Shairi - kisima nimekiacha

Nawashukuru wote kwa tungo hizi kali sana! Thanks you have brightened my day!!!!


Eli tumekusikia, hongera watupatia
Tungo wazifurahia, wasema ziko sawia
Nasi twashukuru pia, ni hoja twashindania
Ni nini maoni yako, visima twajadilia


Twaomba mchango wako, malenga wakusubiri
Zimwage busara zako, sote tuweze kukiri
Yalete yenye mshiko, tuzidi kutafakari
Ni nini maoni yako, visima twajadilia

Tupe yenye uzoefu, jadili pasi kificho
Twangoja yako turufu, itikia huu wito
sinione msumbufu, lete hoja motomoto
Ni nini maoni yako, visima twajadilia


SMG
 
WOSIA NIMEUPATA
kweli nazidi shukuru, mengi wanisaidia
wanipa mwanga na nuru, kwa yale nisojulia
Nisingependa kufuru, na mola takujalia
Wosia nimeupata, nasema tazingatia
.........................................
Mchina ajulikana, popote hakosekani
Iweje twaambiana, vya bara hapatikani
si kama twachunguzana, niondoe mashakani
Wosia nimeupata, nasema tazingatia
SMG


Haijalishi ni wapi;

Nimefurahi mtani, kisima watafutia
Mradi ni kisimani, ambapo waelekea

Iwe bara au pwani, kikubwa ni kutunzia

Kisima bora kutunza, mengine ni majaliwa


Wa bara wamenitonya, mchina awakwepea

Wasema wanawamanya, kuweza watapelia

Wanakukwepa Makanya, Malinyi pia Songea

Kisima bora kutunza, mengine ni majaliwa


Mradi kipenda roho, majiyo ukajinywea
Hata uitwe mroho, wakati wafaidia

Yawe kule Peramiho, ama Pwani asilia

Kisima bora kutunza, mengine ni majaliwa


Haijalishi mchina, na siri hiyo sikia
Mradi unajichana, kwa maji hayo sawia

Ni siri yako kijana, kwa nini kutangazia?

Kisima bora kutunza, mengine ni majaliwa


Nimefurahi mtani, na hapa nakomelea
Haijalishi ni nani, ama wapi chatokea

Si chupa ni kisimani, majiyo kujipatia

Kisima bora kutunza, mengine ni majaliwa
 
ZAFANANA


Mimi mchimba mahiri, kazi yangu naijua
Nimetafiti dhahiri, yote nimeyajua
Nimekula vya hariri, hakuna asiyejua
Zimefanana kwa hila, tabia na maumbile

Visima si tofauti, maumbile nagusia
Utakunywa kwa nyakati, hilo nakumbia
Fanya zako harakati, kiasi utajutia
Zimefanana kwa hila, tabia na maumbile

Kisima wakiingia, mbizi wajipigia
Hazina wakimwagia, maradhi cha kupatia
Kauli yakuishia, vilinge wavikimbia
Zimefanana kwa hila, tabia na maumbile

Sadiki yangu maneno, visima vyote ni sawa
usije jitoa meno, utamu wako maridhawa
Umejikunya kiuno, akili za kupagawa
Zimefanana kwa hila, tabia na maumbile


Usijitie kisoi , utamu wako mwenyewe
Kamuulize mtoi, mrukaji kama mwewe
Hata lile goigoi, lawa tamu kama wewe
Zimefanana kwa hila, tabia na maumbile

Chama
Gongo la Mboto DSM


KUBWA NI SAWA NA NDOGO?

Kwanza acha majisifu, eti mchimba mahiri
Yaonyesha hu nadhifu, kazi kikiri kikiri
una mengi mapungufu, chunguza na tafakari
Naomba hebu nijibu, kubwa ni sawa na ndogo?

Wajidai mtafiti, kumbe wewe kimeo
koti si sawa na shati, u wapi wako upeo
Acha kujipa na chati, umeshapiga kileo?
Naomba hebu nijibu, kubwa ni sawa na ndogo?

Maumbile si yasawa, ni nyingi zimepishana
Na ile ya Havijawa, si kama eti ya Ana
Kata haiwi upawa, iweje zitafanana
Naomba hebu nijibu, kubwa ni sawa na ndogo?

Vyote vyabeba maji, kwa hili nalikubali
Tofauti ni mtaji, ladha na kwenye shughuli
Na pia kuna vipaji, mwali hamuwezi nguli
Naomba hebu nijibu, kubwa ni sawa na ndogo ?

Na ndefu nayo si fupi, jaribu kulinganisha
ureshe wako mshipi, halafu tofautisha
Hoja yako hailipi, mtani wabahatisha
Naomba hebu nijibu, kubwa ni sawa na ndogo

SMG
 
Kubwa kubwa ndogo ndogo iweje kubwa iwe ndogo na ndogo iwe kubwa!!!! Hata siwezi mwaya
 
Kubwa kubwa ndogo ndogo iweje kubwa iwe ndogo na ndogo iwe kubwa!!!! Hata siwezi mwaya

Haha....haha.......but it always worth giving a trial, ukiweka nia utaweza kuandika, mimi nimejifunzia kuandika mashairi humuhumu JF, kule MMU, i was inspired by klorokwini na alini - encourage sana, na bado najifunza kwa wengine
 
Haijalishi ni wapi;

Nimefurahi mtani, kisima watafutia
Mradi ni kisimani, ambapo waelekea

Iwe bara au pwani, kikubwa ni kutunzia

Kisima bora kutunza, mengine ni majaliwa


Wa bara wamenitonya, mchina awakwepea

Wasema wanawamanya, kuweza watapelia

Wanakukwepa Makanya, Malinyi pia Songea

Kisima bora kutunza, mengine ni majaliwa


Mradi kipenda roho, majiyo ukajinywea
Hata uitwe mroho, wakati wafaidia

Yawe kule Peramiho, ama Pwani asilia

Kisima bora kutunza, mengine ni majaliwa


Haijalishi mchina, na siri hiyo sikia
Mradi unajichana, kwa maji hayo sawia

Ni siri yako kijana, kwa nini kutangazia?

Kisima bora kutunza, mengine ni majaliwa


Nimefurahi mtani, na hapa nakomelea
Haijalishi ni nani, ama wapi chatokea

Si chupa ni kisimani, majiyo kujipatia

Kisima bora kutunza, mengine ni majaliwa


MASHARTI NA VIGEZO

Naomba niwie radhi, kwangu si bora kisima
Jambo la kwanza hadhi, kabla ya ndani kuzama
Na iwapo sijaridhi, basi hapo nahama
Mtani nazingatia, masharti na vigezo

Sitaki kilichoguswa, kila mtu ajinywea
Kutwa kuchwa chapanguswa, watu wajiogelea
Ya nini hadhi kushushwa, walafi watabobea
Mtani nazingatia, masharti na vigezo

Cha bara au cha pwani, chochote nitachukua
Nitaweka tena ndani, naomba za kwako dua
Ila kama kisirani, basi hapo napangua
Mtani nazingatia, masharti na vigezo

Mchina hana nafasi, vibovu sitachukua
Nataka tuliza nafsi, sitaki kujizingua
Nizame bila ya wasi, ndo raha ya dunia
Mtani nazingatia, masharti na vigezo

Cha kwangu na kiwe changu, ndo ninalokusudia
sitaki wale machangu, kila kukicha na njia
Naomba kwa mungu wangu, maisha kufurahia
Mtani nazingatia, masharti na vigezo

SMG
 
Kubwa kubwa ndogo ndogo iweje kubwa iwe ndogo na ndogo iwe kubwa!!!! Hata siwezi mwaya
 
KUBWA NI SAWA NA NDOGO?

Kwanza acha majisifu, eti mchimba mahiri
Yaonyesha hu nadhifu, kazi kikiri kikiri
una mengi mapungufu, chunguza na tafakari
Naomba hebu nijibu, kubwa ni sawa na ndogo?

Wajidai mtafiti, kumbe wewe kimeo
koti si sawa na shati, u wapi wako upeo
Acha kujipa na chati, umeshapiga kileo?
Naomba hebu nijibu, kubwa ni sawa na ndogo?

Maumbile si yasawa, ni nyingi zimepishana
Na ile ya Havijawa, si kama eti ya Ana
Kata haiwi upawa, iweje zitafanana
Naomba hebu nijibu, kubwa ni sawa na ndogo?

Vyote vyabeba maji, kwa hili nalikubali
Tofauti ni mtaji, ladha na kwenye shughuli
Na pia kuna vipaji, mwali hamuwezi nguli
Naomba hebu nijibu, kubwa ni sawa na ndogo ?

Na ndefu nayo si fupi, jaribu kulinganisha
ureshe wako mshipi, halafu tofautisha
Hoja yako hailipi, mtani wabahatisha
Naomba hebu nijibu, kubwa ni sawa na ndogo

SMG

AKILI

Kipimo gani watumia, tueleze tupatejua
Kisima wakizamia, kiza chakusumbua
Usije angamia, kwa uroho wa kutumbua
Akili ya juu hulala, ya chini ikiamka

Macho yapo kizani, huna ukionacho
Wageuka hayawani, kwa utamu ukilacho
Mayowe ya punguani, fahamu zaruka macho
Akili ya juu hulala, ya chini ikiamka

Utakipima kwa kipi, akili zimekuruka
Umeyashika makapi, kwa akili ya mzuka
Ndefu imekuwa fupi, pasina kuna kuwa dhihaka
Akili ya juu hulala, ya chini ikiamka

Kama maji huyawezi, waachie majirani
Watakunywa kama wakwezi, warukiapo mnazini
Una papara za panzi, kisima kimekuzini
Akili ya juu hulala, ya chini ikiamka

Usijitie uchimvi, usiozaliwa nao
Kula kwangu chumvi, ujuzi nimekua nao
Usilikimbie jamvi, kwa udaku ulionao
Akili ya juu hulala, ya chini ikiamka

Chama
Gongo la Mboto DSM
 
AKILI

Kipimo gani watumia, tueleze tupatejua
Kisima wakizamia, kiza chakusumbua
Usije angamia, kwa uroho wa kutumbua
Akili ya juu hulala, ya chini ikiamka

Macho yapo kizani, huna ukionacho
Wageuka hayawani, kwa utamu ukilacho
Mayowe ya punguani, fahamu zaruka macho
Akili ya juu hulala, ya chini ikiamka

Utakipima kwa kipi, akili zimekuruka
Umeyashika makapi, kwa akili ya mzuka
Ndefu imekuwa fupi, pasina kuna kuwa dhihaka
Akili ya juu hulala, ya chini ikiamka

Kama maji huyawezi, waachie majirani
Watakunywa kama wakwezi, warukiapo mnazini
Una papara za panzi, kisima kimekuzini
Akili ya juu hulala, ya chini ikiamka

Usijitie uchimvi, usiozaliwa nao
Kula kwangu chumvi, ujuzi nimekua nao
Usilikimbie jamvi, kwa udaku ulionao
Akili ya juu hulala, ya chini ikiamka

Chama
Gongo la Mboto DSM


BASI UJUVI HUNAO

Chama punguza papara, mtani fanya tulia
Uache ya masighara, au umeshafulia?
Sioni lenye busara, hutaki kufikiria
Kama huwezi kupima, basi ujuvi hunao

Punguza zako porojo, eti wewe umjuzi
Kwa hoja hizi urojo, wewe ni wajuzi juzi
Muone bwana kitojo, akupe ya utambuzi
kama huwezi kupima, basi ujuvi hunao

Vipi palipo na shimo, eti ushindwe kupima
sisi wajuzi wa vimo, twaingiza yote nzima
sisemi kwa majivuno, 'machoyo' hayatopima
kama huwezi kupima, basi ujuvi hunao

Viungo 'kazie' nini, anza sasa kutumia
Au ndio majirani, wanao kusaidia?
Huu ni uhayawani, watakuja kuibia
kama huwezi kupima, basi ujuvi hunao

Heri ya kufunga mwaka, nayo ninakupatia
Mola akupe baraka, mwaka unaofatia
Aondoe ya mashaka, nilosema zingatia
kama huwezi kupima, basi ujuvi hunao

kheri akujaalie, akhera na duniani
maisha ufurahie, aondoshe mitihani
shari azikimbishie, vya watu usitamani
Kama huwezi kupima, basi ujuvi hunao

SMG
 
Nakukumbusha Mtani;

Nakujulisha mtani, ni mengi tumeshanena
Wayataka kisimani, ama zako danadana?
Nahisi mwangu kichwani, Unaikwepa dhamana
Kisima bora kutunza, nakukumbusha mtani

Ni mengi umejulishwa, na Chama shahidi yangu
Na pia ukakumbushwa, vina siri kama chungu
Halafu ukaamshwa, vina ladha na machungu!
Kisima bora kutunza, nakukumbusha mtani

Amani naye akaja, kawacha kula kobisi
Na mengi akayataja, kasema bila tetesi
Uwache wako ujanja, tafuta hata Nkasi
Kisima bora kutunza, nakukumbusha mtani

Kitu kikubwa kupenda, mengine ni siri yako
Visima vipo zote kanda, waweza vifata huko
Ufike hata Mpanda, akili kichwani mwako
Kisima bora kutunza, nakukumbusha mtani

Kwa heri ya kuonana, nina kuaga mtani
Ni mengi tuliyonena, mambo yote kisimani
Usifanye kushindana, ameshasema Amani
Kisima bora kutunza, nakukumbusha mtani
 
BASI UJUVI HUNAO



Chama punguza papara, mtani fanya tulia
Uache ya masighara, au umeshafulia?
Sioni lenye busara, hutaki kufikiria
Kama huwezi kupima, basi ujuvi hunao

Punguza zako porojo, eti wewe umjuzi
Kwa hoja hizi urojo, wewe ni wajuzi juzi
Muone bwana kitojo, akupe ya utambuzi
kama huwezi kupima, basi ujuvi hunao

Vipi palipo na shimo, eti ushindwe kupima
sisi wajuzi wa vimo, twaingiza yote nzima
sisemi kwa majivuno, 'machoyo' hayatopima
kama huwezi kupima, basi ujuvi hunao

Viungo 'kazie' nini, anza sasa kutumia
Au ndio majirani, wanao kusaidia?
Huu ni uhayawani, watakuja kuibia
kama huwezi kupima, basi ujuvi hunao

Heri ya kufunga mwaka, nayo ninakupatia
Mola akupe baraka, mwaka unaofatia
Aondoe ya mashaka, nilosema zingatia
kama huwezi kupima, basi ujuvi hunao

kheri akujaalie, akhera na duniani
maisha ufurahie, aondoshe mitihani
shari azikimbishie, vya watu usitamani
Kama huwezi kupima, basi ujuvi hunao

SMG

VIPIMO

Kibaranga wakimbia; mjini wakimbilia
Sindano nakumbia, yamjini vumilia
Uhodari wakudandia, utakuja jililia
Umechanganya hisabu, vipimo vyako batili

Mjini kuna hatari, huna ulijualo
Pokea yako habari, wamjini tujualo
Utaja pigwa kabari, na wahuni tololo
Umechanganya hisabu, vipimo vyako batili

Macheni watumbukia, baridi waibugia
Kimwana waibukia, maneno wamgusia
Nyumbani wakimbilia, kimwana wakilalia
Umechanganya hisabu, vipimo vyako batili

Kimwana chacheza shere, uani cha kupeleka
Walia kama tetere, akili yakuchanguka
Uani wala udere, vya mbele hujavishika
Umechanganya hisabu, vipimo vyako batili

Hakika imedhihiri, kula kizani huwezi
Wajitia uhodari, wa kujifanya mkwezi
Utamu wa jodari, hautazidi wa mbuzi
Umechanganya hisabu, vipimo vyako batili

Mwaka mpya waingia, tuliza wako mzuka
Makini ukiingia, mlango wa mbele tumika
Mola atajalia, kuondelea gharika
Umechanganya hisabu, vipimo vyako batili



Chama
Gongo la Mboto DSM
 
Happy new year to all of you Choveki, Yakuonea & Elli ; 2012 make the best of you. No matter how hard it is God will make the way for and your family
Peace!

Chama
Gongo la Mboto DSM
 
Happy new year to all of you Choveki, Yakuonea & Elli ; 2012 make the best of you. No matter how hard it is God will make the way for and your family
Peace!

Chama
Gongo la Mboto DSM

Thnx so very much bro. I wish you the same, and may the year 2012 be the most successful year in your life

SMG
 
Nakukumbusha Mtani;

Nakujulisha mtani, ni mengi tumeshanena
Wayataka kisimani, ama zako danadana?
Nahisi mwangu kichwani, Unaikwepa dhamana
Kisima bora kutunza, nakukumbusha mtani

Ni mengi umejulishwa, na Chama shahidi yangu
Na pia ukakumbushwa, vina siri kama chungu
Halafu ukaamshwa, vina ladha na machungu!
Kisima bora kutunza, nakukumbusha mtani

Amani naye akaja, kawacha kula kobisi
Na mengi akayataja, kasema bila tetesi
Uwache wako ujanja, tafuta hata Nkasi
Kisima bora kutunza, nakukumbusha mtani

Kitu kikubwa kupenda, mengine ni siri yako
Visima vipo zote kanda, waweza vifata huko
Ufike hata Mpanda, akili kichwani mwako
Kisima bora kutunza, nakukumbusha mtani

Kwa heri ya kuonana, nina kuaga mtani
Ni mengi tuliyonena, mambo yote kisimani
Usifanye kushindana, ameshasema Amani
Kisima bora kutunza, nakukumbusha mtani


KUTUNZA HAKUNA SHAKA


kwanza pokea salamu, kheri ya mwaka mpya
mola akupe fahamu, akukinge na mabaya
wasikudhuru dhalimu, watu wenye roho mbaya
Hili ninalitambua, kutunza hakuna shaka

Na sipigi danadana, ni kweli natafutia
Nalia nae rabana, cha kheri kunijalia
meisha wangu ujana, uzee umeingia
Hili ninalitambua, kutunza hakuna shaka

Na mola nipe subira, nimechoka kusubiri
Niongoze kwenye dira, nimeshakata shauri
Ni njema yangu dhamira, naomba kiso na shari
Hili ninalitambua, kutunza hakuna shaka

Nahimiza msimamo, vya ovyo sintodandia
Angalia hilo somo, waweza jifunza pia
kwa haya yangu makamo, nitakacho kutulia
Hili ninalitambua, wajibu wangu kutunza

Amani ameshauri, kwa nini sinywi ya chupa
Si kwamba nina kiburi, siridhiki hata pipa
Naomba nawe fikiri, hivi kweli yanalipa?
Hili ninalitambua, kutunza hakuna shaka

Chama nae kajongea, asema zina fanana
kwa hapa nimegomea, nadai zinapishana
vipi wewe waongea, hebu tupe bayana
Hili ninalitambua, kutunza hakuna shaka

Nasema nikikipata, mengi nitakifanyia
kutwa kucha nakumbata, kisimani naingia
miliki nitakamata, watani nitawambia
Hili ninalitambua, kutunza hakuna shaka

SMG
 
VIPIMO

Kibaranga wakimbia; mjini wakimbilia
Sindano nakumbia, yamjini vumilia
Uhodari wakudandia, utakuja jililia
Umechanganya hisabu, vipimo vyako batili

Mjini kuna hatari, huna ulijualo
Pokea yako habari, wamjini tujualo
Utaja pigwa kabari, na wahuni tololo
Umechanganya hisabu, vipimo vyako batili

Macheni watumbukia, baridi waibugia
Kimwana waibukia, maneno wamgusia
Nyumbani wakimbilia, kimwana wakilalia
Umechanganya hisabu, vipimo vyako batili

Kimwana chacheza shere, uani cha kupeleka
Walia kama tetere, akili yakuchanguka
Uani wala udere, vya mbele hujavishika
Umechanganya hisabu, vipimo vyako batili

Hakika imedhihiri, kula kizani huwezi
Wajitia uhodari, wa kujifanya mkwezi
Utamu wa jodari, hautazidi wa mbuzi
Umechanganya hisabu, vipimo vyako batili

Mwaka mpya waingia, tuliza wako mzuka
Makini ukiingia, mlango wa mbele tumika
Mola atajalia, kuondelea gharika
Umechanganya hisabu, vipimo vyako batili



Chama
Gongo la Mboto DSM


CHAMA HUISHI UTATA

Naja ninarudi tena, kwako kijana mtata
Lengo ni kukumbushana, ni vyema mema kufata
Usione nakuchana, Wosia hebu kamata
Chama huishi utata, hoja unavyopindisha

Na huo sio ujana, chama haujatulia
sasa watafuta lana, mola wamjaribia
kule hakuna maana, madhambi wajichumia
chama huishi utata, hoja unavyopindisha

Siseme ni yamjini, La hasha hilo ni lako
Eti kwenda kwa macheni, wewe waona ujiko
umo wewe hasarani, achana uchafu wako
chama huishi utata, hoja unavyopindisha

Hivi kwa kweli kisima, takipata magomeni?
Yaonyesha humzima, kushindia kwa macheni
wenye nazo tumepima, sioni yako 'visheni'
Chama huishi utata, hoja unavyopindisha

Na chema hutokipata, danguroni nakwambia
wapo washika ukuta, vipi wajisaidia?
Machafu umefumbata, mtani fanya tulia
chama huishi utata, hoja unavyopindisha

sasa picha napata, wewe wanamna gani
uani unavyopata, utakuwa punguwani
vinyezi kuvikamata, wewe kweli hayawani
chama huishi utata, hoja unavyopindisha

SMG
 
CHAMA HUISHI UTATA

Naja ninarudi tena, kwako kijana mtata
Lengo ni kukumbushana, ni vyema mema kufata
Usione nakuchana, Wosia hebu kamata
Chama huishi utata, hoja unavyopindisha

Na huo sio ujana, chama haujatulia
sasa watafuta lana, mola wamjaribia
kule hakuna maana, madhambi wajichumia
chama huishi utata, hoja unavyopindisha

Siseme ni yamjini, La hasha hilo ni lako
Eti kwenda kwa macheni, wewe waona ujiko
umo wewe hasarani, achana uchafu wako
chama huishi utata, hoja unavyopindisha

Hivi kwa kweli kisima, takipata magomeni?
Yaonyesha humzima, kushindia kwa macheni
wenye nazo tumepima, sioni yako 'visheni'
Chama huishi utata, hoja unavyopindisha

Na chema hutokipata, danguroni nakwambia
wapo washika ukuta, vipi wajisaidia?
Machafu umefumbata, mtani fanya tulia
chama huishi utata, hoja unavyopindisha

sasa picha napata, wewe wanamna gani
uani unavyopata, utakuwa punguwani
vinyezi kuvikamata, wewe kweli hayawani
chama huishi utata, hoja unavyopindisha

SMG

UTATA

Nakupa heri ya mwaka, Mola atujalie
Atujazie fanaka, mabaya tuyakimbie
Atupe zake baraka, wachawi watukimbie
Hakika nakuapia, Chama sina uduvi

Choveki nakutuma, Sindano nitafutie
Kwa Macheni amezama, asubuhi mdamkie
Mpe zangu karama, akili imfungukie
Hakika nakuapia, Chama sina uduvi

Chama hana utata, mtoto wa kiungwana
Jando amelipata, masomo walimshona
Akili ameipata, busara zipo bayana
Hakika nakuapia, Chama sina uduvi

Chama hana madhila, kajaa furaha tele
Ni mtu mwenye fadhila, hajipendei kelele
Usije ntia hila, kwa wivu uliotele
Hakika nakuapia, Chama sina uduvi

Chama mtu makini, hula kwa kuchagua
Hana umasikini, wa kushindwa kutambua
Mola kanipa dini, vya halali navijua
Hakika nakuapia, Chama sina uduvi

Chama namalizia, Kibaranga najiendea
Chelangwa nitamwambia, mjini kutembelea
Maneno kukupatia, utuondelee fedhea
Hakika nakuapia, Chama sina uduvi

Chama
Gongo la Mboto DSM
 
Back
Top Bottom