Serikali kumjibu Lowassa kuhusu ajira...

bibikuku

JF-Expert Member
Feb 16, 2011
832
495
WAZIRI wa Kazi na Ajira, Gaudensia Kabaka amesema leo ataeleza mafanikio ya Serikali katika kutoa ajira kwa vijana ikiwa ni siku moja baada ya Waziri Mkuu aliyejiuzulu, Edward Lowassa kusema tatizo hilo ni bomu linalosubiri kulipuka na kuliomba Kanisa Katoliki liisaidie kutafuta ufumbuzi.

Juzi, akitoa salamu katika sherehe za uzinduzi wa Jimbo Jipya la Kanisa Katoliki la Ifakara, Morogoro, Lowassa alisema: “Nawaomba maaskofu katika miradi yenu mlipe kipaumbele suala la tatizo la ajira kwa vijana... wengi wanaohitimu elimu ya sekondari na vyuo wanakabiliwa na tatizo kubwa la ajira. Hili kama tulivyosema ni bomu linalosubiri kulipuka...”

Akizungumza na Mwananchi jana kuhusu tatizo hilo la ajira, Waziri Kabaka alisema leo atoa takwimu za ajira zilitolewa na Serikali kwa vijana na kueleza kile ambacho Serikali imekifanya na kuendelea kufanya katika kushughulikia tatizo la ajira nchini.

MY TAKE; Mapambano aliyoyasema Lowassa kuwa yuko tayari na fit huenda ndio yanaanza sasa
 
Yaaaani Serikali ya CCM wakimjibu Lowasa kwa kauri yake ya Ifakara hakika kumbe ni kweli Serikali ya CCM itakuwa INAMUOGOPA VIBAYA SANA EL.Hakika itakuwa kituko kwa kuwa Lowasa ataibua ajenda ambayo maskini kumbe CCM wasingefanya kaiz kwa style ya zima moto na mfumuko wa kizibo cha soda ya coca tusingepata Data za kuhoji na kuchimbua takwimu na uhalisia.

Aksante Lowasa kwa kuwa wanajamvi watapata takwimu na walioko arumelu watazitumia kuwakaanga CCM na style ya watendaji wa Kikwete kufanya kazi kwa kauri za kila wanasiasa kwenye majukwaa.

Mama huyo alikuwa wapi kutoa takwimu za ajira za vijana kabla ya dongo la LOWASA,kituko kingine ni kuwa watakuwa wameagiza haraka zitengenezwe kujibu Dongo na pasipo umakini zitamwagwa kisha wenye akili zao watazichambua kulinganisha na uhalisia kisha Lowasa atajibebea ujiko kuwa ni kiona mbali,wakati alikua ndani ya mechi hakuona chochote mpaka kocha wa timu alipomuweka benchi ndio leo kaona uchocholo wa kosa la wapi magoli yanaingilia.

Takwimu hizo wangetumia kabla kumtayalishia Jakaya na kumpa angekuwa ameshazitoa kwenye hotuba zake hata mbele ya wazee wa Dar es Salaam au kupitia hotuba zake za mwisho wa mwezi kuliko kusubilia madongo ya mwenzi wao.

Mama ziletee uone jamaa watakavyokugeuzia ubao!!!!!!! Kosa juu ya kosa basi kama ni paper professor atakuwa anapata shida kujua atamsaidia undergraduate wake vipi.
 
Yaaaani Serikali ya CCM wakimjibu Lowasa kwa kauri yake ya Ifakara hakika kumbe ni kweli Serikali ya CCM itakuwa INAMUOGOPA VIBAYA SANA EL.Hakika itakuwa kituko kwa kuwa Lowasa ataibua ajenda ambayo maskini kumbe CCM wasingefanya kaiz kwa style ya zima moto na mfumuko wa kizibo cha soda ya coca tusingepata Data za kuhoji na kuchimbua takwimu na uhalisia.

Aksante Lowasa kwa kuwa wanajamvi watapata takwimu na walioko arumelu watazitumia kuwakaanga CCM na style ya watendaji wa Kikwete kufanya kazi kwa kauri za kila wanasiasa kwenye majukwaa.

Mama huyo alikuwa wapi kutoa takwimu za ajira za vijana kabla ya dongo la LOWASA,kituko kingine ni kuwa watakuwa wameagiza haraka zitengenezwe kujibu Dongo na pasipo umakini zitamwagwa kisha wenye akili zao watazichambua kulinganisha na uhalisia kisha Lowasa atajibebea ujiko kuwa ni kiona mbali,wakati alikua ndani ya mechi hakuona chochote mpaka kocha wa timu alipomuweka benchi ndio leo kaona uchocholo wa kosa la wapi magoli yanaingilia.

Takwimu hizo wangetumia kabla kumtayalishia Jakaya na kumpa angekuwa ameshazitoa kwenye hotuba zake hata mbele ya wazee wa Dar es Salaam au kupitia hotuba zake za mwisho wa mwezi kuliko kusubilia madongo ya mwenzi wao.

Mama ziletee uone jamaa watakavyokugeuzia ubao!!!!!!! Kosa juu ya kosa basi kama ni paper professor atakuwa anapata shida kujua atamsaidia undergraduate wake vipi.

kwa hali hii hadi serikali kukurupuka na kutaka kumjibu, nadhani madai ya EL yatakuwa na hoja hivyo serikali inataka kufukia mashimo
 
Back
Top Bottom