MTENDAHAKI
JF-Expert Member
- Mar 3, 2011
- 4,013
- 1,448
Kutokana na nukuu zinazoendelea kutolewa na wachambuzi mbalimbali (Hapa namuongelea Lissu) katika mchakato wa katiba mpya, imethibitisha pasipo shaka kuwa Mh. Dr. Mwakyembe anakikana kile alichokiandika miaka ya Tisini ili kupata udaktari wa falsafa (PhD).
Katika kitabu chake alinukuliwa akisema kuwa muundo wa muungano wa Tanzania ni shirikisho pasipo na shaka, na kuthibitisha kuwa migogoro itamalizwa kwa kuwa na serikali tatu! Ni kwa hoja zake hizo aliweza kutunukiwa shahada ya uzamivu (PhD). Sasa kwa kuwa anazikana hoja hizo maana yake ni kuwa alipotosha watu katika utafiti wake!
Aidha aliegemea upande ambao alikuwa anautaka (bias) au aliamua kufuata wengine walisemaje!Sasa kwa kuwa hata yeye hauamini utafiti wake je sio haki yake kuondolewa udaktari wake!?
Prof. Shivji nae ameyakana maandiko yake ya miaka ya 90, ambayo mengine aliyatumia kupanda cheo mpaka kuwa profesor, je nae sio haki yake ashushwe cheo hicho?
Nawasilisha.
Katika kitabu chake alinukuliwa akisema kuwa muundo wa muungano wa Tanzania ni shirikisho pasipo na shaka, na kuthibitisha kuwa migogoro itamalizwa kwa kuwa na serikali tatu! Ni kwa hoja zake hizo aliweza kutunukiwa shahada ya uzamivu (PhD). Sasa kwa kuwa anazikana hoja hizo maana yake ni kuwa alipotosha watu katika utafiti wake!
Aidha aliegemea upande ambao alikuwa anautaka (bias) au aliamua kufuata wengine walisemaje!Sasa kwa kuwa hata yeye hauamini utafiti wake je sio haki yake kuondolewa udaktari wake!?
Prof. Shivji nae ameyakana maandiko yake ya miaka ya 90, ambayo mengine aliyatumia kupanda cheo mpaka kuwa profesor, je nae sio haki yake ashushwe cheo hicho?
Nawasilisha.