Danny greeny
JF-Expert Member
- Feb 6, 2014
- 3,856
- 1,645
Leo ni mechi ya Simba SC na Coastal union inayochezwa uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
===
Nukuu Muhimu
===
Nukuu Muhimu
- Timu ya Coastal union kutoka walianza kuandika bao la kuongoza mnamo dakika ya 19 kupitia kwa Sabo kupitia mpira wa adhabu ndogo ambao alifanikiwa kuukwamisha moja kwa moja nyavuni.
- Baada ya kurudi mapumziko Simba wanafanya mabadiliko mawili kwa Awadhi Juma na Hamis Kiiza kuchukua nafasi za Ndemla na Majavi.
- Dakika ya 49 Simba wanasawazisha bao kupitia kwa Kiiza baada ya kuunganisha mpira mzuri kutoka mpira kutoka kwa Ajib.
- Kuelekea lala salama, Simba wanapata kadi nyekundu dakika ya 83 baada ya Lufunga kumuangusha Shiboli katika eneo la hatari hivyo kupata kadi nyekundu na coastal kupata penati.
- Dakika ya 85, Coastal wanaandika bao la pili kwa mkwaju wa penati kupitia kwa Sabo ambae ameandika mabao mawili kwa siku ya leo.
- Mpira umeisha kwa hitimisho la Simba kufungwa magoli mawili kwa moja na Coastal Union.