Serikali isituingize tena mkenge....

Mohammed Hamad

JF-Expert Member
Jan 17, 2011
3,988
1,304
Nimesoma taarifa ya bwana Felichesmi Mramba kaimu Mkurugenzi mkuu wa Tanesco na ninamnukuu
Alisema shirika linawasiliana na serikali kuangalia uwezekano wa kupata mitambo ya dharura ili kukabiliana na hali inayoweza kujitokeza endapo mvua za masika zitakuwa chini ya wastani.

"Tunajua wananchi wanatuchukia sana kwa sasa hivi lakini hata sisi tunasikitika kwa mgao huu unaoendelea na tunajua unaleta hasara kwa taifa,''alisema. Pia kwa mujibu wa Mramba, kutokana na mgawo huo shirika la umeme mpaka limeshapata hasara ya shilingi bilioni 3.

Napenda kuchukua fursa hii adhimu kuishauri Serikali kuwa hili swala la umeme ni nyeti sana na limeongelewa sana watu wametoa ushauri lakini Serikali imetia pamba masikioni. Sote tunakumbuka Mwakyembe aliwapa ushauri Serikali hasa Tanesco kuwa na mipango ya muda mrefu kutatua hili suala la umeme na sio kusubiri hali inakuwa mbaya then wanakimbilia mipango ya dharura. Nadhani Serikali haikulifanyia kazi pendekezo la kina Mwakyembe na sasa I can smell another RICHMOND/DOWANS. Sitaki tufike huko na CCM na Serikali yake lazima wajue kuwa hata wakereketwa na wanaCCM kindakindaki wanaumia na hii hali labda huyo mkereketwa awe "majinuni" asihisi machungu ya huu mgao.

Nina imani watu wamechoka na Tanesco wanatamani ibinafsishwe au Serikali iruhusu umeme uwe kama secta ya mawasiliano iruhusu kampuni nyingi kuendesha hii biashara kama ilivyoruhusu makampuni ya simu.

Mwisho kabisa napenda kumalizia TUMECHOKA tunataka UMEME isifike wakati tukakosa uvumilivu!
 
Back
Top Bottom