Shairi: Msiba

Dotto C. Rangimoto

JF-Expert Member
Joined
Nov 22, 2012
Posts
1,985
Reaction score
1,286
Wamama na kina baba, ninayosema sikia,
Mwana kumwita Msiba, ni tabu kumtakia,
Atakuwa na uhaba, wa akili nawambia,
Mfano ni huyu daba, uchao atubwatia.

Mtoto kumwita Pombe, haifai zingatia,
Aweza kuwa mzembe, mwenye kinyaa kutia,
Ama akaota pembe, na watu akapigia,
Pengine akawa hambe, mwepesi wa kuchukia.

Siyo jina Polepole, mtoto kumpatia,
Atakuwa kama yule, mkosefu wa tabia,
Leo hili kesho lile, unafiki yake njia,
Matapishi yake ale, huku twamuangalia.

Kwanini asitulie, mweye jina la Tulia?
Sio lake niwambie, ikiwa hajatulia
Jinale atupatie, hilo amelivamia,
Katu asiitikie, au abadili ndia.

Mwana mpa jina zuri, ambalo linavutia,
Na tena liwe la heri, na baraka zake pia,
Siyo jina lenye shari, na zito kuitikia,
Asema hayo Qahari, kwa kupitia Nabia.

Hapa sasa ni tamati, hivyo kikomo natia,
Haya wenzangu wanati, leo nilowaandikia,
Aula mkayanoti, na kazi kuyafanyia,
Nti ni nusu kaputi, si punde itajifia.

31 Machi 2018 Jumamosi 09:31am
Jina la Mtunzi: Dotto Rangimoto
Jina la Utunzi: Jini Kinyonga
+255762845394 Morogoro.

Kama bado hujanipigia kura Tuzo ya NguvuYaUthubutu andika

NU 024

Kisha tuma katika namba hizi +255756094875 kwa njia ya SMS na Whatsp. Asanteni Sana.
 
Musiba tusimlaumu, kumbe tatizo jina...!!!
Na hata ukimpa mtoto jina la pombe basi atakuwa kipombe pombe tuuu.

Looh! Asante mwandishi.
 
Reactions: PNC
we jamaa wewe....!!angalia usije ukajiteka au kujipiga risasi!!
 
we jamaa wewe....!!angalia usije ukajiteka au kujipiga risasi!!
Siku hizi wanasema silaha kumgusa mtu. Ha haaa, Mambozamani huyo. Eti silaha iliyomgusa Akwilina haijajulikana!
 
Uko vizuri sana, ungeshusha na ya chemba, makonda na suluhu
 
Wamama na kina baba, ninayosema sikia,
Mwana kumwita Msiba, ni tabu kumtakia,
Atakuwa na uhaba, wa akili nawambia,
Mfano ni huyu daba, uchao atubwatia.
Mtaka nyingi nasaba, hupata mwingi msiba,
Waulize Maswahaba, kuhusu mingi misiba,
Ya ndugu wenye nasaba, wanapopata msiba,
Mtu kuitwa Musiba, ni balaa la msiba.

Ni balaa la msiba, Mtu kuitwa Musiba,
Usijiletee misiba, kwa Majina ua Musiba,
Epuka yote misiba, Kumuepuka Musiba,
Mtu kuitwa Musiba, ni balaa la msiba.

Musiba anapayuka, kwa habari za msiba,
Akilize zayeyuka, kwa tarifa ya msiba,
Fikira zimeyeyuka, kwa kufikwa na msiba,
Mtu kuitwa Musiba, ni balaa la msiba.

Musiba aleta janga, janga kubwa la msiba,
Majina yenye majanga, kutuletea misiba,
Taifa lenye majanga, yaletwayo na msiba,
Mtu kuitwa Musiba, ni balaa la msiba.

Kaditama nimefika, Musiba aache misiba,
Kwenye heri tumefika, asituletee misiba.
Hapa mwisho nimefika, tusisikie misiba
Mtu kuitwa Musiba, ni balaa la msiba.

p
 
Siku hizi wanasema silaha kumgusa mtu. Ha haaa, Mambozamani huyo. Eti silaha iliyomgusa Akwilina haijajulikana!
ukipewa cheo lzm uwe na shukrani,nasikia eti cheo ni dhamana.
 
Umesahau Makonda, lichambue lake jina
Kwetu sisi kule Pemba, lina na yake maana
Ni mtu asiye pendwa, kwa kutofahamiana
Kila anachokitenda, Mungu hujaza laana

Bashite au Makonda, hivi lipi jina lake
Ni mtu anayependa, kujifanya na makeke
Ila yake ni kuvunda, ubaya ni sifa yake
Kila anachokitenda, sio mwema mwisho wake
 
P kumbe umo? Tumekutana mara nyingi sana Sabasaba Kilwa Road na hata Mnazi Mmoja. Sikujua manju
. Big up bro
 
Huyu bwana Msiba hasipozuiliwa kuna kitu anakipandikiza ndani ya Watanzania,

Yeye kama raia mwema alipaswa kwenda kurepot mahala husika,

Hii ya kutaja taja watu tu madhara yake ni makubwa sana ,

Atajenga tabia ya watu kupuuza habari nyingine za ukweli wakidhani ni Tanzania ya kutaja taja tu,

Adhibitiwe na ashikiliwe kwa mahijihano zaid
 
Nani amdhibiti, nani anamtuma. sema anayemtuma aache kumtuma.
 
Sema pamoja haya mambo yanatokea hawajawai kuigusa family za maaskari wa JWTZ.
Wakiwagusa family za maaskari wa JWTZ ndio tutapata jibu kamili
 
Nimekuwa nikiwaza kwa sauti. Hivi hujuma zinazofanyiwa wananchi na hivi madaktari wakianza kufanya hivyo dhidi yao.

Mfano: Njiani unakutana na trafic anakuambia umezidisha mwendo ulikua 53 badala ya hamsini huyu anamlipisha fine Daktari. Jioni trafic unajisikia vibaya sababu umekaa juani muda mrefu unaenda hospitali kwa daktari na Dr anamwambia pressure yako iko juu kwa unit tatu zaidi ngoja tukupige sindano ya kushusha pressure na akaamua kushusha hadi 0(zero) naamini umenielewa sifuri maana yake ni nini.

Kwa jinsi hali ilivyo na maelezo ya huyu Bwana Musiba ambaye hachukuliwi hatua kutatupelekea kila mmojakwa nafasi yake atafanya jambo kulipiza kisasi kwa watesi wake.

Mamlaka za nchi tuchukue hatua STAHIKI SASA tusisubiri kujenga ukuta
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…