao ni wanafunzi wa kiume.

Ushindi huo umewezekana baada ya uongozi wa shule hiyo, kuamua kufundisha somo la demokrasia kwa vitendo, katika azma ya shule hiyo kutekeleza hoja ya “samaki mkunje angali mbichi” kwa kuwafundisha wanafunzi wa shule hiyo, somo la demokrasia ya uchaguzi kwa vitendo, ili kupanda mbegu ya demokrasia kwa wanafunzi wa shule hiyo tangu wangali wadogo.

Mwalimu Mkuu wa shule hiyo, Sebastian Ngimba, amesema, lengo la mafunzo hayo ya demokrasia kwa vitendo, ni kuwafunza wanafunzi hao jinsi demokrasia inavyofanya kazi, tangu wakiwa wadogo, ili watakapo kuwa watu wazima na kuingia kwenye siasa, wawe wamepata msingi imara wa demokrasia tangu wangali wadogo.

Mafunzo hayo yamefanywa kupitia uchaguzi wa viongozi wa wanafunzi kupangwa kufanyika kidemokrrasia kwa kufuata taratibu kama za Tume ya Taifa ya Uchaguzi, NEC, ambapo iliundwa kamati ya uchaguzi chini ya mwenyekiti wa uchaguzi, wagombea wote wakajaza fomu za kugombea, wakapitishwa, wakapiga kampeni za wazi, kisha uchaguzi ukafanyika kwa karatasi za kura zilizochapwa majina ya wagombea na kupigwa kwa kura za siri kupitia masanduku ya kura yanaoonyesha (transparent), kura zikahesabiwa, na matokeo yakatangazwa na washindi kuapishwa kushika uongozi.

Mwenyekiti wa Kamati ya uchaguzi wa shule hiyo Aristides Peter Mugisha amesema wameendesha uchaguzi wa viongozi wa shule yao kwa kufuata taratibu kama za NEC katika kuendesha uchaguzi ambao umefuata kanuni za uchaguzi huru na wa haki. Makamo Mwenyekiti wa kamati hiyo Arieth Albert amesema wameendesha uchaguzi huo kidemokasia hivyo walioshinda, wameshinda kwa haki na kihalali.

Katika uchaguzi huo, nafasi zote tatu za juu za viongozi wa serikali ya wanafunzi wa shule hiyo, zimeshikwa na wagombea wasichana ambao wamewashinda wavulana, katika hali inayoonyesha, watoto wa kike, wakijengewa uwezo wa kujiamini tangu wakiwa shuleni, wanauwezo wa kushindana na wanaume na kushinda, katika hali itakoyopelekea siku zijazo, kutohitajika tena kwa wanawake kutengewa nafasi za upendeleo wa viti maalu, kwa sababu, uchaguzi wao umethibitisha wanawake wanaweza, na wanauwezo sawa na wanaume na wakati mwingine, wanawake wana uwezo wa juu zaidi hata kuwashinda wanaume.

Viongozi hao wapya ambao ni Dada Mkuu Nancy Mary Mtinga, na Dada Mkuu Msaidizi Magreth Musagusa na Mkuu wa nidhamu, Angel Jacob, wamesema wameweza kuwashinda wanaume kwa sababu, shule yao ya Mt. Kibo, wamefunzwa kujiamini kuwa wanawake wanaweza, na wamegombea na wanafunzi wa kiume, wamepiga kampeni na wamewashinda vibaya wagombea wa kiume.

Mwalimu Prosper Shimili amesema wanafunzi wa kike sio tuu wanauwezo wa kushinda chaguzi, hata darasani, kuna wanafunzi wengi wa kike wanauwezo mkubwa kimasomo kuliko wanaume, hivyo wanafanya vizuri kuliko wanafunzi wa kiume.

Mwalimu Doreen Msangi, amesema ili juhudi hizi za kuwajengea wanawake uwezo wa kujiamini zizae matunda, ni lazima juhudi hizo ziazie nyumbani katika level ya familia, kwa wazazi, familia na jamii, ziwape fursa sawa watoto wa kike na wa kiume, sio kuwaambia kazi fulani ni za kike na nyingine ni za kiume.
IMG_1917.jpg
_MG_1863.jpg
_MG_1866.jpg
_MG_1867.jpg
_MG_1872.jpg
_MG_1894.jpg
IMG_1900.jpg
IMG_1929.jpg
IMG_1922.jpg
IMG_1911.jpg
_MG_1941.jpg
IMG_1917.jpg
_MG_1863.jpg
_MG_1866.jpg
_MG_1867.jpg
_MG_1872.jpg
_MG_1894.jpg
IMG_1929.jpg
IMG_1922.jpg
IMG_1916.jpg
IMG_1913.jpg
IMG_1912.jpg
_MG_1941.jpg


Sensa ya watu na makazi imethibitisha idadi ya wanawake ni wengi kuliko wanaume, hivyo kama wapigakura wanawake tuu wangewachagua wagombea wanawake, hakuna wagombea wanaume wangeshinda chaguzi.

NB. Habari hii pia ilitangazwa, kwenye Redio, kwenye TV, kwenye magazeti, kwenye Blogs na You Tube.

9:02
MT. KIBO PRIMARY SCHOOL YAFUNDISHA DEMOKRASIA KWA VITENDO.

 

Attachments

  • _MG_1954.jpg
    _MG_1954.jpg
    29.2 KB · Views: 70
  • IMG-20170123-WA0009.jpg
    IMG-20170123-WA0009.jpg
    112 KB · Views: 69
  • IMG-20170123-WA0010.jpg
    IMG-20170123-WA0010.jpg
    127.2 KB · Views: 66
Hahahahaaa Pascal Mayalla tena!! Naomba ni jaribu ku solve hii Quiz yako!! Kwanza nianze kwa kukumbushia Uteuzi wa Kikatiba uliofanywa na Mh Rais kwa wabunge wa viti maalum na Andiko lako hapa kuhusu SIFA na VIGEZO!! Pili ni kuhusu electoral commitee!! Inauma sana! Yaani inapigwa bao hadi na watoto wa chekechea? Tatizo ni sifa na vigezo! Jumapili njema
 
Hiyo kamati ya uchaguzi iliyosimamia uchaguzi ilikua guru kwa kiwango gani na ilipatikana kwa modality ipi labda tuanzie hapo kwanza
 
Hakuna demokrasia hiyo shule mwalimu mkuu mwanaume Na mwenyekiti wa tume iliyosimamia uchaguzi mwanaume Na wewe mayala uliyeleta hizi habari mwanaume.Mfumo dume tupu hadi kwenye ofisi yako mayala.Lakini pia ulichoandika ni aibu Kwa taaluma ya habari.Hujaweka takwimu angalau ungeonyesha hiyo shule ina wasichana wangapi Na wavulana wangapi ukaweka sasa matokeo MTU aone maana kama shule labda ina wasichana 100 Na wavulana 8 unategemea matokeo yaweje? Waandishi wengi wa habari ukiwemo Mayala ni janga la kitaifa kwenye Tasnia ya habari.Halafu utakuta mnasifiana ujinga utasikia hii habari imeletwa Na mwandishi mkongwe Na nguli Pascal Mayala!!!!!!! Aibu
 
si ndio wewe ulisema tz hakuna wanawake
wenye sifa ya uongozi kipindi mkulu
ameteua wabunge wake

naona kama unaendeshwa na unafiki na
maslai zaidi
hivi kuna muda huwa unajitoaga akili enh?????
 
Hii Akaunti imekuwa hacked , siamini kama Pasco anaweza weka hii bandiko....kama ni yeye basis nchi inatatizo na watu wake zaidi ya ukweli ulivyo
 
Hakuna demokrasia hiyo shule mwalimu mkuu mwanaume Na mwenyekiti wa tume iliyosimamia uchaguzi mwanaume Na wewe mayala uliyeleta hizi habari mwanaume.Mfumo dume tupu hadi kwenye ofisi yako mayala.Lakini pia ulichoandika ni aibu Kwa taaluma ya habari.Hujaweka takwimu angalau ungeonyesha hiyo shule ina wasichana wangapi Na wavulana wangapi ukaweka sasa matokeo MTU aone maana kama shule labda ina wasichana 100 Na wavulana 8 unategemea matokeo yaweje? Waandishi wengi wa habari ukiwemo Mayala ni janga la kitaifa kwenye Tasnia ya habari.Halafu utakuta mnasifiana ujinga utasikia hii habari imeletwa Na mwandishi mkongwe Na nguli Pascal Mayala!!!!!!! Aibu
Kwa vile jambo hilo linajaribu kuweka wazi Uhuru wa demokrasia basi unakuja kwa hasira kabisa na kumshambulia Mayalla kwa maneno makali kama kama kavunja sheria.
Mbona wanaccm munaichukia sana demokrasi?
 
Watoto wadogo huwa hawana dhambi bali Dunia iliyojaa watenda dhambi na watu corrupt hubadilisha watoto na kuwa corrupt
 
si ndio wewe ulisema tz hakuna wanawake
wenye sifa ya uongozi kipindi mkulu
ameteua wabunge wake

naona kama unaendeshwa na unafiki na
maslai zaidi
hivi kuna muda huwa unajitoaga akili enh?????


ndo raha ya lugha ya picha kila mtu anatafsiri yake ukikurupuka ni ngumu kuielewa.
 
Mpaka hapo kwa picha tu ni kuwa jinsia ya kike ni wengi kuliko ya kiume,obviously wanawake wapo wengi na hakika wangeshinda tu!

Pascal Mayalla lengo la thread kweli ni kuonyesha wanawake wanaweza au kutangaza shule?

Tuna mawaziri wanawake wengi na pia tuna makamo wa raisi anayehimiza jogging na kutazama shilawadu na tukiwa pia tumeshawahi kupata spika Mwanamke,kwa nini usitumie hao kujenga hoja yako na kuonyesha utukufu wao?

Je Tanzania tupo tayari kuwa na raisi Mwanamke?
 
Pascal wewe ni kigeugeu sana aka Kinyonga. Hivi majuzi kwenye sakata la Mh Rais kuchagua wanaume sita kwenye Bunge, ulijinasibu na kutetea hoja yako kuwa hakuna wanawake wenye uwezo wa kuteuliwa kuwa Wabunge. Ulipigilia msumari tena kuwa hujaona hapa Tz.

Leo tena umejitokea na kuanza kuzungumza kivyako. Sasa uelewekeje? Au unajaribu kujitakasa?

Au unaitangaza shule?

Rejea uzi wako,
Tuacheni Kumlaumu Rais Kuteua Wanaume, TZ Hatuna Wanawake Wenye Sifa na Vigezo vya Kuteuliwa!
 
Back
Top Bottom