Shinyanga Mjini Vs Tabora Mjini

Mleta mada ameongelea Taboa mjini na Shy mjini, ajabu watu wanaleta hbr za Kahama na Nzega mara Kishapu mara Igunga.

Tabora ipo vizuri kuliko Shy, maendeleo ni makubwa kwenye kila nyanja mfano miundombinu kama barabara zimeboreshwa sana, Tabora walipata udhamini wa World Bank wakatengenezewa barabara za mitaani toka mwaka juzi.
Nimeambiwa pia lami ya Tbr-Itigi ipo mbioni kukamilika.

Nimeshangaa mtu anasema Tbr ni semi desert, huyu mtu inaonekana haijui Tbr vzr, mpunga unaweza kulimwa na kustawi eneo la semi desert?

Chakula Tbr ni kingi sana na bei ni chini sana, hoteli zimeongezeka, majumba yanajengwa sana pia.

Kuhusu imani za kishirikina zipo tena kwa miaka hii zimepungua kiasi sababu ya muingiliano wa watu kutoka miji mingine.

Husda, chuki, umwinyi, roho za kimasikini na ushirikina bado zipo hasa kwa wazaliwa wa Tabora.

Tabora mabinti ni wengi na wazuri sana, wanaoana sana na kuachana baada ya muda mfupi na sijui ni kwann!!

Mwisho, nitakuwa sijatenda haki kama nisiposema hili, WAARABU ni wengi sana Tabora na wamezishikilia biashara kwa kiasi kikubwa.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kahama siyo shai mkuu sema shai wapi taa za barabarani?

Sent using Jamii Forums mobile app
Mwezi wa Pili nometoka DOM kwenda MWANZA kwa kukamata gari za DAR kwenda MWANZA nilikamata Ally's ambayo haiingii stand ya shy wanasimama pale Ofisini kwao njia kuu kwenda MWANZA Kuna Taa za barabarani wasukuma wanaserereka tu na baiskeli zao..



Shinyanga ni Pazuri kuliko Tabora kwa kila Kitu naamin kuanzia gharama nafuu za maisha upatikanaji wa uhakika Maji Safi na salama na ajabu gharama za Maji Shinyanga ni nafuu kuliko hata Mwanza na wakati Maji yametoka Mwanza urahisi wa kujengeka hata uchapakazi ule mji wachapa kazi wengi wachaga wamejaa kila eneo na wenyeji baadhi, Tabora uvivu mwingi na uswahili sana ni mji ambao umedumaa hivi japo sijawahi fika (hii Ni kwa mujibu wa Kaka angu aliepo Huko)

Kinachoiponza shy ni asili ya Watu wa mkoa ule ambao hawana makuu kabisa ukiwaita washamba hata hawalalamiki ukiwaita sijui wanazaa Sana hawasemi chochote Yaan Hawa jamaa hawashindwi kuishi na mtu yeyote!!

Typed Using KIDOLE
 
Mkuu umwshusha point tupu, Ila nikueleze tu suala la lami katika miji yetu kwasasa kila mkoa Kama sio yote mijini ni lami tupu nimeona Singida, Sumbawanga na Shinyanga hiyo Ni kila eneo na hapa DODOMA kila kinjia Cha mtaani wametandaza mkeka sio Tabora tu

Typed Using KIDOLE
 
Tzn kuna miji yenye pesa 2 tuu,Dar the mighty na Arusha huko kwenu Mwanza hakuna kitu,ukienda jukwaa la DAR VS NRB utakuta kuna Watz eti wanasema Kenya ni NRB tu wakati kiuhalisia hali ya kukosekana usawa huku kwetu imeidi,wakati zaidi ya75% ya pato lote la nchi linatoka Dar kilichobaki ugawanye mikoa yote huoni hali ilivyo mbaya ya kukosekana kwa uwiano wa maendeleo? shida ni kwamba serikali haikuendeleza maeneo mengine ya nchi ko Dar ikajijenga peke yake
Imagine hadi leo hii hakuna barabara ya kuunganisha mikoa ya Kigoma na Kagera,Kigoma na Tabora,Rukwa na Katavi/Kigoma ,Mbeya na TBR ,Ruvuma na Morogoro etc kwa hali hii unategemea maendeleo gani mikoani?
 
Sasa mbona mnahama kutwa utafikiri wakimbizi mnakimbia nini?

Sent using Jamii Forums mobile app
Mnajui nyie ni ndugu ila mnavyobishana sasa, mmoja wa kusini (DAKAMA) na mwingine wa kasikazini (SUKUMA), ila hoja ya msingi ya uzi huu ni kuangalia fursa zozote zilizopo either Shinyanga au Tabora ambazo zitatusaidia kuangalia namna ya kututoa sehemu moja kwenda nyingine. Ila bahati mbaya naona mjadala umehamia kwenye nani ni nani aka wapi ni zaidi kuliko sehemu nyingine badala ya kutaja fursa mbalimbali zinazopatikana Shinyanga hata kama zipo nyingi kuliko Tabora na fursa zilizopo Tabora hata kama ni kwa uchache.

Mwisho wa siku nyie wote ni ndugu na ndio makabila yanayoingiliana kwa kiasi kikubwa hata ukiangalia majina na mila na desturi.
 
GDP ya dar ni $25B...,ya tz ni $62B.
(25÷62)×100%=40.32%.
Wewe hiyo 75% umeitolea wap?
Au hesabu ndo put water kwako
 
Tabora Mjini! ( Nimekaa Miaka Mitatu Hapo) Ni mji mchangamfu Kuliko Shinyanga Mjini ambako nimeishi zaidi ya miaka 20.
Ni Mji wa Starehe sana Tabora Mjini,Ni mji unaokuwa kwa kasi Kuliko Shinyanga Mjini.
Uchumi wa Tabora Unategemea sana Bidhaa na Chakula Kutoka Shinyanga,Mpanda,Kahama,Bukoba,Mwanza na Mbeya.

Majengo Mazuri yameongezeka Sana Tabora Mjini,Barabara za rami ni nyingi kuliko Shinyanga Mjini.
Wenyeji ni Waswahili sana na kwa sifa hii inaambatana na Uvivu Uongo na Ujanja ujanja! Vibaka ni Wengi sana! Omba Omba Stendi ni wengi sana na Maeneo ya NMB Bank Mihayo.

Shinyanga patulivu sana! Maendeleo ni ya pole pole kwa kweli lakini Uhakika.Maeneo Mazuri Shy ni Makazi ya Watu! Majengo Mapya,Bushushu,Bugweto na Ibinzamata na Ndala Kidogo.

Bei ya chakula kwa Tabora ni cheap sana! Magari ya Vyakula ni mengi sana hapo,Ukifika Soko Kuu pale kuja mpaka Mtaa wa Toronto (Salmin) Fuso Kubwa za Machungwa,Ndizi na Mananasi hazikauki Tabora.

Mnada ni Jumamosi na Jumapili - Mtaa wa Salmin Hufungwa kabisa na watu kuachiwa kufanya biashara zao!
Wakati Shy Mjini walishapigwa marufuku Kuuzia Mtaa wa Sukari - Town School kwenda Nguzo nane.
Mnada Shy ni Jumamosi Ngokolo Mtumbani hauja changamka sana.

Nyumba za wenyeji wa Tabora mjini kati ni za ajabu sana! Nyumba za fito ila zimeanza kupungua kiasi.
Ukiangalia nyumba inasema nikuue au nikusamehe? ila Mwanamke anayetoka humo baraa! Mwanamke mrembo kweli kweli.
Kama mdau mmoja alivyoeleza hapo juu! Harusi kila wakati na taraka hivo hivyo!
Mtaa wa Ng'ambo,Kanyenye na Mwinyi ndo Uswazi kwenyewe na Mwanza Road.

Kimsingi miji hii haijaachana sana lakini Tabora iko mbele kwa mambo mengi!
Kwetu Kanda ya ziwa.
 
Umefanya uchambuzi mzuri
 
GDP ya dar ni $25B...,ya tz ni $62B.
(25÷62)×100%=40.32%.
Wewe hiyo 75% umeitolea wap?
Au hesabu ndo put water kwako
Mkuu hilo jamaa utaliweza basi! Watu wanajadili tabora vs shy lenyewe linaleta mambo ya Dar, Mwanza na Arusha. Yaani lenyewe linapenda kuona mwanza inateseka inakuwa chini sema ndo hivyo badala ya Mwanza kuteseka lenyewe ndo linateseka. Linaamini hata njombe inazidi Mwanza.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Huwa namuona anaipondea sana aisee... Sijui kulimfanya nini huko... Ila mwisho wa siku ndo hivyo huwezi danganya kila mtu hapa Jf.
 
Kama hujafika Tabora huna hata sababu ya kuchangia.Mimi nipo shy hadi sasa,na Tabora naenda mara kwa mara,huwezi linganisha Tabora na Shy.

Tabora ipo juu kwa kila nyanja.Panavutia kuishi kuliko shy.

Huyo kaka yako huenda ndio hao mamwinyi ambao hawajawahi kutembea na hawaoni fursa nyingi zilizopo Tabora. Kama si hivyo basi ni mtumishi wa serikali ambaye amekosa jinsi ya kupiga dili hasa kipindi hiki.Anaweza akawa anatamani kuhamia shinyanga kwa sababu huku bado wafanyakazi wanapiga dili.

Ni wachawi wakubwa ndio maana huwezi kuona ziara ya raisi, waziri mkuu,wala mawaziri wengine hapa shy.Miaka mitano hii inaelekea kuisha hawajakanyaga hapa.Mkoa wenye migodi mikubwa ya dhahabu na almasi
Sent using Jamii Forums mobile app
 
[emoji2][emoji2][emoji2]
 
Hapa naona mnabishans ujinga,
sijaona point ya msingi hata moja.

Africa is shit hole, ukiwa ulaya hata hiyo DAR inaitwa kijiji.

Kuzuri ulaya tu hasa Scandinavia counties bila kusahau Singapore.

Tabora na Shy Ni sikio la kushoto na kulia. TZ sijaona mji uliotulia yote imejaa vibaka tu.

By the way sehemu yoyote wanapoishi binadamu unaeza ishi pia.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…