Shule ya Kigoma Sekondary yafungwa

Shule ya Kigoma Sekondary yafungwa

mchemsho

JF-Expert Member
Joined
Jun 8, 2011
Posts
3,230
Reaction score
935
Kuna taarifa kutoka Kigoma kwamba shule maarufu ya Kigoma sekondary imefungwa kwa muda usiojulikana na wanafunzi wote wamerudishwa nyumbani kwa muda usiojulikana. Inasemekana sababu ya mgomo ni wanafunzi kupinga kutoruhusiwa kusoma preparation baada ya saa 5 usiku ambapo umeme huzimwa.

Sababu nyingine ni ufundishaji mbovu wa baadhi ya walimu. Wito: serikali kupitia wizara ya elimu itimize wajibu wake katika sakata hili ili watoto wa maskini wapate haki ya elimu ili kujikomboa na umasikini.
 
awa waha nao... ndo wanataka tujue wanajua kusoma sana au!!!? enzi zetu umeme ukikatika tunafurahi hamna prepo siku hiyo
 
ha ha haaaa wapuuzi kweli hawa, mbona shule zingine saa 4 umeme unazimwa?
 
Jamani msidhalilishe visomo vyenu

Prepo!
Prepal!
 
awa waha nao... ndo wanataka tujue wanajua kusoma sana au!!!? enzi zetu umeme ukikatika tunafurahi hamna prepo siku hiyo
halafu watu wanatoka na madaraja/ divisheni za ukweli,sio wao mpaka wanapewa lifti na serikali
 
by mchemsho;
Kuna taarifa kutoka kigoma kwamba shule maarufu ya kigoma sekondary imefungwa kwa muda usiojulikana na wanafunzi wote wamerudishwa nyumbani kwa muda usiojulikana. Inasemekana sababu ya mgomo ni wanafunzi kupinga kutoruhusiwa kusoma prepal baada ya saa 5 usiku ambapo umeme huzimwa, sababu nyingine ni ufundishaji mbovu wa baadhi ya walimu. Wito: serikali kupitia wizara ya elimu itimize wajibu wake katika sakata hili ili watoto wa maskini wapate haki ya elimu ili kujikomboa na umasikini.





Daaaah mkuu mchemsho hii shule yangu nilisoma hapo form six 2007 naijua vizuri mazingira yake magumu sana kwa kusoma!

Umeme shida sana,
Maji pia shida sana japo ipo karibu sana ziwa Tanganyika! miundo mbinu ya maji mibovuuu mnooo!
 
Last edited by a moderator:
Sikufurahia mgomo uliopelekea shule kufungwa bali nimefurahia kuisikia shule yangu kipenzi ya enzi hizo. Jamani mambo yanabadilika maana enzi zetu umeme wa kutosha, maji masaa ishirini na nne, mazingira yenye miti kibao, staff room ambayo sijawahi kuiona mahali popote.
Jamani Kigoma Secondary a.k.a Livingstone College, enzi hizo hadi raha. Likizo wafungashiwa masurufu, wapi Feruzi Mtika, wapi Ndikumana, wapi Rodrick, wapi Upendo Alex, wapi Deo Katto mzee wa kitu, wapi...
 
Katika hali isiyotarajiwa mkuu wa wilaya ya Kigoma Mjini ndugu Maneno Ramadhani jana alifukuza wanafunzi wote wa shule ya sekondari ya wanaume ya Kigoma baada ya wanafunzi hao kufanya mgomo wa kuukataa uongozi wa shule hiyo.
 
Watu kwa Budjet?yaani wanabania umeme watu wasisiome hawajui kama wengine wametumwa na Kijiji.

Mie nafikiria wangefanya maamuzi ya kuruhusu lile bwalo liwe wazi,hata kama watazima umeme kwenye vyumba.

Bwalo lile ni kubwa sana kuweza Ku accommodate watu wengi sana.
Maana najua mchana watu wanaweza kusoma tu hata kwenye Milima kule juu ya nyumba za waalim au upande wa Magereza,kuna miti na upepo mzuri sana huku ukiangalia Mandhari ya Lake Tanganyika.
Nakumbuka mwaka 1994 wakati nipo Form One pale ndio kipindi mheshimiwa Zitto alikuwa Kaka Mkuu,na timu yake walianzisha mgomo,maana wote walioanzsiha Mgomo walikuwa very bright Shuleni,na walipofukuzwa wote walipasua Form 5 vizuri kwenye shule walizohamia.
Basi siku ya mgomo yaani Polisi walipata tabu sana mwanzo.
Maana tulikuwa tunaenda mlimani,na kuna mawe kule kibaooo,yaani ukiokota tu urarusha,basi Polisi walifanya kupotezea,basi ilifikia mida Field Force waliuzingira ule mlima wote,weee ziliwaka huko za moto balaa.Kula kichapo sana.
Watu wengine kimbia hadi Katonga Fish Market.
 
awa waha nao... ndo wanataka tujue wanajua kusoma sana au!!!? enzi zetu umeme ukikatika tunafurahi hamna prepo siku hiyo
Mbona hii shule inachukuwa wanafunzi kutoka mikoa yote! Kumbuka hii ni High School ya Serkali siyo ya Kata.
 
Mbona hii shule inachukuwa wanafunzi kutoka mikoa yote! Kumbuka hii ni High School ya Serkali siyo ya Kata.

Hao Ma-haters wala usihangaike kujibizana nao ni wabaguzi wakubwa sana. Unafikiri wangegoma kilimanjaro wangekuja hapa kubwabwaja pumba??? Wangekua mstari wa mbele kuwahamasisha wanafunzi kudai haki zao.

Wana roho mbaya sana kwan wakishamchukia mtu basi wanakandia kila kitu kinachomzunguka.

Hizi ndizo siasa nyepesi.
 
Wapi mwl Fredy uthibitishe hili? najua upo maeneo hayo kwa wakati huu utueleze zaidi
 
NIJUAVYO MIMI WENYE MAKOSA NI WANAFUNZI.TATIZO LILIANZA SIKU YA JUMAMOSI USIKU AMBAPO KUNA WANAFUNZI WALITOROKA WAKAENDA FIESTA KATIKA UWANJA WA LAKE TANGANYIKA.WAO WANADAI WALILAZIMIKA KWENDA HUKO KWA SABABU MMOJA WA WANAMUZIKI ALIWEPO KUTUMBUIZA ALIWAHI KUSOMA KATIKA SHULE HIYO NA ALIWAHI KUFIKA SHULENI HAPO AKAWACHANGIA LAKI TATU.
WALIMU WALiPOFANYA UKAGUZI SAA TISA USIKU MABWENINI WALIBAINI WANAFUNZI WENGI KUTOKUWEPO.KWA KUWA WANAFUNZI HAO WATORO WALIJUA KITAKACHOFUATA NI ADHABU KALI,WAKAANZISHA MAANDAMANO WAKIDAI MAMBO MBALIMBALI,LIKIWEMO LA KUWAONDOA WALIMU WA NIDHAMU NA WA BWENI AMBAO NDIYO WALIHUSIKA ZAIDI KUBAINI UTORO HUO.NA waKATAJA KABISA HATA WALIMU WALIOTAKA WABADILI KATIKA NAFASI HIZO.KWA MAONI YANGU HAPA WANAFUNZI WALIFANYA KOSA LA KWANZA KATIKA MKAKATI WAO WA KUJISAFISHA.koSA LA PILI LILIKUWA KUOMBA WAACHWE HURU KUANZIA SAA 2 USIKU HADI ASUBUHI BILA KUKAGULIWA NA WALIMU USIKU ILI WASOME KWA UHURU ZAIDI.
SIKU HIYO YA JUMATATU,MIMI NIKIWEPO,WALIKUBALIWA KARIBIA MAOMBI YAO YOTE ISIPOKUWA LA KUACHWA HURU USIKU NA KUWAWEKA WALE WALIMU WALIOWATAKA WAO KATIKA NAFASI YA NIDHAMU NA BWENI.LAKINI WALIKUBALIWA KWAMBA WALE WALIMU WALIOLALAMIKIWA WATAONDOLEWA.
WAKATI KILA MTU ALIYEKUWEPO KATIKA KIKAO KILE ALIAMINI MAMBO YAMETULIA NA WANAFUNZI WANGERUDI MADARASANI WAKATI MAOMBI YAO YANAENDELEA KUSHUGHULIKIWA, KESHO YAKE,YAANI JANA,WAKAFANYA MGOMO TENA.ALICHOFANYA MKUU WA WILAYA ALIWATANGAZIA TU KUWA SHULE INAFUNGWA HADI WATAKAPOTANGAZIWA.HAKUTAKA KUWASIKILIZA TENA.
MIMI NAAMINI KUWA TANZANIA BADO TUNAHITAJI DEMOKRASIA LAKINI SI KWA KIWANGO CHA JUU HIVYO.BADO TUNA UKAKASI VICHWANI HUMU AMBAO "LAZIMA" IWEPO ILI KUPUNGUZA HIYO KITU MBAYA.
 
Acha uongo FIESTA imefanyika lini kigoma tofauti na ya 2013???
 
Back
Top Bottom