- Thread starter
- #21
Nawashukuru wote kwa tungo hizi kali sana! Thanks you have brightened my day!!!!
Eli tumekusikia, hongera watupatia
Tungo wazifurahia, wasema ziko sawia
Nasi twashukuru pia, ni hoja twashindania
Ni nini maoni yako, visima twajadilia
Twaomba mchango wako, malenga wakusubiri
Zimwage busara zako, sote tuweze kukiri
Yalete yenye mshiko, tuzidi kutafakari
Ni nini maoni yako, visima twajadilia
Tupe yenye uzoefu, jadili pasi kificho
Twangoja yako turufu, itikia huu wito
sinione msumbufu, lete hoja motomoto
Ni nini maoni yako, visima twajadilia
SMG