SHEIKH Alhad Mussa, aunga mkono juhudi za Makonda

Ghazwat

JF-Expert Member
Oct 4, 2015
23,718
66,262
cc7b955b738291b77461f09cffd20b6f.jpg


Baraza la viongozi wa dini la kupambana na dawa za kulevya Tanzania, linaunga mkono juhudi za Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam kupambana na dawa za kulevya

Akizungumza na waandishi wa habari jijini hapa leo, Sheikh wa Mkoa wa Dar es salaam, Alhad Mussa amesema baraza linapinga na kulaani hatua yoyote ya kushiriki katika biashara na utumiaji wa dawa za kulevya

"Tunampongeza kwa dhati kabisa Mkuu wa Mkoa kwa ujasiri aliouonyesha kwa kuwa ameamua kujitoa mhanga kwa ajili ya Taifa", amesema.

Chanzo: Mwananchi
 
Kimsingi hakuna mtu mwema atakayepinga Vita dhidi ya Madawa ya Kulevya.
Watu wanapinga mbinu inayotumiwa kupambana na Madawa ya kulevya.
 
Hili lijamaa mnafiki kichizi
Shehe upo sahihi, hakuna mtu ambaye anaweza kupinga hiyo vita maana inaharibu vijana, kinacholalamikiwa ni namna vita hiyo inavyopiganwa, vita yeyote hata iwe ya maneno huhitaji maandalizi na mikakati thabiti inayoandaliwa mapema ili kupata matokeo sahihi, kinachoendelea hapa ni papara na haraka ambazo zinasababisha sasa wahusika halisi wajihami na kitakachoendelea baadaye ni kukosa ushahidi wa maana. Fikiria pamoja na kuwa na watuhumiwa zaidi ya 150 mpaka sasa madawa ya kulevya yaliyopatikana ni KETE 12 kweli? tena nyingi ni za bangi. Nafikiri nia ni njema lakini namna vita inavyopiganwa tutajikuta tumeshindwa dakika za mwanzo kabisa. Vita ili ipiganwe lazma umjue adui wako, silaha alizonazo n.k, kujiingiza kichwakichwa uwanja wa vita hatari kama hii ni kutafuta tu kushindwa mapema. Jamii ihusishwe kikamilifu na mijadala ifanywe ili kupata njia sahihi za kutokomeza tatizo hili.
 
tangia huyu sheikh aunde urafiki na ccm ninem underestimate sana... na maamuzi yake au yao na jopo la pro ccm asihusishe na uislam kabisa hiyo dhambi aibebe peke yake
 
tangia huyu sheikh aunde urafiki na ccm ninem underestimate sana... na maamuzi yake au yao na jopo la pro ccm asihusishe na uislam kabisa hiyo dhambi aibebe peke yake
Hayo ni maoni yake.Anapenda kujipendekeza kwa wanasiasa hata kama anajua anchofanya ni kinyume na dini.
 
Ulitegemea nini wakati makonda anawajengea makao makuu ya Bakwata kwa hisani ya GSM
 
Kumshambukia Shekhe sidhani ni busara. Sasa sijajua itakuwaje ila nadhan Makonda kapatia katika kukosea
 
cc7b955b738291b77461f09cffd20b6f.jpg


Baraza la viongozi wa dini la kupambana na dawa za kulevya Tanzania, linaunga mkono juhudi za Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam kupambana na dawa za kulevya
chezea kukaa gorofani.haha
Akizungumza na waandishi wa habari jijini hapa leo, Sheikh wa Mkoa wa Dar es salaam, Alhad Mussa amesema baraza linapinga na kulaani hatua yoyote ya kushiriki katika biashara na utumiaji wa dawa za kulevya

"Tunampongeza kwa dhati kabisa Mkuu wa Mkoa kwa ujasiri aliouonyesha kwa kuwa ameamua kujitoa mhanga kwa ajili ya Taifa", amesema.

Chanzo: Mwananchi
 
Siku Makonda akiita Mashoga itabidi amwite na huyu Sheikh sababu anatuhumiwa kuwa ni mtoto si riziki
 
Back
Top Bottom