Sote waja tumeumbwa, mola kumsujudia
Pekeye ndo wakuombwa, dini kumtakasi
tuyawache tulogombwa, mema kuyakimbila
JF itambue,lengo la sisi kuumbwaaa
Tumeumbwa kwa kusudi, si bahati ilo mbaya
Kujua hatuna budi, hiso faradhi kifaya
elimu na uweledi, ujinga mwisho mbayaa
JF itambue,lengo la sisi kuumbwaa
Dunia chumba cha dhiki, mola amejaalia
tuishi kwa tekiniki, kifo chatukaribia
usije dhani hung'oki, mauti yatakujia
JF itambue,lengo la sisi kuumbwaa.
Ndugu ulotoa mada, haya majibu nakupa
upate nyingi faida, usije kutoka kapa
elimu yako mazida, kwazote dhambi kukwepwa
JF itambue,lengo la sisi kuumbwaaa
Sent using
Jamii Forums mobile app