Serikali irudishe ada mashuleni

Serikali irudishe ada mashuleni

nguruka wa kig0ma

JF-Expert Member
Joined
Jan 16, 2020
Posts
2,943
Reaction score
2,934
Saalam!

Ni muda mrefu sasa Watanzania wakilalamikia michango mashuleni bila majibu ya serikali.

Malalamiko yanatoka na kukizana kwa kauli za viongozi wa kuu wa nchi na utendaji wa viongozi wa halmashauri zetu na wakuu wa shule za serikali.

Viongozi wakuu wanasema elimu bure na asiwepo Mwananchi kudaiwa michango.

Viongozi Halmashauri na wakuu wa shule za serikali wanasema matamko ya viongozi wa juu ni siasa tu.

Hali hii inasababisha chuki kati ya wazazi na walimu, kwani mzazi akishasikia hakuna michango, ni lazima amuhoji mwalimu atakayemwambia achangie dawati au ujenzi wa uzio/ madarasa

Chuki hizo huendelea, walimu wakifahamu kuwa mzazi wa mwanafunzi fulani ndiye aliyekuwa anahoji na kupinga michango kwenye vikao, mwanafunzi huyo hatasoma kwa amani, hasira za walimu huamia kwa watoto.

Ni wakati sasa serikali kuweka Jambo hili sawa.

Serikali imeshindwa kutekeleza sera ya elimu bure, irudishe ada mashuleni ili shule ziwezekujiendesha.

Maana ukipiga hesabu utakuta zaidi ya laki tatu mzazi anatoa kwa ajili ya mwanafunzi kwa mwaka.

Dawati
Ujenzi wa madarasa/uzio
Nembo
Faili la mwanafunzi
Rimu nk.
Kwa lugha rahisi shule siyo za serikali Bali ni shule za wananchi

SERIKALI RUDISHA ADA MASHULENI
 
Upo sahihi lakini haliwezi kutokea. WHY?

Hatuna ujasiri wa kukiri udhaifu. Ndiyo sifa yetu kuu. Tazama ishu ya "koona" utaelewa nachosema.
 
VIPI MNAONAJE TUMKOPESHE MITANO TENA AENDELEE MPAKA 2030 AU???

Hivi ni raisi gani ambaye aliwahi kupendwa na wananchi wake kiroho safi? Maana jiwe mi naona saivi anakubalika 0.00000000001% sababu kuu ni Kodi kubwa biashara zinakufa.

Mikopo ya elimu ya juu ile 6% ni kipele cha mkundi( hapo kwenye 'i' weka 'u') na nyongeza ya mishahara kwa watumishi unafanya kazi miaka saba mshahara uko vilele haiwezekani maisha ya mwaka 2014 yawe sawa na 2021.
 
Hilo SAHAU!! Yaani aonekane ameshindwa kutoa ELIMU BURE kwa watoto wa WANYONGE wake!!!
 
Saalam!

Ni muda mrefu sasa Watanzania wakilalamikia michango mashuleni bila majibu ya serikali.

Malalamiko yanatoka na kukizana kwa kauli za viongozi wa kuu wa nchi na utendaji wa viongozi wa halmashauri zetu na wakuu wa shule za serikali.

Viongozi wakuu wanasema elimu bure na asiwepo mwananchi kudaiwa michango.

Viongozi halmashauri na wakuu wa shule za serikali wanasema matamko ya viongozi wa juu ni siasa tu.

Hali hii inasababisha chuki kati ya wazazi na walimu, kwani mzazi akishasikia hakuna michango, ni lazima amuhoji mwalimu atakayemwambia achangie dawati au ujenzi wa uzio/ madarasa

Chuki hizo huendelea, walimu wakifahamu kuwa mzazi wa mwanafunzi fulani ndiye aliyekuwa anahoji na kupinga michango kwenye vikao, mwanafunzi huyo hatasoma kwa amani, hasira za walimu huamia kwa watoto.

Ni wakati sasa serikali kuweka Jambo hili sawa.

Serikali imeshindwa kutekeleza sera ya elimu bure, irudishe ada mashuleni ili shule ziwezekujiendesha.

Maana ukipiga hesabu utakuta zaidi ya laki tatu mzazi anatoa kwa ajili ya mwanafunzi kwa mwaka.

Dawati
Ujenzi wa madarasa/uzio
Nembo
Faili la mwanafunzi
Rimu nk.
Kwa lugha rahisi shule siyo za serikali Bali ni shule za wananchi

SERIKALI RUDISHA ADA MASHULENI
Ujumbe mzito huu. Walio karibu na sekta ya Elimu wataelewa zaidi ujumbe wako. Mahusiano ya walimu, wazazi na watendaji wa serikali wa ngazi za chini ikiwemo watendaji wa kata,vijiji n.k. ni tete kutokana na sintofahamu kubwa iliyopo katika michango.

Matamko na maelekezo kwa umma katika majukwaa ya siasa na uhalisia ni vitu viwili tofauti. Tusifanye SI-HASA katika elimu, katika maendeleo ya Taifa letu. Kwa hali ilivyo sasa, hakika serikali bila kushirikisha umma kuchangia maendeleo yao hususan Elimu tutaliangiza Taifa na umasikini utazidi kutopea.
 
Saalam!

Ni muda mrefu sasa Watanzania wakilalamikia michango mashuleni bila majibu ya serikali.

Malalamiko yanatoka na kukizana kwa kauli za viongozi wa kuu wa nchi na utendaji wa viongozi wa halmashauri zetu na wakuu wa shule za serikali.

Viongozi wakuu wanasema elimu bure na asiwepo Mwananchi kudaiwa michango.

Viongozi Halmashauri na wakuu wa shule za serikali wanasema matamko ya viongozi wa juu ni siasa tu.

Hali hii inasababisha chuki kati ya wazazi na walimu, kwani mzazi akishasikia hakuna michango, ni lazima amuhoji mwalimu atakayemwambia achangie dawati au ujenzi wa uzio/ madarasa

Chuki hizo huendelea, walimu wakifahamu kuwa mzazi wa mwanafunzi fulani ndiye aliyekuwa anahoji na kupinga michango kwenye vikao, mwanafunzi huyo hatasoma kwa amani, hasira za walimu huamia kwa watoto.

Ni wakati sasa serikali kuweka Jambo hili sawa.

Serikali imeshindwa kutekeleza sera ya elimu bure, irudishe ada mashuleni ili shule ziwezekujiendesha.

Maana ukipiga hesabu utakuta zaidi ya laki tatu mzazi anatoa kwa ajili ya mwanafunzi kwa mwaka.

Dawati
Ujenzi wa madarasa/uzio
Nembo
Faili la mwanafunzi
Rimu nk.
Kwa lugha rahisi shule siyo za serikali Bali ni shule za wananchi

SERIKALI RUDISHA ADA MASHULENI
Hivi ni moja ya maelfu ya viini macho vya awamu hii ya hovyo.
 
Saalam!

Ni muda mrefu sasa Watanzania wakilalamikia michango mashuleni bila majibu ya serikali.

Malalamiko yanatoka na kukizana kwa kauli za viongozi wa kuu wa nchi na utendaji wa viongozi wa halmashauri zetu na wakuu wa shule za serikali.

Viongozi wakuu wanasema elimu bure na asiwepo Mwananchi kudaiwa michango.

Viongozi Halmashauri na wakuu wa shule za serikali wanasema matamko ya viongozi wa juu ni siasa tu.

Hali hii inasababisha chuki kati ya wazazi na walimu, kwani mzazi akishasikia hakuna michango, ni lazima amuhoji mwalimu atakayemwambia achangie dawati au ujenzi wa uzio/ madarasa

Chuki hizo huendelea, walimu wakifahamu kuwa mzazi wa mwanafunzi fulani ndiye aliyekuwa anahoji na kupinga michango kwenye vikao, mwanafunzi huyo hatasoma kwa amani, hasira za walimu huamia kwa watoto.

Ni wakati sasa serikali kuweka Jambo hili sawa.

Serikali imeshindwa kutekeleza sera ya elimu bure, irudishe ada mashuleni ili shule ziwezekujiendesha.

Maana ukipiga hesabu utakuta zaidi ya laki tatu mzazi anatoa kwa ajili ya mwanafunzi kwa mwaka.

Dawati
Ujenzi wa madarasa/uzio
Nembo
Faili la mwanafunzi
Rimu nk.
Kwa lugha rahisi shule siyo za serikali Bali ni shule za wananchi

SERIKALI RUDISHA ADA MASHULENI
nakubaliana na wewe 100%
 
Back
Top Bottom