duCCM YAMUAGA PROF BAREGU
Familia wamshukuru Rais SAMIA
Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimeshiriki ibada ya kuaga mwili wa Profesa Mwesiga Laurent Baregu iliyofanyika usharika wa KKKT Kunduchi Beach, Dar es Salaam Ijumaa 18 Juni 2021.
"Mwenyekiti wa CCM na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan amemtaja Prof Mwesiga Baregu kuwa alikuwa ni mwanazuoni mzalendo, aliyetumia taaluma yake katika kuimarisha na kuhuisha demokrasia nchini na ni mwanasiasa nguli aliyependa siasa safi na siasa za hoja kwa ustawi wa watanzania, daima tutamkumbuka na kuenzi."
Alisema Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Shaka Hamdu Shaka wakati akiwasilisha salam za Rambirambi.
Msemaji wa Familia hiyo Prof Kaijage amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mwenyekiti wa CCM Mhe Samia Suluhu Hassan kwa moyo wake wa kiungwana kwa kuwa nao katika kipindi chote cha msiba na maombelezo ya mpendwa wao.
"Rais Samia ametufariji sana wote mlisikia kupitia Vyombo vya Habari na mitandao baada msiba huu kutokea alitufariji, kwa salam za pole na leo amemtuma mwakilishi wake ametupa nguvu na tunathamini sana hili kwa kuwa tumekuwa nae katika kipindi hiki kigumu kwetu wanafamilia " Prof Kaijage.
Prof Baregu amesafirishwa leo kuenda nyumbani kwao Mkoani Kagera kwa Mazishi.
MY TAKE:
Barakoa ina kazi gani? Au changa la macho? Corona ipo.
View attachment 1822954View attachment 1822955View attachment 1822956View attachment 1822957View attachment 1822958View attachment 1822959
View attachment 1822960
View attachment 1822961
Mungu fundi sana mkuu ndio maana kamuondoa mapemaMwendazake hakutaka kuona Watanzania wakipendana. Alipenda kuhubiri amani huku akikumbatia manyoka kama Sabaya waliokuwa wakitesa wananchi
Huu ndio uhuni wa ccm wa kutaka ku-take advantage ya kila kitu hadi kwenye misiba!Familia wamshukuru Rais SAMIA
Hapa mama anajenga umoja wa kitaifa kwa vitendoHuu ndio utanzania Sasa
Kwakweli afanye vema maana tuligawanyika Kama nchi sio yetu yaaniHapa mama anajenga umoja wa kitaifa kwa vitendo
Huu ndio utanzania Sasa
SAA nyingine na wewe uwe mwelewa, SHAKA Ni mwenezi wa chama. Unataka akieneze vipi chama chake? Ni hivyo tu!Hivi lazima magwanda kwenye misiba!!!
Kupata chanjo haina maana usivae barakoa .Jamaa mboye si alisema ameshapata chanjo sasa barakoa ya nn
swali la msingi sana hiliAmetoa Chozi kwenye hizo Salamu za Rambirambi alizotuma kutumia mwakilishi wake ?
Anyway Rest in Peace Prof...
Kwahio aliyetoa chozi ni Shaka na sio Samia ? Duh basi hii lugha yetu ya Taifa ni ngumu sana wewe hii sentensi ungeielewa vipi ?Mkuu huyo mvuta uzi, anamaana Rais Samia katuma ujumbe kwenye ulioongozwa na Katibu Mwenezi wa CCM Shaka, basi suala la kutokwa na Chozi ni la SHAKA.
DJ msaniiJamaa mboye si alisema ameshapata chanjo sasa barakoa ya nn
Hivi ni lazima USIVAE magwanda msibani ?Hivi lazima magwanda kwenye misiba!!!
Ndo nini sasa?Kupata chanjo haina maana usivae barakoa .
Unaweza ukawa na virusi vya korona huku ukiwa na chanjo na visikuathiri wewe na vikawaathiri wengine ukawasambazia