Shipping container homes

Graph

JF-Expert Member
Joined
Jul 20, 2016
Posts
2,735
Reaction score
6,170
Nimekutana na hizi nyumba zilizojengwa kwa shipping containers nimezipenda sana.
Very simple and clean design, contemporary houses. Na hata kama sio kwa ajili ya nyumba nadhani inafaa kitu kama a small coffee au chilling area. Kwa anayefahamu bei ya shipping containers kubwa naomba anitajie bei tafadhali na wapi zinaweza patikana Tanzania.



Nadhani tatizo kubwa ni cooling, kwa joto la bongo inaweza kua a huge mess to cool this structure.
 
Hizo nyuba kwa equatorial area sio kabisa. Ikipigwa na mvua halafu jua likawaka inapinda pinda. Jua ni kali sana
 
Hizo nyuba kwa equatorial area sio kabisa. Ikipigwa na mvua halafu jua likawaka inapinda pinda. Jua ni kali sana
toka nipo mdogo napata fahamu hadi leo hii zaidi ya miaka 20 kuna duka jirani na nyumbani limetengenezwa na container 2 na pembeni yake kiwanja hiko hiko kuna kama ofisi zina container nne sijawahi kuziona hata siku moja zikipinda.

labda kuna material tofauti tofauti ya kutengenezea mkuu
 
Now nimeelewa vizuri. Shipping container
 
Container zinapatikana.. 40ft $3000 20ft $2500. Zinauzwa legally na risiti unapata kama uko serious njoo PM
Nijuze tafadhari, hayo makasha yana urefu wa futi 40 na mengine 20. Je upana huwa ni futi ngapi?
 
Nammi nimeiona hiyo kitu nilipohivi sasa wilayani nachingwea Ni ghorofa mbili sehemu moja iitwayo jiwe la mzungu ( calfonia) Niliipenda kwa kweli
 
Hiyo nyumba itadumu hata miaka 500
 
Hizo nyuba kwa equatorial area sio kabisa. Ikipigwa na mvua halafu jua likawaka inapinda pinda. Jua ni kali sana

Mahakama ya mwanzo ya Ilala wanatumia makontena kama nyumba miaka nenda rudi,sijawai kuona yamepinda
 
Mahakama ya mwanzo ya Ilala wanatumia makontena kama nyumba miaka nenda rudi,sijawai kuona yamepinda
Kuna watu nahisi ni wanadamu ya kufeli maisha.....yaani huwa hawafikirii kujenga au kuboresha wao huwa wanawaza kiharibu au kubomoa......ndio huyo sasa anaetupa nadharia za kubomoa bomoa sijui kupinda pinda utadhani alishawahi kujenga ikamfanyia hivyo.....
 
Kontena ikiongezewa Cooling material kwenye kuta zake....au ikowekewa covervya jua kwa juu inakuwa haina joto hata kidogo.......infact inakuwa ya baridi sana ndani....kama unataka kuona mifano......nenda pale eneo la Tabata liwiti (karibu na ofisi za ttcl).....utakuta tanesco wametumia hiyo style kujengea office zao na iko poa tu.....sidhani hata kama kuna tatizo la joto.......
 
Kwa hapa tanzania kuna mafundi ambao wana uwezo wa kudesign interior na exterior kama kwenye hizo picha??
 
hili wazo la hizo nyumba nimelipenda bure kibongo bongo inaweza kucost Tsh ngapi ili niwe namiliki kitu kama hicho?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…