pantheraleo
JF-Expert Member
- Jan 5, 2013
- 691
- 878
CCM YAMUAGA PROF BAREGU
Familia wamshukuru Rais SAMIA
Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimeshiriki ibada ya kuaga mwili wa Profesa Mwesiga Laurent Baregu iliyofanyika usharika wa KKKT Kunduchi Beach, Dar es Salaam Ijumaa 18 Juni 2021.
"Mwenyekiti wa CCM na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan amemtaja Prof Mwesiga Baregu kuwa alikuwa ni mwanazuoni mzalendo, aliyetumia taaluma yake katika kuimarisha na kuhuisha demokrasia nchini na ni mwanasiasa nguli aliyependa siasa safi na siasa za hoja kwa ustawi wa watanzania, daima tutamkumbuka na kuenzi."
Alisema Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Shaka Hamdu Shaka wakati akiwasilisha salam za Rambirambi.
Msemaji wa Familia hiyo Prof Kaijage amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mwenyekiti wa CCM Mhe Samia Suluhu Hassan kwa moyo wake wa kiungwana kwa kuwa nao katika kipindi chote cha msiba na maombelezo ya mpendwa wao.
"Rais Samia ametufariji sana wote mlisikia kupitia Vyombo vya Habari na mitandao baada msiba huu kutokea alitufariji, kwa salam za pole na leo amemtuma mwakilishi wake ametupa nguvu na tunathamini sana hili kwa kuwa tumekuwa nae katika kipindi hiki kigumu kwetu wanafamilia " Prof Kaijage.
Prof Baregu amesafirishwa leo kuenda nyumbani kwao Mkoani Kagera kwa Mazishi.
MY TAKE:
Barakoa ina kazi gani? Au changa la macho? Corona ipo.
Familia wamshukuru Rais SAMIA
Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimeshiriki ibada ya kuaga mwili wa Profesa Mwesiga Laurent Baregu iliyofanyika usharika wa KKKT Kunduchi Beach, Dar es Salaam Ijumaa 18 Juni 2021.
"Mwenyekiti wa CCM na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan amemtaja Prof Mwesiga Baregu kuwa alikuwa ni mwanazuoni mzalendo, aliyetumia taaluma yake katika kuimarisha na kuhuisha demokrasia nchini na ni mwanasiasa nguli aliyependa siasa safi na siasa za hoja kwa ustawi wa watanzania, daima tutamkumbuka na kuenzi."
Alisema Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Shaka Hamdu Shaka wakati akiwasilisha salam za Rambirambi.
Msemaji wa Familia hiyo Prof Kaijage amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mwenyekiti wa CCM Mhe Samia Suluhu Hassan kwa moyo wake wa kiungwana kwa kuwa nao katika kipindi chote cha msiba na maombelezo ya mpendwa wao.
"Rais Samia ametufariji sana wote mlisikia kupitia Vyombo vya Habari na mitandao baada msiba huu kutokea alitufariji, kwa salam za pole na leo amemtuma mwakilishi wake ametupa nguvu na tunathamini sana hili kwa kuwa tumekuwa nae katika kipindi hiki kigumu kwetu wanafamilia " Prof Kaijage.
Prof Baregu amesafirishwa leo kuenda nyumbani kwao Mkoani Kagera kwa Mazishi.
MY TAKE:
Barakoa ina kazi gani? Au changa la macho? Corona ipo.