Serikali isipandishe mishahara!

Serikali isipandishe mishahara!

Tulimumu

JF-Expert Member
Joined
Mar 11, 2013
Posts
14,395
Reaction score
13,266
Wafanyakazi na watu wengi wamekuwa wakidai kupandishwa kwa mishahara kama suluhu la kupunguza au kuondoa ugumu wa maisha. Mimi nina mawazo tofauti na hayo. Kama ingekuwa kupanda kwa mishahara ndio suluhisho la ugumu wa maisha, basi kusingekuwa na tatizo tena.

Mimi nashauri serikali isipandishe mishahara badala yake idhibiti mfumuko wa bei na kushusha kodi katika bidhaa za mafuta na mishahara ya wafanyakazi ili kuleta nafuu ya maisha. Utaratibu huu utawanufaisha hata wasiokuwa na ajira rasmi ya kutegemea mishahara.

Sasa hivi baada ya fununu ya kupandisha mishahara kutoka nauli zimepanda kabla hata ya mshahara mpya. Hii ina maana hata huduma na bidhaa nyingine zitapanda au zimepanda kwa usafiri ndio kiungo cha mahitaji yote. Kupandisha nauli hakuna tofauti na kupandisha bei ya mafuta. Sasa hata mishahara ikipanda faida yake itakuwa ni nini wakati nyongeza itakuwa imemezwa mara mbili au tatu kutokana na kupanda kwa mishahara? Wakati huo huo huduma mbali mbali zitapanda kama kodi za nyumba.

Hapa ndipo ninapomkumbuka Mkapa ambaye hakuwa akipandisha mishahara kila wakati bali alidhibiti mfumuko wa bei na nafuu ilikuwa kubwa kuliko kupandisha mishahara. Hvyo wito wangu kwa wafanyakazi na vyama husika ni kuibana serikali idhibiti mfumuko wa bei na kushusha kodi ya PAYE lakini kuongeza mishahara sio suluhisho! Mishahara ikipanda kila kitu kitapanda kwa kisingizio cha kupanda kwa mishahara na ushahidi wa hili ni kupanda kwa gharama za usafiri kabla ya kupanda kwa mishahara. Sasa ongezeko la mishahara litakuwa na faida gani wakati tayari gharama zimepanda kabla yake.

Kama ingekuwa mishahara ikipanda vitu vinabaki na bei ile ile bila kupanda, maana ya kupanda kwa mishahara ingekuwepo. Balaa la sasa ni kuwa asilimia ya ongezeko la gharama za usafiri inaweza kuwa kubwa kuliko ongezeko la mishahara lililoahidiwa. Hili ni rahisi wala halihitaji digrii kujua. Hivyo kama serikali iko makini isitishe gharama mpya za usafiri, ishushe kodi ya PAYE, idhibiti mfumuko wa bei katika bidhaa za mafuta, umeme na vyakula bila shaka hali itakuwa nzuri. Kumbukeni wakati mdai mishahara mipya tayari Tanesco nao wanataka kuongeza gharama za umeme. Mishahara ikiongezeka watatumia kama sababu ya kuongeza gharama kwakuwa nao itawabidi kulipa mishahara mipya.

Hivyo kwa kutazama hali ya maisha ya Tanzania itakuwa ni kosa kubwa kupandisha mishahara bila kudhiti mfumuko wa bei za vitu na kwa kuwa tayari serikali yenyewe imeshaanza kwa kuongeza gharama za usafiri, itazuia vipi wenginie kuongeza bei za huduma zao. Mkapa bado yupo hebu serikali imtumie kwasababu sisi walipa kodi ndio tunaendelea kugharimia maisha yake mpaka atakapo kufa. Fuateni sera yake ya kudhibiti mfumuko wa bei bila kuongeza mishahara.

Kitu kingine kilicho wazi ni kuwa mishahara ikipanda maana yake na thamani ya shilingi inashuka! Kwa hiyo tutakuwa na hela nyingi zisizoweza kukidhi mahitaji. Tusipokuwa makini tutakuwa kama kisiwa cha Zimbabwe kama Mulugo alivyo alivyosema
 
Nashangaa kwanin watu wanashindwa kuchangia mada za maslai ya maendeleo ya taifa kama hii na badala yake wanapoteza muda kwa kubishana maswala ya vyama...mkubwa kuhusiana na hilo nakuunga mkono kabisa, imefika wakati sasa nchi(kiongozi wa nchi) kuchukua ushauri unaohusiana na kupunguza ukali wa mfumuko wa bei kupitia kwa viongozi waliopita ambao walifanikiwa kwa hilo..

Kikwete acha kulalama kwenye vyombo vya habari, chapa kazi.

Mpenda maendeleo ya nchi ya tanzania, mungu ibariki tanzania yetu!

Sent from my BlackBerry 9320 using JamiiForums
 
Tatizo familia za watawala wetu ni wafanya biashara za mafuta na usafirishaji wa abiria na mizigo, hiyo mishahara mipya ni "JUSTIFICATION" ya kupiga deal kwenye biashara zao. Hao wafanya kazi wapo wangapi TZ mpaka uongeze nauri na mafuta kwa kigezo cha ongezeko la mishahara?
 
Unashauri washushe wenzio ndio wanapandisha mtakoma kwa kuichagua ccm vibaka,
 
Mkuu nadhani wafanyakazi huwa wanalalamika utofauti wa vima vya mshahara kati ya wafanyakazi wa ngazi za juu na wale wa ngazi za chini.
 
ukweli haupigiki utabaki daima maana maisha yako juu sana kwa sasa hata wakipandisha haitasaidia kikubwa mfumko wa bei ndio ushushwe na si mishahara
 
Mkuu tembelea Filling Station uone jinsi wadau walivyo fasta kupandisha, toka Tsh. 2050 mpaka Tsh. 2085 kwa Petrol.
 
hivi kweli ccm wamekubali kumwacha jk akizike kabisa chama chao huku wakimwangalia?jamaa is a total failure na hajui hata anaipeleka wapi nchi.watu kama Mkapa wangeingilia kati kuiendesha nchi maana jamaa kashindwa kabisa na tukisema tumvumilie hadi mwisho wa kipindi chake nchi itaangamia na itatuchukua miaka mingi sana kuirudisha kwenye ramani ikasimama.huyu mtu hata kujitambua hajitambui ni sawa na mgonjwa ambaye yuko nusu kaputi.sasa bado eti tunamwamini atuongoze.above all,tunawafikiriaje ambao wapo sekta isiyo rasmi?wataishije?
 
Haaswaaa! Umenikumbusha mambo ya price floor na ceiling!
 
Pawe na usawa wa kima cha mishahara baina ya sekta moja na nyingine
 
Mkuu umeongea zaidi ya ukweli, hakuna haja ya kulipwa mapesa mengi huku matumizi yake yakiwa makubwa kuliko fedha zenyewe....Tudhibiti mfumuko wa bei na kama tukiushusha ni wazi tutakuwa tumewaongezea wafanyakazi kiasi kikubwa cha mshahara kwani watasalia na chochote ktk kazi zao. Nampongeza hapmpoma kwa nakisi yake kwani ukifungua zile thread zenye mabishano ya kisiasa utawakuta wasomi wetu wengi wanasodoana ila haya yanayowagusa moja kwa moja hata page 1 haijai.
 
Uko sawa,kwani hata dhumuni la kutangaza nyongeza ya mshahara ni mchezo wa panya wa kung'ata na kupuliza ili BUDGET ipite bila kupigiwa kelele na wananchi haswa tukizingatia mabadiliko ya kukaa kwa bunge la bajeti kunawapa kimuhemuhe.
 
huu ushauri jk hawezi kukusikiliza, labda umshauri jinsi ya kuidhibiti chadema. we angalia vitu wanavyoongea akina Wassira,Mwigulu na Nappe ndio vitu anavyovitaka mkulu.!!!
 
Nakifikiri suala la uchumi lisijadiliwe kichama.Pia nakifiri hata kama mchumi yuko upinzani achaguliwe kuwa waziri wa uchumi.Hii dhana ya kuchagua mawaziri toka chama tawala tunakosa mengi.Ebu vichwa vilivyobobe tunusuru. Umeme ,maji,naulli viko juu hivyo hata ukiongeza mshahara ni kazi bure.Kumbuka enzi za Idi Amini wananchi waliposema hali mbaya alisema PRINT MORE MONEY.
 
Tatizo ni viongozi wetu/ndugu zao kuwa ndani ya uongozi na kuchanganya na biashara ndio kitu kinachotutesa sisi watz kwasababu ni lazima waangalie faida za biashara zao kwa kupitia mfumo wa kudanganya umma kuwa mshahara unasuluhisho la kufanya maisha kuwa rahisi kwa wote,huku wakijua kuwa hiyo ni mbinu ya kuchukua hata kile kidogo walichonacho wananchi wa nchi hii,eeeh Mungu ona tunavyo fanywa waja wako,Tufanye tuwe wenye kuona,kusikia,kuamini au kutoamini ili tuwe na maamuzi sahihi kwa manufaa ya nchi yetu
 
Kutoongeza mishahara kiuchumi kunalenga kupunguza kiasi cha fedha mikononi mwa watu ili hiyo iliyopo kidogo ilazimishe upunguaji wa bei za bidhaa na huduma. Hiyo ni sayansi ya kiuchumi lakini je, inafanya kazi hivo katika mazingira ya Tanzania?? Jibu ni hapana!! Serikali haijaweza kudhibiti inflation na hili linafanya watu watumie pesa nyingi katika kidogo walizonazo hivo kushindwa kufanya hata savings!!

Ninaunga mkono kwa mishahara kupanda hata kama net gain itakuwa zero! Kwa sababu savings za wafanyakazi zinapungua katika mazingira ya sasa. Ni baada ya hapo tu ndio inflation management ianze na ndipo savings zitaanza kupanda tena.

Tunajenga taifa la "from pocket to mouth" na kushidwa kugharimia mambo ya mbeleni kama maandalizi ya uzeeni (wakati mtu hana kazi), savings kwa ajili ya elimu ya watoto na mambo ya ghafla kama maradhi, tozo za kisheria (faini za mahakamani) na kadhalika.
 
hata mimi nakuunga mkono Mkuu, hali inakoelekea ni kubaya dalili la ongezeko la umaskini i wazi..Wachache wanakaa wanaamua maisha ya watu kwa kupiga madili.. nchi inaongozwa kwa madili..
 
Swala kama hili na mengine yanayohusu maslahi ya wafanyakazi yanapaswa kuwa adressed na TUCTA lakini TUCTA amebaki mbwa asiye na meno! umewahi kumsikia tena Mgaya? kazi kukata mishahara yetu kuchangia vyama vya wafanyakazi!Utawasikia Mei Mosi na hotuba kubwa kubwa na madai mengi halitekelezwi hata moja mwaka mwingine wanakuja na mengine! Mtu akate pesa yangu safari hii ninaye nimechoka!!
 
Naunga Hoja, Kikubwa kwa Viongozi aka Watawala wetu, ni kudhibiti Mfumuko wa Bei, ili mwananchi wa chini aweze kumudu hali ya maisha.


Wafanyakazi na watu wengi wamekuwa wakidai kupandishwa kwa mishahara kama suluhu la kupunguza au kuondoa ugumu wa maisha. Mimi nina mawazo tofauti na hayo. Kama ingekuwa kupanda kwa mishahara ndio suluhisho la ugumu wa maisha, basi kusingekuwa na tatizo tena.

Mimi nashauri serikali isipandishe mishahara badala yake idhibiti mfumuko wa bei na kushusha kodi katika bidhaa za mafuta na mishahara ya wafanyakazi ili kuleta nafuu ya maisha. Utaratibu huu utawanufaisha hata wasiokuwa na ajira rasmi ya kutegemea mishahara.

Sasa hivi baada ya fununu ya kupandisha mishahara kutoka nauli zimepanda kabla hata ya mshahara mpya. Hii ina maana hata huduma na bidhaa nyingine zitapanda au zimepanda kwa usafiri ndio kiungo cha mahitaji yote. Kupandisha nauli hakuna tofauti na kupandisha bei ya mafuta. Sasa hata mishahara ikipanda faida yake itakuwa ni nini wakati nyongeza itakuwa imemezwa mara mbili au tatu kutokana na kupanda kwa mishahara? Wakati huo huo huduma mbali mbali zitapanda kama kodi za nyumba.

Hapa ndipo ninapomkumbuka Mkapa ambaye hakuwa akipandisha mishahara kila wakati bali alidhibiti mfumuko wa bei na nafuu ilikuwa kubwa kuliko kupandisha mishahara. Hvyo wito wangu kwa wafanyakazi na vyama husika ni kuibana serikali idhibiti mfumuko wa bei na kushusha kodi ya PAYE lakini kuongeza mishahara sio suluhisho! Mishahara ikipanda kila kitu kitapanda kwa kisingizio cha kupanda kwa mishahara na ushahidi wa hili ni kupanda kwa gharama za usafiri kabla ya kupanda kwa mishahara. Sasa ongezeko la mishahara litakuwa na faida gani wakati tayari gharama zimepanda kabla yake.

Kama ingekuwa mishahara ikipanda vitu vinabaki na bei ile ile bila kupanda, maana ya kupanda kwa mishahara ingekuwepo. Balaa la sasa ni kuwa asilimia ya ongezeko la gharama za usafiri inaweza kuwa kubwa kuliko ongezeko la mishahara lililoahidiwa. Hili ni rahisi wala halihitaji digrii kujua. Hivyo kama serikali iko makini isitishe gharama mpya za usafiri, ishushe kodi ya PAYE, idhibiti mfumuko wa bei katika bidhaa za mafuta, umeme na vyakula bila shaka hali itakuwa nzuri. Kumbukeni wakati mdai mishahara mipya tayari Tanesco nao wanataka kuongeza gharama za umeme. Mishahara ikiongezeka watatumia kama sababu ya kuongeza gharama kwakuwa nao itawabidi kulipa mishahara mipya.

Hivyo kwa kutazama hali ya maisha ya Tanzania itakuwa ni kosa kubwa kupandisha mishahara bila kudhiti mfumuko wa bei za vitu na kwa kuwa tayari serikali yenyewe imeshaanza kwa kuongeza gharama za usafiri, itazuia vipi wenginie kuongeza bei za huduma zao. Mkapa bado yupo hebu serikali imtumie kwasababu sisi walipa kodi ndio tunaendelea kugharimia maisha yake mpaka atakapo kufa. Fuateni sera yake ya kudhibiti mfumuko wa bei bila kuongeza mishahara.

Kitu kingine kilicho wazi ni kuwa mishahara ikipanda maana yake na thamani ya shilingi inashuka! Kwa hiyo tutakuwa na hela nyingi zisizoweza kukidhi mahitaji. Tusipokuwa makini tutakuwa kama kisiwa cha Zimbabwe kama Mulugo alivyo alivyosema
 
Back
Top Bottom