Serikali yafunga migodi 4 Mererani

kandabongo

New Member
Joined
Jul 23, 2013
Posts
2
Reaction score
1
Kufuatia kupigwa risasi kwa mfanyakazi wa Tanzanite one William Onesmo Mushi na kufariki papo hapo serikali kupitia wizara ya nishati na madini imefunga migodi minne inayozunguka eneo hilo kwa muda usiojulikana ili kupisha uchunguzi wa kina kufuatia tukio hilo.

Kamishna Msaidizi wa madini kanda ya kaskazini Benjamin Mchwampaka alitaja migodi iliyofungwa kuwa ni inayomilikiwa na Joseph Mwakipesile maarufu kwa jina la Chusa,Abdulhakimu Mula,Maning'oo na Jackson Saimon.

Aidha Jeshi la polisi mkoa wa Manyara linamshikilia Chusa kwa mahojiano kuhusiana na tuhuma za kudaiwa kuhusikana kifo cha Mushi usiku wa kuamkia Julai 20 mwaka huu.

Uchunguzi wa madaktari wa mwili wa marehemu umebaini kuwa maremu aliuwawa kwa kupigwa risasi mbili kifuani upande wa kushoto zilizomsababishia kifo cha papo hapo.
 
Hao raian wengine wameuwawa miaka nenda rudi kwa kisingizio cha kutress pass mboona migodi haikufungwa?
 
Damu ya mtu inapotea kisa mawe tu? Achukuliwe hatua bila kujali ni tajiri au la.
 
Vipi kwan naye hakutii sheria? au ndiyo ile kauli wapigwe tu! OOh Tanzania my beloved country why this happening?
 
Vipi kwan naye hakutii sheria? au ndiyo ile kauli wapigwe tu! OOh Tanzania my beloved country why this happening? R.I.P MUSHI
 
RIP Wilee nakumbukaga ile Noah asee.

Atafutwe mhusika alietuulia kamanda wetu afungwe na "apigwe tu".

Kwa wanaomjua mazishi ni Alhamisi.
 
Kwa wale mliokuwa hamumjui marehemu ndio huyu, ni jamaangu kabisa! so sad!!! Lala salama willy!
 
Kufuatia kifo cha mfanyakazi wa Tanzanite One,serikali imefunga migodi minne ya wachimbaji wadogo jrani na mgodi wa kampuni hiyo.

Habari mwananchi .
 
Huo ni upepo tu, baada ya siku mbili ukishapita mgodi wataufuungua!!!! Ndiyo serikali yetu hiyo, never mind its people, hasa kama huna hela!! Wenye hela wanapeta kila kona, kuanzia hata katika sharia na mambo mengine!! Kimemo kitatoka juu!! Subiri mkuu uone na kusikia kwa macho yako.
 

Sikuwa nimeinyaka vizuri, kumbe ni ya walala hoi imefungwa? Kwani hicho kifo cha mtumishi kimesababishwa na hao watumishi wa migodi midogo? Au ndiyo mlamgo wa kutokea kuwazuia hao wadogo na kesho viwanja vyao wanapewa hao mafisadi wa Tanzania one!!!? So sad!
 

mnyonge mnyongeni haki yake mpeni,hii ni serikali ya maccm bwana.
 

ni kawaida ya serikali yoyote kandamizi duniani uone watu wake na kuwathamini wageni.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…