Serikali ya awamu ya tano imetaharuki kujeruhiwa Lissu

Tumuache lissu auguze majeraha yake mungu yuko naye lakini ninyi wanachadema kutumia hali ya lisu kujijenga kisiasa mungu atawalaani.hivi chadema wanaopata m 300 Kwa mwezi wanahitaji michango hiyo?
 
Tumuache lissu auguze majeraha yake mungu yuko naye lakini ninyi wanachadema kutumia hali ya lisu kujijenga kisiasa mungu atawalaani.hivi chadema wanaopata m 300 Kwa mwezi wanahitaji michango hiyo?


Mungu ni mwema na mkubwa mpaka sasa yeye ni Ebenezer na kwa imani kubwa uliyonayo Mungu keshamponya Lisu. kuhusu michango hiyo ni shekeli tuu na vile hujalazimshwa kuchanga acha wanaona ni vema kuchanga watachanga... binafsi nimechanga nitachanga... Na sio shurti hivyo tutachanga tuu
 
Hata sisi au mimi mwana CCM kwa kiasi fulani, nimekerwa na jaribio hili la kumuua Tundu Lissu.
Mtu mwenye mikono ya damu haui mtu mmoja, itakuwa tabia.

Visasi vikiingia, Burundi itakuwa cha mtoto.

Mtani utaumia zaidi ukisikia kwamba hata ukivaa Tshirt za Pray4Lissu uko matatani ndipo CCM ilipofikia
 
Hakika Nguvu ya Mungu imeonekana< Hakika pia Lissu amelipigania Taifa hili mpaka Damu yake kumwagika kwa ajili ya Taifa hili, nionavyo binafsi huyu ndie afaaye kuungwa mkono na daima tumwombee kwani ndie raisi ajae !!!!!!!
kweli kabisa
 
Lisu hajasema aombewe, wananchi wanaojua umuhimu wake ndio wanajitokeza kumuombea na Mungu husikiliza haraka na kujibu maombi hayo.
 
Hayo yangefanyika mapema kwa nia nyingine ingekua haina shida ila kwa sasa hawa waçhangia damu walionitokeza wanalifanya kujipatia umaarufu wa kisiasa kupitia tukio la TL
 
Tumuache lissu auguze majeraha yake mungu yuko naye lakini ninyi wanachadema kutumia hali ya lisu kujijenga kisiasa mungu atawalaani.hivi chadema wanaopata m 300 Kwa mwezi wanahitaji michango hiyo?
Wewe unajua gharama za kuendesha chama au unafikiri CHADEMA wamepora maeneo ya serikali kama Chama cha mauwaji?
 
Tatizo ni kwamba Serikali inafikiria kwamba Mungu anafanya kazi yake kama Serikali. Kwa Mungu, ukikusudia kwenda kuiba, halafu ukakatisha mpango baada ya kuona kwamba kuna walinzi au usalama wako ni mdogo, au siri imefichuka, kwa Mungu wewe tayari umeiba na unapata adhabu ya Mwizi. kwa hiyo, mtu kama amekusudia kusali kumwombea Tundu Lissu, halafu akafurushwa na Polisi, ile nia ya mtu au kikundi kile, tayari ni sala na imefika kwa Mungu!!!! Polisi sijui kama wanalijua hilo.
 
Yaani hata mimi nilijiuliza, hivi kwa mfano baada ya Dr. Mashinji kuagiza wanachadema wakatoe Damu, tuseme Polepole naye, au Kinana, angesimama na kusema kwa kweli kutoa Damu ni jambo jema sana, na tunawatia moyo wanaccm na watanzania wote wajitokeze kutoa Damu kwa ajili ya wagonjwa wetu, mbona tungepata Damu nyingi tu? Maana tukumbuke kwamba huwezi kutembeza mchango kwa ajili ya maafa ya tetemeko, kama hakuna tetemeko. limetokea janga, ni nafasi ya kuchangisha damu, fedha, nk. maana watu wanakuwa wameguswa na hilo tukio. tumepoteza fursa nzuri sana kwa ajili ya cheap politics
 
Mkuu umeandika kwa hekima bravo
 
Kuna MTU anahitaji kuombewa kwa lazima kila anaposima. Inakuwa kama lazima. Wengine wamefika kila kanisa.

Sasa, WaTz kwahiari yao wenyewe, tumeona anayehitajika kuombewa automatically.
Hata napoandika huu Ujumbe najikuta tu naandika
Pray for Lissu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…