Viongozi wa juu wa kitaifa wanahitaji mahitaji maalumu kila waendapo na yanahusisha gharama. Misafara yao na wasaidizi wao. Ikiwa hilo halitoshi wenyeji nao wana misafara yao kila panapokuwa na tukio linalohusisha kiongozi mkuu. Hivi kweli ni sawa.
- Waziri mkuu kuandaliwa rasmi shughuli ya kugawa vishkwambi? Pangetolewa muongozo wa ugawaji si ingetosha!
- Kila mwaka serikali inanunua magari na pikipiki. Hivi kweli ni sahihi kumtumia Makamu wa Raisi kugawa vitu kama hivi?
Hebu wakubwa zetu mambo mengine yafuate taratibu tu labda iwe kama kuna kutafuta political mileage na si utendaji wa kawaida wa serikali.