Shiriki katika Tathmini Fupi Kuhusu Hali ya Haki za Binadamu Tanzania

Shiriki katika Tathmini Fupi Kuhusu Hali ya Haki za Binadamu Tanzania

LHRC

New Member
Joined
Mar 3, 2026
Posts
1
Reaction score
6
LHRC inatarajia kutoa taarifa ya hali ya haki za binadamu nchini kama sehemu ya kazi zake za kila siku.

Ili kufanikisha ubora wa taarifa hii tunaomba maoni yako ya dhati kuhusiana na mtazamo wako kuhusu hali ya haki za binadamu nchini.

Majibu ni ya siri (hayatahusishwa na jina lako) na yatatumika kwa ufanyaji tathmini na uchechemuzi.

Kushiriki kwenye tathmini hiyo bonyeza hapa👇👇

 
BTW, LHRC alieandaa hii survey ameweka ndefu sana. Wabongo wengi wavivu.

Pili, ili swali like serious?
IMG_6773.png

By the way, all the best.
 
Binadamu wanatekwa, wanajeruhiwa, na kuuawa miaka yote hiyo hamjafanikisha la maana la kuzuia udhulumaji wa haki zao za kuishi. Sasa mpo kwa ajili gani?
 
LHRC inatarajia kutoa taarifa ya hali ya haki za binadamu nchini kama sehemu ya kazi zake za kila siku.

Ili kufanikisha ubora wa taarifa hii tunaomba maoni yako ya dhati kuhusiana na mtazamo wako kuhusu hali ya haki za binadamu nchini.

Majibu ni ya siri (hayatahusishwa na jina lako) na yatatumika kwa ufanyaji tathmini na uchechemuzi.

Kushiriki kwenye tathmini hiyo bonyeza hapa👇👇

Tanzania hakuna haki za binadamu. Watu wanaishi kwa hofu. Polisi,Mahakama,bunge,kote hakuna haki. Ni mwendo wa kuburuzwa tu.
 
baada ya tathimini nini way forward?kwa mifumo ilivyo sahivi ni ngume ku exercise haki
 
LHRC inatarajia kutoa taarifa ya hali ya haki za binadamu nchini kama sehemu ya kazi zake za kila siku.

Ili kufanikisha ubora wa taarifa hii tunaomba maoni yako ya dhati kuhusiana na mtazamo wako kuhusu hali ya haki za binadamu nchini.

Majibu ni ya siri (hayatahusishwa na jina lako) na yatatumika kwa ufanyaji tathmini na uchechemuzi.

Kushiriki kwenye tathmini hiyo bonyeza hapa👇👇

kwa maoni yangu na kwa hali ilivyo Tanzania,
heshima kwa haki za binadamu inazingatiwa kwa kiwango cha juu sana na wananchi na dola inafanya kazi kubwa na nzuri sana kuhakikisha matukio ya uvunjifu wa haki za binadamu hayatokei na wananchi wanaishi kwa uhuru, amani na utulivu wakiendelea na shughuli zao za kila siku kwa usalama.

chanagamoto kidogo ni upotoshaji katika kutoa taarifa kuhusu haki za binadamu.
kumekua na porojo, uzushi na upotoshaji wa kiwango cha juu sana dhidi ya uvunjifu wa haki za binadamu usio na uthibitisho, jambo ambalo wakati mwingine huzua taharuki na kuchochea chuki miongoni mwa wananchi kutoka ndani ya vyama mbalimbali vya siasa dhidi ya chama tawala.

kwa ujumla,
serikali ya Tanzania inafanya kazi kubwa na kwa weledi mkubwa katika kuhakikisha haki za binadamu zinaheshimiwa ipasavyo, lakini pia kuanakua na uwazi, usawa na uwajibikaji katika vyombo vya dola katika kuhakikisha wananchi wanapata au kutumia haki zao kwa uhuru bila vikwazo vyovyote na bila kukiuka sheria.
 
Kwenye hiyo tamthilia mm ntacheza kama atakayeuawa kutokana na kukosekana haki za kibinadamu, hvy sitoonekana bali nitatajwa jina tuu kama mmoja kati ya waliouawa na system
 
Kwenye hiyo tamthilia mm ntacheza kama atakayeuawa kutokana na kukosekana haki za kibinadamu, hvy sitoonekana bali nitatajwa jina tuu kama mmoja kati ya waliouawa na system
Kwa hii nchi unaweza kuuliwa kweli kwenye hilo Igizo

Zingatia hilo
 
Back
Top Bottom