Kiranja wa jamii
JF-Expert Member
- Jan 2, 2023
- 966
- 2,215
Kwa mfano, nasema kwa mfano!
Tundu Lisu afutiwe mashitaka yanayomkabili, mwanasheria mkuu wa serikali atoe hoja ya kutunga sheria ya kuunda serikali ya mseto, wabunge wote waridhie, Rais asaini halafu wataalamu wakae chini waone nani ana mlengo gani na akae wapi.
Wizara na sekta mbalimbali ziwe chini ya watu wenye itakadi tofauti za vyama lakini zenye mlengo wa kujenga nchi na kuleta maendeleo kwa wananchi. Si ndivyo wanavyojinadi huko? Kwamba tuwape nchi walete maendeleo, sasa tusiwapendelee watu fulani, tuwape wote! Wote si ni watanzania baana?
Tutengeneze dira ya nchi, tuwape vipaumbele vyetu, tuwape KPI za kila sekta, kila idara na kila Wizara kisha tukae pembeni tusubiri matokeo
Halafu baada ya muda hivi kama miaka miwili hali ikishatulia, vichwa vinawaza sawasawa na mihemuko imepoa, liitwe bunge la katiba kisha watu wapite mule mule alikopita Warioba kwa kufanya maboresho na nyongeza kidogokidogo kadiri ya wataalamu watakavyoona na katiba mpya iandikwe
Hivi hamuoni kama Tanzania itaitwa nchi ya mageneus sana? Hamuoni kama tutarudisha heshima tuliyokuwa nayo ukanda wetu wa maziwa makuu, Afrika na dunia nzima kwa ujumla?
Watu hawataamini maana huko waliko wao wanataka tupigane marisasi watucheke! Tuvurugane watukebehi! Tushenyetane wao waje wazoe marasilimali yetu
Tuukwepe huu mtego kwa kuunda serikali ya mseto ambayo itatuletea katiba mpya na uchaguzi huru na wa haki huko mbeleni. Vingenevyo hii hali itakuwa ya kujirudia rudia
Tundu Lisu afutiwe mashitaka yanayomkabili, mwanasheria mkuu wa serikali atoe hoja ya kutunga sheria ya kuunda serikali ya mseto, wabunge wote waridhie, Rais asaini halafu wataalamu wakae chini waone nani ana mlengo gani na akae wapi.
Wizara na sekta mbalimbali ziwe chini ya watu wenye itakadi tofauti za vyama lakini zenye mlengo wa kujenga nchi na kuleta maendeleo kwa wananchi. Si ndivyo wanavyojinadi huko? Kwamba tuwape nchi walete maendeleo, sasa tusiwapendelee watu fulani, tuwape wote! Wote si ni watanzania baana?
Tutengeneze dira ya nchi, tuwape vipaumbele vyetu, tuwape KPI za kila sekta, kila idara na kila Wizara kisha tukae pembeni tusubiri matokeo
Halafu baada ya muda hivi kama miaka miwili hali ikishatulia, vichwa vinawaza sawasawa na mihemuko imepoa, liitwe bunge la katiba kisha watu wapite mule mule alikopita Warioba kwa kufanya maboresho na nyongeza kidogokidogo kadiri ya wataalamu watakavyoona na katiba mpya iandikwe
Hivi hamuoni kama Tanzania itaitwa nchi ya mageneus sana? Hamuoni kama tutarudisha heshima tuliyokuwa nayo ukanda wetu wa maziwa makuu, Afrika na dunia nzima kwa ujumla?
Watu hawataamini maana huko waliko wao wanataka tupigane marisasi watucheke! Tuvurugane watukebehi! Tushenyetane wao waje wazoe marasilimali yetu
Tuukwepe huu mtego kwa kuunda serikali ya mseto ambayo itatuletea katiba mpya na uchaguzi huru na wa haki huko mbeleni. Vingenevyo hii hali itakuwa ya kujirudia rudia