Serikali kununua ndege nyingine..

Serikali kununua ndege nyingine..

barafu

JF-Expert Member
Joined
Apr 28, 2013
Posts
6,739
Reaction score
32,916
Serikali ya Tanzania ipo ktk mkakati wa kununua ndege kwa matumizi na safari za viongozi wa serikali ndani na nje ya nchi.
Ndege hiyo aina ya Embraer 190(E190) yenye hadhi ya VIP inatazamiwa kununuliwa toka nchi ya Morroco na Serikali ya Tanzania kupitia Wakala wa Ndege za Serikali (Tanzania Government Flight Agency)
Kama ndege hiyo itanunuliwa,basi itafanya TGFA kuwa na ndege 5 ikiwemo ile Gulfstream 550 iliyozua balaa.Juzi ktk ziara yake uwanja wa ndege inasemwa Dr Harison Mwakyembe alifanya ukaguzi kuangalia ubora wa ndege hiyo ambapo aliruka nayo toka Dar-Zanzibar-K'njaro-Dar.
Wakati haya yanatokea,inasemwa kuwa shirika la ndege Tanzania bado lipo taabani na linamiriki ndege moja tu aina ya DH8 inayofanya safari zake ktk mikoa ya Tabora,Kigoma,Mtwara na Hahaya-Commoro
 
Serikali ya Tanzania ipo ktk mkakati wa kununua ndege kwa matumizi na safari za viongozi wa serikali ndani na nje ya nchi.
Ndege hiyo aina ya Embraer 190(E190) yenye hadhi ya VIP inatazamiwa kununuliwa toka nchi ya Morroco na Serikali ya Tanzania kupitia Wakala wa Ndege za Serikali (Tanzania Government Flight Agency)
Kwa nini wasinunue mpya kutoka kiwandani Brazil maana ni cheap ... au ndio kutengeneza mazingira ya rushwa

E-190_1.jpg


Embraer190_800.jpg
 
Kweli tumefikia mahali tunanunua mtumba kutoka kwenye nchi ya Africa/ wenzetu kabisaaaa..!!!!Ni shida gani hadi Morrocco watuuzie sisi ndege???.Molaa tusaidie.
 
Tunakwenda kununua ka mtumba toka morocco! ambayo itakuwa na lifespan ya around 5 yr a we nutty!
 
Duh! hii aibu, tunanunua mtumba kutoka Morroco? Sijui hawa viongozi huwa hawaoni haibu hii, kila siku mitumba mpaka lini?
 
Aina hiyo ya ndege zinatengenezwa brazil iweje ikanunuliwe morocco!! Hapa kunanunuliwa mtumba na ni kinyume na sheria ya manunuzi ya umma kumbukeni sababu ya kugomewa kununuliwa mitambo ya dowans.hii ni rushwa tu naomba wakiinunua ianguke iwaue!
 
Hii ni ajabu ya mwaka.
Serikali kununua ndege iliyotumika? tena Afrika? ...Hapana!...kuna tatizo kubwa mno somewhere.
Mimi nachukulia kuwa huu ni utani wa makabila yetu tu, hadi labda tuanze kula nyasi kiukweli.
Watanzania tunapenda utani na imetusaidia kujenga umoja na upendo, lakini si kwa masuala ya kiufundi na sensitive kama ya Aviation Sector.
 
Kwa maelezo yako,na details ulizoweka,jumlisha akili ya hawa watawala wetu, nadhani hii taarifa itakuwa kweli kabisa..lets wait and see..
 
hii ndo Tanzania kama huijui ndo ufahamu sasa, na hayo ndo mawazo ya viongozi wetu
 
serikali yetu imelogwa hakyanani
hivi tunaongozwa na vilaza hadi lini?
kama habari hii ni ya kweli basi kuna haja ya kuiondoa madarakani serikali hii ya vilaza waliosoma uchumi lkn hawajui uchumi.
what I know makampuni yanayotengeneza ndege unaweza kuagiza ndege na ukalipa kwa awamu
shame upon them........agrrrrrrrr wameharibu wekend yangu
 
Nasubiri hii habari iwe kamili sio tetesi ndio ntarudi kuchangia
 
Back
Top Bottom