yutong
JF-Expert Member
- Apr 15, 2011
- 1,601
- 338
Mfumo uliopo wa sasa wa CCM unastahili kufanyiwa marekebisho makubwa kwani ni mzigo mkubwa kwa watzanzania na hasa ukizingatia unatumia kodi za watz ambao ndo kwanza hawana maji, hawana umeme, hawana shule za uhakika kwa ajili ya watoto wao.
Hebu nianze na Mkoa wa Dar es Salaam labda; viongozi hawa wote tija iko wapi?
1. Mkuu wa Mkoa (RC)
2. Katibu tawala wa Mkoa (RAS)
3. Meya wa Jiji
4. Mkurugenzi wa Jiji
5. Wakuu wa wilaya watatu
5. Makatibu tawala wa wilaya watatu (MaDAS)
6. Mameya wa Manispaa watatu
7. Wakurugenzi wa Manispaa watatu
sasa huo utitiri wa viongozi hapo juu tujiulize je unaendana na maendeleo ya Jiji la Dar es Salaam? labda mniambie nini wajibu wa kila kiongozi hapo juu? lakini tunashuhudia mji uko ovyo ovyo. Pia ukiangalia hapo juu kila aliyetajwa hapo ana Shangingi lake la kumtoa nyumbani kwenda kazini. Kweli mtu ambaye yuko Dar es Salaam anahitaji gari kubwa namna hiyo kumtoa nyumbani kwenda ofisini na kumrudisha nyumbani kila siku? Tujiulize hapo?
Pia kuna utitiri wa taasisi na mashirika ambayo hayana Tija kwa mfano ktk Tanesco kuna kitengo cha Umeme vijijini, lakini kuna REA nk? Kazi hasa ya REA sasa ninini? Je, Toka REA ianze imeshafanikiwa kuweka umeme vijiji vingapi? Kuna TIRDO, TPDC, TIPPER, nk. Pia kuna EWURA, SUMATRA, hebu tujiulize haya mashirika hasa yanachangia ama yameleta mabadiliko gani ya msingi kwa watz zaidi ya kuongeza gharama kwa watz? maana kila unaponunua umeme unakatwa pcntg kwenda Ewura, ukinunua petrol unakatwa pcntg kwenda ewura, maji unakatwa pcntg kwenda ewura, sasa tujiulize kwanza katika hela wanayopata ewura inakwenda wapi? je ni wao kujilipa tu na safari zisizo za msingi, je wizara kama wizari haiwezi kusimamia? Kuna NHC, kuna TBA nk tofauti ya NHC na TBA ni nini? je kazi za shirika moja wapo haziwezi fanywa na shirika moja ama wizara? Hii yote ni matumizi mabaya ya kodi za watz, badala ya kuongeza shule zaidi, hospitali zaidi CCM wao wameamua kujaza mashirika mengi zaidi yasiyo na Tija kwa watz na ambayo nimzigo kwa serikali. Kunaidara mbalimbali kila wizara ambazo zingeweza kusimamia shughuli zote hizo kwa gharama nafuu. Mashirika yaundwe pale ambapo kunaulzima wa kufanya hivyo na wakati fula yawe ya muda ili kutimiza lengo fulani.
Hivyo basi inawezekana CCM wameunda mashirika yote hayo ili kuweka mitego ya mapato yao na njia ya kuiba pesa ya watz. Kwa mfano mashirika ya hifadhi za jamii kwa nini yawe mengi hivyo wakati kazi zao nimoja? Kama hivyo ndivyo kwa nini Shirika la Bima ya Afya ni moja kwa wafanyakazi wote? watz fumbueni macho CCM wana mbinu nyingi kutuibia. sasa tuseme basi imefika mwisho. katika taifa masikini kama letu nilitegemea kuona serikali inajenga shule nyingi toka za nasale mpaka vyuo vikuu na hospitali za kutosha. wansema wananchi wachangie ujenzi wa zahanati/shule mbona kununua magari hawasemi tuchangie? je hizo hela wanazipata wapi? kwa nini zisingetumika kujenga shule/zahanati? Serikali ya CCM ni wanafiki ambao wanawadanganya wananchi kuwa serikali haina hela wakati wao wakiishi maisha ya kifahari nakuendesha magari ya kifahari ambayo hata waliotengeneza hawayatumii kukwepa gharama.
Natumaini mmenielewa na kama bado mtu unaona CCM iko ok basi utakuwa unamtindio wa ubongo.
Hebu nianze na Mkoa wa Dar es Salaam labda; viongozi hawa wote tija iko wapi?
1. Mkuu wa Mkoa (RC)
2. Katibu tawala wa Mkoa (RAS)
3. Meya wa Jiji
4. Mkurugenzi wa Jiji
5. Wakuu wa wilaya watatu
5. Makatibu tawala wa wilaya watatu (MaDAS)
6. Mameya wa Manispaa watatu
7. Wakurugenzi wa Manispaa watatu
sasa huo utitiri wa viongozi hapo juu tujiulize je unaendana na maendeleo ya Jiji la Dar es Salaam? labda mniambie nini wajibu wa kila kiongozi hapo juu? lakini tunashuhudia mji uko ovyo ovyo. Pia ukiangalia hapo juu kila aliyetajwa hapo ana Shangingi lake la kumtoa nyumbani kwenda kazini. Kweli mtu ambaye yuko Dar es Salaam anahitaji gari kubwa namna hiyo kumtoa nyumbani kwenda ofisini na kumrudisha nyumbani kila siku? Tujiulize hapo?
Pia kuna utitiri wa taasisi na mashirika ambayo hayana Tija kwa mfano ktk Tanesco kuna kitengo cha Umeme vijijini, lakini kuna REA nk? Kazi hasa ya REA sasa ninini? Je, Toka REA ianze imeshafanikiwa kuweka umeme vijiji vingapi? Kuna TIRDO, TPDC, TIPPER, nk. Pia kuna EWURA, SUMATRA, hebu tujiulize haya mashirika hasa yanachangia ama yameleta mabadiliko gani ya msingi kwa watz zaidi ya kuongeza gharama kwa watz? maana kila unaponunua umeme unakatwa pcntg kwenda Ewura, ukinunua petrol unakatwa pcntg kwenda ewura, maji unakatwa pcntg kwenda ewura, sasa tujiulize kwanza katika hela wanayopata ewura inakwenda wapi? je ni wao kujilipa tu na safari zisizo za msingi, je wizara kama wizari haiwezi kusimamia? Kuna NHC, kuna TBA nk tofauti ya NHC na TBA ni nini? je kazi za shirika moja wapo haziwezi fanywa na shirika moja ama wizara? Hii yote ni matumizi mabaya ya kodi za watz, badala ya kuongeza shule zaidi, hospitali zaidi CCM wao wameamua kujaza mashirika mengi zaidi yasiyo na Tija kwa watz na ambayo nimzigo kwa serikali. Kunaidara mbalimbali kila wizara ambazo zingeweza kusimamia shughuli zote hizo kwa gharama nafuu. Mashirika yaundwe pale ambapo kunaulzima wa kufanya hivyo na wakati fula yawe ya muda ili kutimiza lengo fulani.
Hivyo basi inawezekana CCM wameunda mashirika yote hayo ili kuweka mitego ya mapato yao na njia ya kuiba pesa ya watz. Kwa mfano mashirika ya hifadhi za jamii kwa nini yawe mengi hivyo wakati kazi zao nimoja? Kama hivyo ndivyo kwa nini Shirika la Bima ya Afya ni moja kwa wafanyakazi wote? watz fumbueni macho CCM wana mbinu nyingi kutuibia. sasa tuseme basi imefika mwisho. katika taifa masikini kama letu nilitegemea kuona serikali inajenga shule nyingi toka za nasale mpaka vyuo vikuu na hospitali za kutosha. wansema wananchi wachangie ujenzi wa zahanati/shule mbona kununua magari hawasemi tuchangie? je hizo hela wanazipata wapi? kwa nini zisingetumika kujenga shule/zahanati? Serikali ya CCM ni wanafiki ambao wanawadanganya wananchi kuwa serikali haina hela wakati wao wakiishi maisha ya kifahari nakuendesha magari ya kifahari ambayo hata waliotengeneza hawayatumii kukwepa gharama.
Natumaini mmenielewa na kama bado mtu unaona CCM iko ok basi utakuwa unamtindio wa ubongo.