Serikali inaposhindwa kutoa ajira mpya kwa kigezo cha Uhakiki wa watumishi

Kang kin

Senior Member
Mar 21, 2017
154
122
Salaam
Kama kichwa kinavyoeleza ni mwaka wa pili sasa serikali haijatoa ajira wala kupandisha mishahara na vyeo kwa watumishi kwa kigezo kwamba bado inafanya uhakiki wa watumishi hewa hakuna anayepinga kwamba zoezi hili si jema.

Baada ya Mhe. Rais kukabidhiwa ripoti ya watumishi hewa watanzania wengi walipata matumaini kwamba zoezi hili limefikia ukomo badala yake hivi karibuni mawaziri wanasimama majukwaani na kuuambia umma kwamba uhakiki bado unaendelea, madhalani kauli zao zimekuwa zikibadilika mara kwa mara,

Wakati Mhe. Simbachawene akijibu swali bungeni kuhusu upungufu wa watumishi uliojitokeza baada ya uhakiki aliahidi kwamba mwez june ajira zingetangazwa kuziba pengo kwa watumishi waliokutwa na vyeti feki lakini kauli ya mhe.Angela kairuki ya hivi karibuni ajira hizo ni mwezi august sasa swali la kujiuliza serikali moja lugha tofauti kuna nn?.

Bila shaka japo jambo hili la ajira na kupandisha mishahara na vyeo halijapewa kipaumbele watanzania wengi wanayo maswali kadhaa mioyoni mwao.

1.Je, kwa mwaka wa fedha ulipoita 2016/2017 serikali ilipanga kuajiri na ikatenga fungu kwa ajili ya watumishi wapya na badala yake haikuajiri kama ilivyo kusudia kwa kigezo cha uhakiki hizo hilo fungu lilienda wapi?

2. Ikiwa Rais alikabidhiwa ripoti ya watumishi hewa kauli za mawaziri kwamba uhakiki bado unaendelea ripoti iliyotolewa na yenyewe ni feki tusubiri original?

3. Ikiwa watanzania wanalipa kodi na bado kuna upungufu wa watumishi zahanati, mashuleni n.k na kwann hawapati huduma stahiki kwa sababu niwalipa kodi?

4. Je, kwanini serikali isitangaze kufuta baadhi ya Degree, Diploma na certificate programme kwa sababu hakina mpango wa kuajili mfano Ualimu wa sanaa?.

Mtazamo wangu.
1. Mawaziri wenye dhamana na masuala ya ajira na utumishi ni vizuri wakae kimya kuliko kutoa matamko tata kila itwapo leo.
2. Serikali itamke wazi kwamba haina mpango wa kuajiri kwa kipindi cha miaka kadhaa kuliko kuja na siasa za danganya toto kila kukicha.

3. Serikali itangaze mwisho wa zoezi la uhakiki ni lini.
4. Serikali iache kujificha kwenye koti la uhakiki itamke wazi nini kinasibu mpaka isitoe ajira mpya.

5. Serikali itoe mikopo isiyo na riba kwa wahitimu wenye uhitaji wa mikopo ili waweze kujiajiri wao wenyewe kuliko kuwaambia wajiajiri na wakati hawana mitaji na yule anayesisitiza wajiajiri ili hali yeye ameajiriwa

Karibuni kwa maoni wadau
 
Kuna Muda nataman wale masniper wa sehemu flani wangekua wanawadungua watu kama hawa.. Watanzania tunaenda kuwa kama wakongo kila siku kudanganywa tu.. Waanze kuwafyatua mawaziri waongowaongo at least wengine watakuwa na nidham.. Sio kuua innocents.. Jitu limeajiriwa linakwambia jiajiri.. Si uzuzu uo.. IPO siku hizo nafasi wanazotunyanyasa nazo hawatazitaman hata kidogo.. Masniper jaman..Msaada wawajibisheni hawa watuu
 
Kuna Muda nataman wale masniper wa sehemu flani wangekua wanawadungua watu kama hawa.. Watanzania tunaenda kuwa kama wakongo kila siku kudanganywa tu.. Waanze kuwafyatua mawaziri waongowaongo at least wengine watakuwa na nidham.. Sio kuua innocents.. Jitu limeajiriwa linakwambia jiajiri.. Si uzuzu uo.. IPO siku hizo nafasi wanazotunyanyasa nazo hawatazitaman hata kidogo.. Masniper jaman..Msaada wawajibisheni hawa watuu
You need to be careful now, moderator wanaweza kukupa adhabu kubwa kwa hayo maneno
 
Salaam
Kama kichwa kinavyoeleza ni mwaka wa pili sasa serikali haijatoa ajira wala kupandisha mishahara na vyeo kwa watumishi kwa kigezo kwamba bado inafanya uhakiki wa watumishi hewa hakuna anayepinga kwamba zoezi hili si jema.

Baada ya Mhe. Rais kukabidhiwa ripoti ya watumishi hewa watanzania wengi walipata matumaini kwamba zoezi hili limefikia ukomo badala yake hivi karibuni mawaziri wanasimama majukwaani na kuuambia umma kwamba uhakiki bado unaendelea, madhalani kauli zao zimekuwa zikibadilika mara kwa mara,


Me Ni Mwana Ccm Dam Dam Pia Mh Magu Ana Kura Yangu Ila Kiukweli I Miss My Prev President J.kikwete Kpnd Hicho Nasoma Nilikuaga Nasikia Kila Mwaka Ajira Zinatoka Kwa Kusema Hvo Cpingi Hatua Za Mh Magu Bali Naunga Mkono Sana La Ulipaji Wa Kod Na Maana Ndio Inawezesha Kulipa Mishahara Pia Swala La Chet Feki Let Him Do As He Wish Naamin Mungu Yupo Pamoja Nae Tuendelee Kumuombea Yeye Mh Na Serikari Yake
 
You need to be careful now, moderator wanaweza kukupa adhabu kubwa kwa hayo maneno


Yeaaah sometimes I got too emotional.. And I let the beast in me take over.. Bt usinifkirie vibaya.. Cpend hiyo kitu itokee bt kuna muda inakera.. Watumishi wa umma tumegeuzwa vikaragosi..
 
Sometimes ni Vizuri kuuficha ukweli hasa pale inapo onekana kuwa madhara ya watu kufahamu ukweli ni makubwa kuliko wasipo fahamu. Watanzania wenzangu endeleeni kuwa wavumilivu nchi imefulia balaa!

666
 
Poleni watanzania na serikali yenuu ya hapa kazi tu wakati wasomi na mashule yao kichwani wanasota mtaani shida yenu ikifika 2020 mnafanya makosa ya kujirudia tu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom