KATIKA ULIMWENGU WA ROHO ukitoa ndio unapata.
Hii ni kanuni ya ulimwengu wa roho ,kanuni ya Mungu mwenyewe ambapo pia inatumiwa na pande zote za kiroho ukimwengu wa giza(watu /wafuasi wa shetani) na ulimwengu wa nuru(watu wa Mungu)
na hata wasio dini au waapagani au wanaoamini katika karma,nature kwa kujua au kutokujua.
Shetani anaijua hii ndio mana naye anaitumia kwa watu wake wafuasi wake wachawi,waganga wa kienyeji,mafreemansory n.k
1)KWA IMANI YA KIKRISTO UKISOMA BIBLIA UTATHIBITISHA HILI
mkono unaotoa ndio inaonarikiwa kuliko mkono unaotoa.
kipimo kile unachowapimia watu kuwapa ndicho hicho hicho Mungu atakupimia kwa scale yake mana kwa Mungu miaka 1000 ni sawa na siku moja,kipimo chako mwanadamu mfano ukimpa mtu kwa kipimo cha mkono wako mwanadamu Mungu anapokurudishia akikupimia mkono wake mkubwa mkuu basi inakuwa kingi kicho jaa kusukwa sukwa hata kumwagika.
Anayemsaidia masikini anakuwa anamkopesha Mungu Mungu atamlipa kwa tendo lake hilo jema.
KIFUPI MKONO UNAOTOA NDIO UNAOBARIKIWA ZAIDI KULIKO UNAOPOKEA .
Kwa dini nyingine pia naona wao wanatoa zaidi kwa masikini,wagonjwa mahospitalini,wafungwa ,yatima ,na wasiojiweza
kama waislamu kwakweli huwa naona watoa sana sadaka kwa wahitaji...hasa wagonjwa na hao wengine masikini ,yatima ..nafikiri kwao ni NGUZO KABISA ya imani yao..mfano mahospitalini wanawaletea wagonjwa chakula alfajiri,mchana,nguo ,maji,na kadhalika.
FREEMANSORY ..wao ndio kabisa wanajiita shirika la kutoa misaada kwa wahitaji charity.
WAGANGA WA KIENYEJI NA WACHAWI
Baadhi ya masharti yanahusisha kutoa zawadi au vitu kwa watu,
zawadi kamaa vyakula ,nyama za kafara,pesa zilizonuiziwa,nguo,viatu,vinywaji n.k
unaweza kukuta mshirikina kazi yake anachinja makafara yake anawagawia watu nyama ,au anaandaa sherehe watu waje kula na kunywa,au anawagawia watu pesa,zawadi,vyakula,vinywaji n
k
kupitia kutoa ndio anapata zaidi...
Hata nchi wahisani...zinatoa sana misada kuja nchi za kiafrica kwa sababu zinafaidika zaidi kwa kanuni hii ya kiroho KUWA ANAYETOA NDIO ANAYEBARIKIWA ZAIDI KULIKO ANAYETOA.
Na waliogundua KANUNI HII watakubalina na mimi kuwa kuoitia kutoa wamepokea baraka zaidi,na mara nyingi utagundua watu walioifahamubsiri hii utakuta hawaachi kutoa kila wakati ,wameshagundua siri iliyopo.
HATA katika ibada yoyote iwe ya madhabahu za nuru au zile za giza
lazima kuna sadaka utoe sadaka
tena wachawi na wa waganga wa kienyeji freemansory wanatoa sadaka 60% tena inatolewa kwa lazima na kwa wakati..
wakati Zaka inayotolewa kwa Mungu ni 10% ..tu.
yani ukiona mpaka mchawi anafanikiwa kuwa na nguvu za kichawi au kiganga ametoa sana sadaka hata damu yake kama watoto ama kuimarisha vizimba vyake sadaka mbalimbali.
kutoa kunakupa nguvu ya kiroho ya madhabahu yako,kama ni ya guza au nuru.
Hata waumini wanaotoa sadaka ya ZAKA 10% kwa Mungu kwa uaminifu wanakuwa na nguvu kubwa ya madhabahu zao na baraka nyingi.
na mchawi anayetoa sadaka mara kwa mara sadaka kubwa naye anaimarisha vizimba vyake nguvu zake za uchawi wake.
KIFUPI HAKUNA CHA BURE ILI UPATE LAZIMA UTOE KWANZA.
na kuna azuiaye isivyo haki lakini huishia kuwa muhitaji.
yani kuna azaniaye kuwa anakusanya kumbe anataoanya au anatia katika mfuko uliotoboka.
WENYE UELEWA WA KANUNI HII huwa wanapenda sana kutoa bila kuchoka sio wachoyo kabisa.
lakini wachawi wanaitumia vibaya..USIPENDE KUPOKEA POKEA vutu vya bure bure hovyo,usipende kula kula ovyo wengine wanaandaa sherehe na kugawa vyakula bure,au vinywaji au pesa wakiwa na lengo la kuchukua kutoka kwenu ushurikina,au ni rahisi ukala nyama ama vyakula vya matambiko,auakafara yaliyonenewa nuiziwa.
SALI OMBEA CHAKULA KABLA YA KULA..ombea zawadi unazopewa .
omba sali kila wakati.