Shetani ndani ya Kanisa

Mwiba

JF-Expert Member
Oct 23, 2007
7,607
1,744
Gafla Shetani aliingia kanisani kwa kishindo,upepo milango kujipiga na mataa kuyumba,hapo kikazuka kitimtimu jamaa mbio nje kukatokea m'banano mlangoni wa kuumia mtu ,mara kanisa lote lilikuwa tupu hamna aliebakia isipokuwa mzee mmoja ,aliekaa na kutulia bila ya wasiwasi wowote ule.

Shetani akamfuatia huyo mzee pele alipokaa na kumuuliza :- Hivi hunijui mimi nani ?
Mzee akajibu nakujua vizuri sana.
Shetani akauliza tena;-Hivi wewe mbona hukimbii.
Mzee akajibu mimi sikimbii wala sina nia ya kukukimbia.
Shetani akaona huyu vipi akamuuliza hivi huniogopi mimi na kunikimbia kwa nini ?

Mzee kwa kujiamini akajibu :Mimi naishi na dada yako kwa muda wa miaka 48 nimemuoa ni mke wangu wa ndoa kabisa sasa kuna mtu akamkimbia shem wake !!!:becky:
 
Hilo kanisa halikuwa na upako wa Bwana shetani anaingia mpaka ndani??
kuna tofauti kati ya madracula wa zamani na wa sasa ,wa sasa hawaungui kwa msalaba ,angalia usifananishe andazi na mkate !
 
Nilifikiri huyo Mzee atamjibu shetani kwamba ana upako ndo maana akimbii.kumbe na yy ni shetani.
 
Ah ah ah ah ah! Hii nmeipenda sana, dawa ya moto ni moto, kikulacho kinguoni mwako, ukikidhibiti umetibu bwana shemeji hawezi mdhuru shemejie sister atakosa buzi
 
Back
Top Bottom