Shujaa amelala, ametuacha imara

Shujaa amelala, ametuacha imara

EllySkyWilly

JF-Expert Member
Joined
Aug 28, 2020
Posts
2,204
Reaction score
2,086
Shujaa hafi, daima huendelea kuishi ndani ya mioyo ya watu kwa kupitia yale mema aliyoyafanya enzi za uhai wake. Ile alama aliyoiacha, namna alivyoyagusa maisha na mioyo ya wengi, kwa kadri alivyouishi uhalisia wake na kuisimamia nafasi yake kikamilifu enzi za uhai wake, hayo ndiyo humfanya mtu aonekane ni shujaa pale anapokuwa ameumaliza mwendo wake wa kuendelea kuishi hapa duniani.

Moyo ulipata ganzi ghafla, miguu ikakosa nguvu ya kuendelea kusimama, huku macho yakiukosa uvumilivu wa kuendelea kuyazuia machozi. Kwa kweli taarifa za kuondokewa na mpendwa wetu, rais wetu, ndugu yetu na mwafrika wa kweli Dkt. J. P. Magufuli, nilizipokea kwa mshituko na masikitiko makubwa sana kama ilivyokuwa kwa watanzania wengine. Hapo ndipo nilipoelewa, kumbe machozi huziwakilisha zile hisia nzito ambazo haziwezi kuonekana au kuelezeka hata kidogo kwa kupitia maneno au matendo yetu.

Nikiwa katika tafakuri na kuangalia mafunzo mhimu ninayoweza kuyapata kutokana na maisha ya mzee wetu Magufuli. Nimejikuta katika maswali haya: "ellyskywilly" tayari mzee wetu ameukamilisha mwendo wake. Enzi za uhai wake aliielewa vyema nafasi yake na akaisimamia kikamilifu kiasi ambacho alikuwa tayari kujitoa kama sadaka kwa ajili ya nafasi hiyo. Wewe nafasi yako ni ipi katika Dunia hii? Ni kwa kiwango gani unaisimamia nafasi hiyo? Maisha yako yana maana gani ikiwa hautaielewa nafasi yako katika duniani hii na kuamua kujitoa kama sadaka kwa ajili ya kuisimamia nafasi hiyo?

Maswali hayo yameongezea uchungu zaidi ndani yangu. Yameongeza kilio moyoni mwangu. Maswali hayo yamenifanya niendelee kuyachimba zaidi maisha yangu na kuangalia umhimu sasa wa kuyafanyia mabadiliko makubwa yenye tija.

Kwako rafiki unayeusoma ujumbe huu! Nafahamu fika kuwa, moyoni mwako kumejaa huzuni nzito kufuatia kifo cha mpendwa wetu. Hapa natamani nawe uingie kwenye tafakuri kama ilivyo kuwa kwangu, uangalie yale mafunzo unayoweza kuyapata kutokana na maisha ya aliyekuwa rais wetu. Usiishie kuumia na kuhuzunika moyoni, bali uhakikishe unaondoka na funzo kubwa la kukusaidia ili uweze kuyaishi maisha yenye tija.

Je, unaielewa vyema nafasi yako ndani ya Dunia hii?
Unataka Dunia ikukumbuke kwa lipi?
Upo tayari kujitoa kama sadaka kwa ajili ya kuisimamia nafasi hiyo?

Ni vyema tufahamu kwamba, Dunia itatukumbuka na kutuenzi kwakuwa tulizielewa vyema nafasi zetu na kuamua kuzisimamia nafasi hizo kwa uaminifu mkubwa. Dunia haitatukumbuka kwa sababu ya magari na majumba ya kifahari tuliyokuwa nayo wala kwa idadi ya starehe tulizozifanya. Dunia itatukumbuka kutokana na juhudi kubwa tuliyokuwa nayo katika kuhakikisha tunazisimamia nafasi tulizokuwa nazo na kuyagusa maisha ya walio wengi kwa kupitia nafasi hizo.

Ielewe nafasi yako na uhakikishe unaisimamia nafasi hiyo kwa gharama zote. Hiyo ndiyo maana halisi ya wewe kuendelea kuwepo katika Dunia hii. Kama ni muimbaji imba kweli kiasi ambacho hata vizazi vitakavyokuja, vikiri kama alikuwepo muimbaji katika Dunia hii. Kama ni mwandishi andika haswa, mpaka vizazi vitakavyokuja miaka elfu baada yako viuone uhai ndani ya maandiko yako. Kama ni mjasiriamali fanya ujasiriamali kwa namna ambayo, uwepo wako utaendelea kuwa na umhimu mkubwa sana katika Dunia hii hata baada ya wewe kuondoka. Kama ni mwalimu fundisha kweli kiasi ambacho mafundisho yako yataendelea kudumu vizazi hadi vizazi. Kwa nafasi yoyote uliyonayo, hakikisha unaisimamia kikamilifu na kuwa tayari kujitoa kama sadaka kwa ajili ya nafasi hiyo.

Kama hauifahamu nafasi yako katika Dunia hii basi itafute. Kumbuka "Hatari kubwa zaidi siyo kifo ila yale bora tunayoyaruhusu yafe ndani yetu wakati huu ambao bado tuko hai" Mzee wetu J.P. Magufuli amelala kishujaa, tuzifuate nyayo zake kwa kujitoa kikamilifu kwa ajili ya kuzitafuta na kuzisimamia nafasi zetu kweli kweli!

RIP JPM tutakuenzi kwa vitendo, umetufundisha kujituma tutajituma baba, hakika uliishika mioyo yetu ikajawa na tumaini la kujituma kufanya kazi, umetufundisha kuwa jasiri tutakuwa jasiri kila tupitapo. Umetufundisha kutafuta maisha ya halali tutafanya hivyo.

Ni mimi "ellyskywilly"
 
Kaondoka na huzuni sanaView attachment 1733328
ikulu_mawasiliano-20210323-0001.jpg
 
Magufuli ni rais aliye wanyonga wanyonge
Bomoa nyumba.
Kufumuka kwa bei sukari cement.
Kutoajiri
Kutokuongeza mishahara
Kufilisi biashara, kuua viwanda,
Kilicho mkasirisha Sana mungu ni kile kitendo cha kuiba kura na kutaka kujiongezea muda wa kutawala eti mitano tena, Mungu akiwa na malaika wakashauriana wakasema ngoja tumkatie umeme kwenye moyo
 
katika vitu nilikua naburudika ni pamoja na yeye
kusimama njian na kutatua kero za watu papo kwa papo yaan haina barua wala mchakato.
1.)kula vitu vya wajasiriamali wadogo kama mahindi,madafu na kahawa.yaan hawa wengime sijawah kuwaona wakinywa hata seuze maji tu ya chupa.
2.)kuwa na taarifa kamili ya eneo analoenda na kuyasolve palepale matatizo yao au maombi yao mfano Temeke waliomba eneo la Tba kumbe walijichanganya aliwakatalia palepale kuliko kuwa mnafik watume barua wakae na hope ya kusubiria majibu hapana anawapa kweli yao palepale kila mmoja anaondoka anajua anaenda kufanya nini
3.) kujua kila senti ya nchi ipo wap na anaipangia matumizi kwa hakika hapa aliwashinda woteeeeeeee.
 
Eeenh Heee!

Magufuli angependwa sana kwa baadhi ya mambo, lakini kukosa ubinaadam na kiburi chake viliharibu mazuri na sifa yake.
kawasaidia walemav amekaa na mama pale ubungo chini ya lami em niambie nan aliwahi kukaa chini na mtu masikin.nyie mlishaombea kifo tuachen wenyewe sasa
 
Shujaa hafi, daima huendelea kuishi ndani ya mioyo ya watu kwa kupitia yale mema aliyoyafanya enzi za uhai wake. Ile alama aliyoiacha, namna alivyoyagusa maisha na mioyo ya wengi, kwa kadri alivyouishi uhalisia wake na kuisimamia nafasi yake kikamilifu enzi za uhai wake, hayo ndiyo humfanya mtu aonekane ni shujaa pale anapokuwa ameumaliza mwendo wake wa kuendelea kuishi hapa duniani.

Moyo ulipata ganzi ghafla, miguu ikakosa nguvu ya kuendelea kusimama, huku macho yakiukosa uvumilivu wa kuendelea kuyazuia machozi. Kwa kweli taarifa za kuondokewa na mpendwa wetu, rais wetu, ndugu yetu na mwafrika wa kweli Dkt. J. P. Magufuli, nilizipokea kwa mshituko na masikitiko makubwa sana kama ilivyokuwa kwa watanzania wengine. Hapo ndipo nilipoelewa, kumbe machozi huziwakilisha zile hisia nzito ambazo haziwezi kuonekana au kuelezeka hata kidogo kwa kupitia maneno au matendo yetu.

Nikiwa katika tafakuri na kuangalia mafunzo mhimu ninayoweza kuyapata kutokana na maisha ya mzee wetu Magufuli. Nimejikuta katika maswali haya: "ellyskywilly" tayari mzee wetu ameukamilisha mwendo wake. Enzi za uhai wake aliielewa vyema nafasi yake na akaisimamia kikamilifu kiasi ambacho alikuwa tayari kujitoa kama sadaka kwa ajili ya nafasi hiyo. Wewe nafasi yako ni ipi katika Dunia hii? Ni kwa kiwango gani unaisimamia nafasi hiyo? Maisha yako yana maana gani ikiwa hautaielewa nafasi yako katika duniani hii na kuamua kujitoa kama sadaka kwa ajili ya kuisimamia nafasi hiyo?

Maswali hayo yameongezea uchungu zaidi ndani yangu. Yameongeza kilio moyoni mwangu. Maswali hayo yamenifanya niendelee kuyachimba zaidi maisha yangu na kuangalia umhimu sasa wa kuyafanyia mabadiliko makubwa yenye tija.

Kwako rafiki unayeusoma ujumbe huu! Nafahamu fika kuwa, moyoni mwako kumejaa huzuni nzito kufuatia kifo cha mpendwa wetu. Hapa natamani nawe uingie kwenye tafakuri kama ilivyo kuwa kwangu, uangalie yale mafunzo unayoweza kuyapata kutokana na maisha ya aliyekuwa rais wetu. Usiishie kuumia na kuhuzunika moyoni, bali uhakikishe unaondoka na funzo kubwa la kukusaidia ili uweze kuyaishi maisha yenye tija.

Je, unaielewa vyema nafasi yako ndani ya Dunia hii?
Unataka Dunia ikukumbuke kwa lipi?
Upo tayari kujitoa kama sadaka kwa ajili ya kuisimamia nafasi hiyo?

Ni vyema tufahamu kwamba, Dunia itatukumbuka na kutuenzi kwakuwa tulizielewa vyema nafasi zetu na kuamua kuzisimamia nafasi hizo kwa uaminifu mkubwa. Dunia haitatukumbuka kwa sababu ya magari na majumba ya kifahari tuliyokuwa nayo wala kwa idadi ya starehe tulizozifanya. Dunia itatukumbuka kutokana na juhudi kubwa tuliyokuwa nayo katika kuhakikisha tunazisimamia nafasi tulizokuwa nazo na kuyagusa maisha ya walio wengi kwa kupitia nafasi hizo.

Ielewe nafasi yako na uhakikishe unaisimamia nafasi hiyo kwa gharama zote. Hiyo ndiyo maana halisi ya wewe kuendelea kuwepo katika Dunia hii. Kama ni muimbaji imba kweli kiasi ambacho hata vizazi vitakavyokuja, vikiri kama alikuwepo muimbaji katika Dunia hii. Kama ni mwandishi andika haswa, mpaka vizazi vitakavyokuja miaka elfu baada yako viuone uhai ndani ya maandiko yako. Kama ni mjasiriamali fanya ujasiriamali kwa namna ambayo, uwepo wako utaendelea kuwa na umhimu mkubwa sana katika Dunia hii hata baada ya wewe kuondoka. Kama ni mwalimu fundisha kweli kiasi ambacho mafundisho yako yataendelea kudumu vizazi hadi vizazi. Kwa nafasi yoyote uliyonayo, hakikisha unaisimamia kikamilifu na kuwa tayari kujitoa kama sadaka kwa ajili ya nafasi hiyo.

Kama hauifahamu nafasi yako katika Dunia hii basi itafute. Kumbuka "Hatari kubwa zaidi siyo kifo ila yale bora tunayoyaruhusu yafe ndani yetu wakati huu ambao bado tuko hai" Mzee wetu J.P. Magufuli amelala kishujaa, tuzifuate nyayo zake kwa kujitoa kikamilifu kwa ajili ya kuzitafuta na kuzisimamia nafasi zetu kweli kweli!

RIP JPM tutakuenzi kwa vitendo, umetufundisha kujituma tutajituma baba, hakika uliishika moyo yetu ikajawa na tumaini la kujituma kufanya kazi, umetufundisha kuwa jasiri tutakuwa jasiri kila tupitapo. Umetufundisha kutafuta maisha ya halali tutafanya hivyo.

Ni mimi "ellyskywilly"
Nimekumbuka kauli moja ya kishujaa kweli kweli: Baki na mavi yako nyumbani kwako
 
kawasaidia walemav amekaa na mama pale ubungo chini ya lami em niambie nan aliwahi kukaa chini na mtu masikin.nyie mlishaombea kifo tuachen wenyewe sasa

Wewe unapopaka wanja unadhani unakufanya kuwa bora sana kuliko ulivyo?

Kama huelewewi niliyoandika kwenye mstari huo, ngoja nikupe tafsiri: maigizo hata siku moja hayamsaidii anayeonyeshwa maigizo hayo kwa lolote zaidi ya kicheko cha sekunde moja.

Au bado huelewi niendelee kukutafsiria zaidi?

Magufuli kwa sehemu kubwa alikuwa ni muigizaji; akigeuka huku anakukandamiza baada ya kuigiza kukuchekesha kwa muda mfupi.
..., ahhh, basi nikuache kwa sababu wewe ni mgumu wa kuelewa.

Na sishangai, kwa maana nikisoma tena mstari mmoja uliouandika hapo juu, ni wazi kwamba ni vigumu sana kumwelewesha mtu kama wewe.

Samahani lakini, sio nia yangu kukudharau au kukuudhi.
 
kawasaidia walemav amekaa na mama pale ubungo chini ya lami em niambie nan aliwahi kukaa chini na mtu masikin.nyie mlishaombea kifo tuachen wenyewe sasa
Kwa hiyo kukaa na walemavu barabarani nayo ni sifa? kwani walemavu siyo watu? Siyo watanzania? Wewe ulitaka akae na akina nani?
 
Wewe unapopaka wanja unadhani unakufanya kuwa bora sana kuliko ulivyo?

Kama huelewewi niliyoandika kwenye mstari huo, ngoja nikupe tafsiri: maigizo hata siku moja hayamsaidii anayeonyeshwa maigizo hayo kwa lolote zaidi ya kicheko cha sekunde moja.

Au bado huelewi niendelee kukutafsiria zaidi?

Magufuli kwa sehemu kubwa alikuwa ni muigizaji; akigeuka huku anakukandamiza baada ya kuigiza kukuchekesha kwa muda mfupi.
..., ahhh, basi nikuache kwa sababu wewe ni mgumu wa kuelewa.

Na sishangai, kwa maana nikisoma tena mstari mmoja uliouandika hapo juu, ni wazi kwamba ni vigumu sana kumwelewesha mtu kama wewe.

Samahani lakini, sio nia yangu kukudharau au kukuudhi.
Nasikia wanatafakari kuahirisha mazishi ili iwe Ijumaa ijayo waendelee kutumbua fedha za umma kwa kuzungusha mwili wa mwenzao kama maandazi ya jana vile yaliyonunulika.
 
kama Maandazi yasiyonunulika. Ni kuzungusha mtaani kwa kwenda mbele.
 
Back
Top Bottom