Nakumbuka mjini Tabora kuna wakati katika kutafuta riziki vijana kwa wingi sana walijiingiza kutoa huduma ya kubeba watu kwa baiskeli! Ni usafiri salama sana, wingi wa watoa huduma hii ambayo inawezekana iliwasaidia sana wateja wao ilileta nongwa toka kwa wamiliki wa Taxi baada ya kuona watu wengi hawahangaiki kukodi Taxi, Taxi drivers wakaanzisha vita kutaka kuwaondoa wenye baiskeli hata kuanza kuwagonga, kipindi hicho boda boda ilikuwa haijakolea. Fujo zilipozidi, Mkuu wa Mkoa (kama sijakosea) aliwashauri wamiliki wa Taxi kwamba anaeona biashara ya Taxi sasa hailipi apaki gari lake au basi waingie nao kwenye usafiri huu kipenzi cha wateja!
Huko Misri Jiji la El Arish kwenye jangwa la Sinai lililoko karibu na lango la Rafa kuingia Ukanda wa Gaza, Jiji hilo usafiri maarufu unaohudumia watu ni vigari vya Benzi vyenye shepu kama saloon vyenye uwezo wa kubeba abiria 6 lakini zinafanya biashara kwa kusanya jijini.
Kenya kuna vigari Toyota Probox, zimejaaa kama utitiri zikihudumia watu kama daladala kuwapeleka nje ya jiji. Probox za Kenya huwezi kulinganisha na Noah! Na nilikuwa nashangaa kuona Kenya wanaruhusu Probox wakati Tanzania wamezuia Noah ambazo zinanafasi na uwezo mkubwa kuliko Probox.
Nadhani wale ambao maslahi yao yataathirika kwa kuwepo Noah barabarani watatafuta vizingizio vya kitaalamu au kuwapaka matope wanasiasa, lakini suala ni kwamba nchi zetu hizi zinatatizo kubwa la usafiri! Kuna maeneo mengi watu wanatumia usafiri wa Malori na Landrover 109 mbona hizi hazilalamikiwi?
Wafanya biashara wa NOah Morogoro kwenda Dodoma wamekuwa wakifanyiwa fujo sana na wamiliki wa mabasi (waarabu na wahindi) baada ya kuona kuwa share yao kubwa ya abiria imemegwa na Noah! Kwa vile ni matajiri walifanikiwa kujenga hoja kwa Trafik wa Morogoro matokeo yake ilikuwa inashangaza Mkoani Morogoro Noah zilipigwa marufuku, lakini ukienda Singida, Nzega, Shinyanga na kanda ya Ziwa Michomoko imejaa inahudumia watu.
Tusome alama za nyakati kuelewa soko linataka nini na kuendana na mahitaji ya Soko, waziri Mwakyembe ni Intelligent person na hakika kasoma alama za nyakati. Hayo magari yalitengenezwa kwa matumizi ya abiria na siyo mbuzi, hata kama ni family car bado hao nao ni watu wale wale!