Serikali iwanusuru wafanyakazi

Serikali iwanusuru wafanyakazi

Aman Ng'oma

JF-Expert Member
Joined
Nov 8, 2011
Posts
966
Reaction score
537
Hali ya maisha kwa wafanyakazi wa kada za chini ni duni sana.Hali hii inatokana na viwango vya mishahara visivyokidhi mahitaji yao.Hakuna uwiano sawa wa viwango vya mishahara kati ya wafanyakazi wa kada fulani na nyingine.

Maisha ya sasa hivi ni magumu na kwa viwango hivi vya mishahara vinawakatisha tamaa wafanyakazi wengi matokeo yake ari ya utendaji wa kazi unapungua.Tusitarajie maendeleo kutoka kwa wafanyakazi waliokata tamaa ndio maana kila siku mambo yatazidi kuharibika tu,mfano mzuri tazama secta ya elimu,namna ambayo wanafunzi walivyofeli.

Tutaunda tume nyingi sana,lakini kama stahiki za wafanyakazi hazitatazamwa tutarajie mambo kwenda kombo zaidi kila leo.Hii nchi yakwetu sote na lazima matunda yake yaliwe na wote.

Viongozi wetu wamekuwa wabinafsi wanaojijali zaidi wenyewe .Kama tukihitaji ufanisi lazima tukubali wafanyakazi wanapata stahiki zao za mishara inayokidhi mahitaji yao.Mfanyakazi anayelia njaa hawezi akafanya kazi kwa moyo,hivyo nchi itaendelea kuwa masikini.

Kama serikali itaamua, ina uwezo mkubwa sana wa kuwaondolea manung'uniko wafanyakazi.

Pia serikali iangalie namna bora ya malipo ya mishahara,kama inafuata viwango vya TGS,basi iwe kwa ngazi zote bila kujali huyu mbunge,waziri ,hakimu au mwalimu.Mfanyakazi alipwe mshahara kulinana na elimu yake. Hapo nadhani manung'uniko kwa wafanyakazi yataisha.
 
Kama mishahara ya watumishi wa serikali serikali imefikia hatua ya kukopa ndipo iwalipe watumishi wake habari ya kuongeza mishahara ni ndoto na msahau.
 
lakini hii mifanyakazi ya Tanzania ni shida tupu. hayana ubunifu na yanafanyia kazi kimazoea tu karibia ofisi zote utakazoenda. hakuna ufanishi kabisa. ingekuwa amri yangu wala nisingewaongezea mishahara mpaka watie akili juu ya uwajibikaji kwenye majukumu yao yanayoambatana na ufanishi.
 
Hebu jaribu kufuatilia viwango vya mishahara katika hizo zinazoitwa "LDC" halafu uje hapa ueleze tena. Viwango vya mshahara lazima viwe backed-up na uchumi wa nchi, uchumi wetu mbovu hao chichiemu wameshindwa kuja na uchumi imara so kabla ya kulalamika mishahara kwanza unganeni nyi wafanyakazi muitoe chichiemu, hata kama chama kitakachokuja kushika dola ni cha dovutwa, but kwanza magamba wakae pembeni mengine yafuate.
 
lakini hii mifanyakazi ya Tanzania ni shida tupu. hayana ubunifu na yanafanyia kazi kimazoea tu karibia ofisi zote utakazoenda. hakuna ufanishi kabisa. ingekuwa amri yangu wala nisingewaongezea mishahara mpaka watie akili juu ya uwajibikaji kwenye majukumu yao yanayoambatana na ufanishi.
Afanye ubunifu ili iweje kama atakachofikiria na kukibuni na kukishauri kinaenda kuishia kwenye mafaili na walio juu yao kufanya walioshauriwa na wapenzi wao. Usicheze serikali hiyo kufanyia kazi, ngumu kinoma, hakuna kabisa kitu kinachoitwa ubunifu. Ni fanya twende tu.
 
lakini hii mifanyakazi ya Tanzania ni shida tupu. hayana ubunifu na yanafanyia kazi kimazoea tu karibia ofisi zote utakazoenda. hakuna ufanishi kabisa. ingekuwa amri yangu wala nisingewaongezea mishahara mpaka watie akili juu ya uwajibikaji kwenye majukumu yao yanayoambatana na ufanishi.

akili yako ya kimbululambulula na uwezo wako wa kufikiri na wakiwasilisha mawazo nao wa kimbululambulula tu.Ila sikushaghai kwavile kazi yako inaimudu vizuri humu,kwa kupinga na kutetea serikali yako ccm endelea. Siunafahamu ukisha post unakwenda kulipwa pale limumba.
 
Hata kura zenu hazitakiwi na Magamba.sasa mshahara muongezwe kwa ajili ya kitu gani?.
 
lakini hii mifanyakazi ya tanzania ni shida tupu. Hayana ubunifu na yanafanyia kazi kimazoea tu karibia ofisi zote utakazoenda. Hakuna ufanishi kabisa. Ingekuwa amri yangu wala nisingewaongezea mishahara mpaka watie akili juu ya uwajibikaji kwenye majukumu yao yanayoambatana na ufanishi.

ufanisi mkuu hauwezi kuja ukiwa na njaa
 
lakini hii mifanyakazi ya
Tanzania ni shida tupu. hayana ubunifu na yanafanyia kazi kimazoea tu
karibia ofisi zote utakazoenda. hakuna ufanishi kabisa. ingekuwa amri
yangu wala nisingewaongezea mishahara mpaka watie akili juu ya
uwajibikaji kwenye majukumu yao yanayoambatana na ufanishi.
nakuunga mkono asilimia mia, mifanyakazi haitulii ofisini kutwa kwenye ishue binafsi watabuni saa ngapi mambo mapya, stori ofisini ndo code of ethics zao. lakini pia wanatakiwa kufahamu mishahara haiwezi kuringana kati ya kada moja hadi nyingine. tuwe wabunifu sio kutaka tu mishahara mikubwa
 
lakini hii mifanyakazi ya Tanzania ni shida tupu. hayana ubunifu na yanafanyia kazi kimazoea tu karibia ofisi zote utakazoenda. hakuna ufanishi kabisa. ingekuwa amri yangu wala nisingewaongezea mishahara mpaka watie akili juu ya uwajibikaji kwenye majukumu yao yanayoambatana na ufanishi.

Mjomba ndio maana na wao hawana mzuka wa kufanya kazi kwa bidii,ajitume kwa lipi analopata?,ndo maana anazuga huku akipiga dili zake zingine,we fikiria mkuu,mazingira ya kazi hayaeleweki,sometimes unatakiwa kuhudumia watu walioko mbali na hapo makao makuu ya ofisi ilipo,kama huwezeshwi atatumia mshahara wake kwenda huko?,mtu anaamua tu kuhudumia taasisi zilizo karibu na eneo lake,zilizo mbali anazipotezea au labda zimuwezeshe kwenda kule kufanya hizo kazi,kuna factors nyingi mno mkuu zinazowafanya watumishi wa serikali wasiperform vizuri,ukimwona mtumishi anaperform vizuri mfuatilie vizuri utagundua yupo kwenye kitengo kinachomwezesha vema afanye kazi zake poa
 
mshahara mdogo alafu hauji kwa wakatai. wa feb haujatoka kwa watumishi wengi alaf unategemea wajitume, wawe wabunifu?
 
Back
Top Bottom