Shida ni kuwa na Waziri Mkuu anayeutamani Urais

mapessa

JF-Expert Member
Oct 9, 2014
612
1,045
Namtazama waziri mkuu wa awamu ya tano jinsi alivyokuwa akichapa kazi. Jinsi alivyokuwa akisimamia utendaji wa serikali akiongea kwa mamlaka ya nafasi yake.

Nikimlinganisha na huyu wa awamu ya sita nagundua kabisa ni mtu aliyejivua kwa kuwa ana ndoto zaidi ya hapo hataki lawama, hataki kuchafuka hataki kuwa sehemu ya mitihani mingi iliyopo sasa. Japo ni mtu yuleyule mmoja.

Huenda shughuli za utendaji wa serikali zimebadilika siku hizi, shughuli usimamizi na kusema kwa niaba ya Rais na Serikali ambazo kimsingi nj za Waziri Mkuu kama mtendaji Mkuu wa shughuli za Serikali hazina mwenyewe tena.

Tulipaswa kumuona Waziri Mkuu kama sehemu ya kusimamia Serikali akisimamia mijadala na kuhamasisha watendaji walio chini yake kuwa kitu kimoja.

Hii inaonyesha wazi Waziri Mkuu ni mtu anayelipwa mshahara mkubwa, anatuzwa vizuri, anapokea kila aina ya vipaumbele pamoja na kuhakikishiwa kila aina ya msaada kikazi, akiwa hajui tena wajibu wa kazi yake.

Rais amepata Waziri Mkuu anayetamani kuwa Rais akijiandaa na kushindana na wanaotaka urais wengine. Hawezi kukubali kuchafuka kwa niaba ya Rais. kuna kitu Rais Samia anahitaji sasa msaidizi wa kutimiza maono yake.
 
Namtazama waziri mkuu wa awamu ya tano jinsi alivyokuwa akichapa kazi. Jinsi alivyokuwa akisimamia utendaji wa serikali akiongea kwa mamlaka ya nafasi yake.

Nikimlinganisha na huyu wa awamu ya sita nagundua kabisa ni mtu aliyejivua kwa kuwa ana ndoto zaidi ya hapo hataki lawama, hataki kuchafuka hataki kuwa sehemu ya mitihani mingi iliyopo sasa. Japo ni mtu yuleyule mmoja.

Huenda shughuli za utendaji wa serikali zimebadilika siku hizi, shughuli usimamizi na kusema kwa niaba ya Rais na Serikali ambazo kimsingi nj za Waziri Mkuu kama mtendaji Mkuu wa shughuli za Serikali hazina mwenyewe tena.

Tulipaswa kumuona Waziri Mkuu kama sehemu ya kusimamia Serikali akisimamia mijadala na kuhamasisha watendaji walio chini yake kuwa kitu kimoja.

Hii inaonyesha wazi Waziri Mkuu ni mtu anayelipwa mshahara mkubwa, anatuzwa vizuri, anapokea kila aina ya vipaumbele pamoja na kuhakikishiwa kila aina ya msaada kikazi, akiwa hajui tena wajibu wa kazi yake.

Rais amepata Waziri Mkuu anayetamani kuwa Rais akijiandaa na kushindana na wanaotaka urais wengine. Hawezi kukubali kuchafuka kwa niaba ya Rais. kuna kitu Rais Samia anahitaji sasa msaidizi wa kutimiza maono yake.
USISAHAU NA MAWAZIRI WA NISHATI HABARI NA FEDHA WOTE WANAUTAKA SIO KUUTAMANI URAIS
 
Nadhani Wewe mwenyewe umesema "HATAKI KUCHAFUKA"

Rekodi yake inajulikana, shida ninyi hambebeki siku hizi, mnanuka uozo. Mtengueni tu maana akitangaza kujiuzulu itahesabika kuwa ni Utukutu kwa Mteule wake.
Hambebeki. Kazi ya Waziri Mkuu mmewapa Machawa, ishini hivyo tu.
 
Namtazama waziri mkuu wa awamu ya tano jinsi alivyokuwa akichapa kazi. Jinsi alivyokuwa akisimamia utendaji wa serikali akiongea kwa mamlaka ya nafasi yake.

Nikimlinganisha na huyu wa awamu ya sita nagundua kabisa ni mtu aliyejivua kwa kuwa ana ndoto zaidi ya hapo hataki lawama, hataki kuchafuka hataki kuwa sehemu ya mitihani mingi iliyopo sasa. Japo ni mtu yuleyule mmoja.

Huenda shughuli za utendaji wa serikali zimebadilika siku hizi, shughuli usimamizi na kusema kwa niaba ya Rais na Serikali ambazo kimsingi nj za Waziri Mkuu kama mtendaji Mkuu wa shughuli za Serikali hazina mwenyewe tena.

Tulipaswa kumuona Waziri Mkuu kama sehemu ya kusimamia Serikali akisimamia mijadala na kuhamasisha watendaji walio chini yake kuwa kitu kimoja.

Hii inaonyesha wazi Waziri Mkuu ni mtu anayelipwa mshahara mkubwa, anatuzwa vizuri, anapokea kila aina ya vipaumbele pamoja na kuhakikishiwa kila aina ya msaada kikazi, akiwa hajui tena wajibu wa kazi yake.

Rais amepata Waziri Mkuu anayetamani kuwa Rais akijiandaa na kushindana na wanaotaka urais wengine. Hawezi kukubali kuchafuka kwa niaba ya Rais. kuna kitu Rais Samia anahitaji sasa msaidizi wa kutimiza maono yake.
Mwache Majaliwa, Hana HATIA.
 
Cha ajabu hatujawahi kupata rais alietokea kwenye uwazir mkuu tangia nchi ipate uhuru
 
ACHENI KUPIGA RAMLI,KUWA RAIS NI KITU KIMOJA NA KUWATUMIKIA WANANCHI NI KITU KINGINE,INGAWA HAIKATAZWI MTU KUTAMANI,ILA WANGAPI WALITAMANI HATA KUONGEZA MUDA WA U RAIS BAADA YA MUDA WAO KUISHA NA MUNGU AKAWAPENDA ZAID??
 
Namfahamu Kassim Kwa miaka mingi

Toka ktk ualimu,Ubunge,Unaibu Waziri hata au Uwaziri Mkuu.Kwa haiba ya Hayati Magufuri haikuwa ngumu kufahamu uwezo usio na shaka wa Mwl Majaliwa..Nchi hii imekuwa na viongozi mahiri wengi wenye msingi wa ualimu (Hayati JK Nyerere,Mzee Mangula,Mama Mongera,Etc…)

Kulikuwa na Mawaziri wengi seniors lakini akampendekeza huyu ndugu..Utendaji wake Una ushupavu wa kipekee..

Anayo mapungufu kibinadamu na kimfumo ambayo ni kikwazo Kwa wengi wa aina yake..
.Kukua na kupanda kisiasa si jambo baya na ni kiu ya kila mwanasiasa..

Anaegombea ubunge Ana kiu ya Unaibu Waziri au Uwaziri,Diwani anakuwa na kiu ya kuwa mbunge n.K..Vivyo hivyo mawaziri wengi wanatamani kuwa Waziri Mkuu na wanafanya fitina kila kukicha..Makamu wa Rais ikimpendeza Mungu na kikatiba anaweza kuwa Rais hata Kama hakupigiwa kura..Wala kuwa mgombea mwenza..

Mwisho Mungu akikusudia kumpa yeyote Ukuu wa nchi ktk kipindi chochote hakuna awezae kuzuia..Si pesa,Fitna,Faraka wala husuda..

Mh Majaliwa Tenda Kwa haki,Simamia Kweli,Jitenge na biashara,Mche Mwenyezi Mungu..
 
Back
Top Bottom