Dotto C. Rangimoto
JF-Expert Member
- Nov 22, 2012
- 1,985
- 1,286
Wamama na kina baba, ninayosema sikia,
Mwana kumwita Msiba, ni tabu kumtakia,
Atakuwa na uhaba, wa akili nawambia,
Mfano ni huyu daba, uchao atubwatia.
Mtoto kumwita Pombe, haifai zingatia,
Aweza kuwa mzembe, mwenye kinyaa kutia,
Ama akaota pembe, na watu akapigia,
Pengine akawa hambe, mwepesi wa kuchukia.
Siyo jina Polepole, mtoto kumpatia,
Atakuwa kama yule, mkosefu wa tabia,
Leo hili kesho lile, unafiki yake njia,
Matapishi yake ale, huku twamuangalia.
Kwanini asitulie, mweye jina la Tulia?
Sio lake niwambie, ikiwa hajatulia
Jinale atupatie, hilo amelivamia,
Katu asiitikie, au abadili ndia.
Mwana mpa jina zuri, ambalo linavutia,
Na tena liwe la heri, na baraka zake pia,
Siyo jina lenye shari, na zito kuitikia,
Asema hayo Qahari, kwa kupitia Nabia.
Hapa sasa ni tamati, hivyo kikomo natia,
Haya wenzangu wanati, leo nilowaandikia,
Aula mkayanoti, na kazi kuyafanyia,
Nti ni nusu kaputi, si punde itajifia.
31 Machi 2018 Jumamosi 09:31am
Jina la Mtunzi: Dotto Rangimoto
Jina la Utunzi: Jini Kinyonga
+255762845394 Morogoro.
Kama bado hujanipigia kura Tuzo ya NguvuYaUthubutu andika
NU 024
Kisha tuma katika namba hizi +255756094875 kwa njia ya SMS na Whatsp. Asanteni Sana.
Mwana kumwita Msiba, ni tabu kumtakia,
Atakuwa na uhaba, wa akili nawambia,
Mfano ni huyu daba, uchao atubwatia.
Mtoto kumwita Pombe, haifai zingatia,
Aweza kuwa mzembe, mwenye kinyaa kutia,
Ama akaota pembe, na watu akapigia,
Pengine akawa hambe, mwepesi wa kuchukia.
Siyo jina Polepole, mtoto kumpatia,
Atakuwa kama yule, mkosefu wa tabia,
Leo hili kesho lile, unafiki yake njia,
Matapishi yake ale, huku twamuangalia.
Kwanini asitulie, mweye jina la Tulia?
Sio lake niwambie, ikiwa hajatulia
Jinale atupatie, hilo amelivamia,
Katu asiitikie, au abadili ndia.
Mwana mpa jina zuri, ambalo linavutia,
Na tena liwe la heri, na baraka zake pia,
Siyo jina lenye shari, na zito kuitikia,
Asema hayo Qahari, kwa kupitia Nabia.
Hapa sasa ni tamati, hivyo kikomo natia,
Haya wenzangu wanati, leo nilowaandikia,
Aula mkayanoti, na kazi kuyafanyia,
Nti ni nusu kaputi, si punde itajifia.
31 Machi 2018 Jumamosi 09:31am
Jina la Mtunzi: Dotto Rangimoto
Jina la Utunzi: Jini Kinyonga
Kama bado hujanipigia kura Tuzo ya NguvuYaUthubutu andika
NU 024
Kisha tuma katika namba hizi +255756094875 kwa njia ya SMS na Whatsp. Asanteni Sana.