Chamoto
Platinum Member
- Dec 7, 2007
- 9,856
- 22,189
Mabango katikati ya barabara ni hatari
Usalama barabarani ni jambo kubwa na la msingi katika maendeleo ya nchi yetu. Moja ya vitu ambavyo vinaweza kuleta ajali barabarani ni vizingiti vinavyo mfanya dereva ashindwe kuona vizuri mbele.
Katika kipindi cha miaka ya nyuma, kumekuwa na ongezeko kubwa sana la mabango makubwa ya kutanganza biashara katikati ya barabara. Yapo Dar es salaam, Dododma, Mwanza n.k, unakuta dude kubwa tuu mbele yako linakuvuta macho uliangalie badala ya unakokwenda, hovyo kabisa. Barabara zinatakiwa ziwe wazi ili dereva aweze kuona mbali zaidi anakokwenda.
Serikali inabidi iyaondoe kabisa mabango yaliyo katikati mwa barabara ilikuongeza usalama kwa wananchi. Nchi zote zilizo endelea zina sheria kali za kuzuia mabango ya kibiashara katikati mwa barabara. Serikali inashindwa vipi kuzuia hili? Naelewa huko nyuma kulikuwa na rushwa na mambo mengi yalikuwa yanaenda kiholela lakini kwa awamu hii ya kutetea wanyonge nini kinashindikana?
Usalama barabarani ni jambo kubwa na la msingi katika maendeleo ya nchi yetu. Moja ya vitu ambavyo vinaweza kuleta ajali barabarani ni vizingiti vinavyo mfanya dereva ashindwe kuona vizuri mbele.
Katika kipindi cha miaka ya nyuma, kumekuwa na ongezeko kubwa sana la mabango makubwa ya kutanganza biashara katikati ya barabara. Yapo Dar es salaam, Dododma, Mwanza n.k, unakuta dude kubwa tuu mbele yako linakuvuta macho uliangalie badala ya unakokwenda, hovyo kabisa. Barabara zinatakiwa ziwe wazi ili dereva aweze kuona mbali zaidi anakokwenda.
Serikali inabidi iyaondoe kabisa mabango yaliyo katikati mwa barabara ilikuongeza usalama kwa wananchi. Nchi zote zilizo endelea zina sheria kali za kuzuia mabango ya kibiashara katikati mwa barabara. Serikali inashindwa vipi kuzuia hili? Naelewa huko nyuma kulikuwa na rushwa na mambo mengi yalikuwa yanaenda kiholela lakini kwa awamu hii ya kutetea wanyonge nini kinashindikana?