Solomon David
JF-Expert Member
- Mar 1, 2009
- 1,148
- 16
Hawa inabidi adhabu yao iwe mara mbili ya adhabu ya wabakaji wasio viongozi wa dini:
Ustaadhi wa Madrasa akamatwa akibaka Mwanafunzi
Na Samuel Msuya,Morogoro
JESHI la Polisi mkoani Morogoro linamshikilia ustaadh wa madrasa, Dadi Ramadhani, 35, ambaye ni mkazi wa Mafiga mkoani hapa kwa tuhuma za kujaribu kumbaka mwanafunzi wa darasa la sita wa Shule ya Msingi Kinondoni jijini Dar es Salaam.
Kamanda wa polisi mkoani Morogoro, Thobias Andingenye alisema mwalimu huyo wa dini alikamatwa Desemba 24 majira ya saa 6:00 mchana kwenye nyumba ya kulala wageni ya Bembea iliyo maeneo ya Kiwanja cha Ndege mkoani hapa.
Kamanda Andingenye alisema awali wazazi wa binti huyo mara baada ya mtoto wao kurudi likizo walimuomba ustaadh huyo amsaidie masuala ya kidini katika madrasa yake na ndipo ustaadh huyo alipoanza kushikwa na tamaa na kuanza kumlaghai ili afanye mapenzi na mwanafunzi huyo.
Akisimulia tukio hilo, Andingenye alisema kutokana na mtoto huyo kuchoshwa na kusumbuliwa na ustaadh huyo aliamua kumshtaki kwa wazazi wake, ambao kwanza walimuonya, lakini mwalimu huyo wa dini alikana kufanya kitendo hicho.
Alisema pamoja na ustaadh huyo kuonywa na wazazi, aliendelea na ushawishi wake na safari hii akaamua kutumia mbinu ya kumnunulia binti huyo nguo kwa ajili ya sikukuu ya Krismasi.
Kamanda Andingenye alisema baadaye wazazi wa binti huyo waliamua kuweka mtego kwa kushirikiana na binti yao na ndipo walipomnasa Desemba 24 kwenye chumba namba 10 cha nyumba ya wageni ya Bembea akifanya jaribio la kumbaka.
Alisema kabla ya kumfikisha binti huyo katika nyumba ya wageni, ustaadh huyo alimpeleka kwenye duka la nguo na kumchagulia nguo za sikukuu na kisha kuziacha dukani huku akiahidi kuzifuata baadaye.
Kamanda Andingenye alisema mtuhumiwa huyo anatarajiwa kufikishwa mahakamani mara baaada ya uchunguzi wa tuhuma hizo kukamilika.
Katika tukio jingine jeshi la Polisi mkoani hapa linawashikilia wanafunzi wawili wa mwaka wa pili wa Chuo Kikuu cha Kiislam, Sadi Ayubu, 23, na Joseph Mwinjake, 27, kwa kuwashambulia na kuwajeruhi Abdul Mhanga, 22, na Mussa Rajabu wakiwatuhumu kuwa ni vibaka.