GE2025 Serikali ya zionya NGOs na AZAKI kuepuka kutumika kuelekea uchaguzi mkuu 2025

GE2025 Serikali ya zionya NGOs na AZAKI kuepuka kutumika kuelekea uchaguzi mkuu 2025

Matukio, Taarifa, Habari na Mijadala ya Wananchi WAKATI wa Mchakato wa Uchaguzi Mkuu 2025

Mkalukungone Mwamba

JF-Expert Member
Joined
Aug 29, 2022
Posts
2,437
Reaction score
5,235
Serikali imeonya Mashirika Yasiyo ya Kiserikali (NGOs) na Asasi Za Kiraia (AZAKI) kutokubali kutumika kama njia ya kutakatisha fedha kwa maslahi ya watu binafsi au vikundi mbalimbali, ikiwemo vya kisiasa, hasa katika kipindi hiki ambacho taifa linajiandaa kwa Uchaguzi Mkuu wa Rais, Wabunge na Madiwani mwaka huu wa 2025.

Onyo hilo limetolewa Jumatatu Agosti 11, 2025, jijini Dodoma na Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Mwanaidi Ali Khamis, wakati akifungua Kongamano la Mwaka la Mashirika Yasiyo ya Kiserikali, kwa niaba ya Waziri wa wizara hiyo Dkt. Dorothy Gwajima.

Kupata taarifa na matukio yanayojiri kuelekea uchaguzi mkuu kwa kila mkoa ingia hapa:
Special Thread: Mijadala na Matukio ya Uchaguzi Mikoa yote Tanzania Bara na Zanzibar kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025

Mwanaidi amesema kuwa mashirika hayo yanapaswa kuwa na uwazi na uwajibikaji wa hali ya juu, kwani ndiyo msingi wa kutambuliwa kwa mchango wao katika maendeleo ya taifa.

“Ni muhimu kwa Mashirika Yasiyo ya Kiserikali kuzingatia misingi ya maadili, sheria na kanuni. Tusikubali kutumiwa kwa maslahi ya watu binafsi au vyama vya siasa, hasa katika mwaka huu wa uchaguzi,” amesisitiza.

 
Back
Top Bottom