Serious kichwa kinaniuma, shemeji yangu ana mimba yangu

juvenile davis

JF-Expert Member
Apr 13, 2015
4,752
4,449
Habari zenu wapendwa,

Hakika jana haikuwa siku nzuri kwangu,kama mnavojua nilishasema kwamba nina watoto watatu wa mama tofauti, kuna Travis, Sean na Moureen. Sasa iko hivi, ni kwa muda mrefu nimekuwa na mahusiano ya kimapenzi na mdogo wa mama Moureen, tumekuwa kwenye mahusiano ya siri sana na mkumbuke mama Moureen ndie yule niliyembikiri kisha baadae akanizalia mtoto na nishasema sitamuoa kwasababu ya mdomo na gubu lake, basi kuna siku mimi na mdogo wa mama Moureen tulikuwa tunachat Whatsapp.

Kwa bahati mbaya mama Moureen alikuja akaona zile conversations zote za mapenzi na ndipo akagundua ya kwamba natoka na mdogo ake, kwa kweli aliniuliza na aliumia sana na nilishindwa kujitetea wala kubisha zaidi tu ya kuomba msamaha, ila mahusiano na mdogo wake hayakuisha, tumeendelea kimyakimya na kwa siri sana.

Sasa jana mtoto kaniambia siku zake za period zimepitiliza, harafu anatapika na anachagua misosi, nikaogopa, tumeenda hospital flani ya binafsi kupima mimba kwa kweli ni kwamba huyu binti ni mjamzito yaani jana nzima kichwa kinanigonga balaa, sijui hata nifanye nini, maana sina raha kabisa na huyu binti anashinda analia kutwa kwao ila hajawaambia anacholia ni nini.

Naogopa itakuwa ni aibu kwenye familia yangu na kwa jamii pia kutoa naogopa mana sijawahi kumtoa yeyote yule na naogopa asije akafa ila pia ni dhambi, sielewi hata nifanye nini, nahisi kukonda siku mbili tu, kila nikiwaza mwili unashtuka maana hili jambo linaninyima amani sana.
 
kumtongoza umtongozee weweee
Kumvua umvue weweee
Kuzama chumvini uzame wewee
Kumlamba sikio umlambee weweee
Kumgegeda umgegedede weweee
utamu mpatee nyieee
kumpa mimba umpee weweee

afu ushaurii tutoee sieeeeeeeeee
Majangaaaaaaaaaa
Mbona majangaaaaaaaaa
 
kumtongoza umtongozee weweee
Kumvua umvue weweee
Kuzama chumvini uzame wewee
Kumlamba sikio umlambee weweee
Kumgegeda umgegedede weweee
utamu mpatee nyieee
kumpa mimba umpee weweee

afu ushaurii tutoee sieeeeeeeeee
Majangaaaaaaaaaa
Mbona majangaaaaaaaaa
Hahaha,mkuu umeamua kumwimbia sasa...teh teh
 
Back
Top Bottom