Lupweko
JF-Expert Member
- Mar 26, 2009
- 20,693
- 20,453
Tusubiri maimamu watakua upande upi sasa, wa serikali au wa imamu mwenzao! Sitegemei kama watatoa tamko hapa kwani kila upande unawahusu!... Akizungumzia vurugu hizo, Waziri wa Nchi Afisi ya Makamu wa Rais (Muungano), Samia Suluhu Hassan, alisema waliofanya vurugu hizo ni wahuni.
Alisema kikundi hicho cha wahuni kilikwenda katika mkutano huo kwa malengo maalumu, ili ionekane watu hawataki Muungano.
Aidha, alisema amesikitishwa na kitendo cha watu kuchana nakala za muswada huo na kutoa wito kwa wananchi kujiepusha na vitendo vya jazba, lakini alisema maoni yote yaliyotolewa kamati imeyachukua na itayafanyia kazi.
Vurugu hizo zilitokea katika ukumbi wa Shule ya Haile Selassie mjini Zanzibar jana, baada ya Mwenyekiti wa Jumuiya ya Maimamu Zanzibar, Sheikh Farid Hadi Ahmed, kuchangia kwa maneno makali na baadaye kuuchana hadharani muswada huo na kutoka nje ya ukumbi.
...
Tukio hilo lilisababisha baadhi ya wajumbe kuzichana nakala za muswada huo huku wengine wakinyanyua viti juu wakiashiria kwamba mkutano huo umekwisha na baadhi yao wakimfuata Sheikh Farid nje ya ukumbi wa mkutano.