Mungi
JF Gold Member
- Sep 23, 2010
- 16,975
- 9,566
Pamoja na tuhuma zote zilizoibuliwa kuhusu ubadirifu na matumizi mabaya ya madaraka kwa baadhi ya mawaziri, imeonekana dhahiri hakuna hatua zitakazochukuliwa dhidi ya watuhumiwa wakuu ambao ni mawaziri.
Mawaziri kwa upande wao inaonekana wameitunishia misuli serikali, kwamba hawako tayari kuwajibika.
Inaonekana pia madudu yote yaliyofanyika yanaonekana ni ngeni mbele ya bunge, lakini siyo ngeni mbele ya Rais na serikali yake.
Kilichoonyeshwa na waziri mkuu ambaye ni kiongozi wa shughuli za serikali kwa kutokuchukua hatua ni udhaifu mkubwa mbele ya watanzania. Ni katika mazingira haya ambayo kila mtanzania mzalendo aliyekereka na wizi mkubwa uliofanywa na watendaji wa serikali kuachwa mdomo wazi baada ya waziri mkuu kushindwa kuwajibika.
Sote tunafahamu kuwa waziri mkuu hana madaraka ya kumwondoa mteule wa rais. Lakini kama kweli waziri wetu mkuu kama mbunge na kama waziri mkuu naye ameguswa na wizi mkubwa namna hii, alitakiwa kufanya kile ambacho kiko kwenye uwezo wake, ambayo ni kuachia ngazi badala ya kulialia mbele ya wabunge.
Waziri mkuu amewatega wabunge pamoja na wananchi waliokereka na huu ujambazi uliofanywa na watendaji wa serikali.
Serikali imetega wabunge waliokereka kwa kutochukua hatua za dhati za uwajibikaji, kuona nini kitatokea endapo kama haitachukua hatua. Serikali ilichokifanya ni kuweka ahadi feki kusema kuwa waziri mkuu atatoa tamko la maamuzi ya serikali dhidi ya tuhuma zilizotolewa kwa mawaziri wake.
Ninachokiona ni kwamba hii game ya serikali itachezwa bila mtu kuwajibishwa, kutokana na baadhi ya mawaziri waliotuhumiwa kusema wao wakimwaga mboga na sisi tunamwaga ugali.
Hatari kwa afya ya Tanzania
Hatari kwa afya ya wazalendo
Imefikia wakati ambao watanzania hawatakuwa na uwoga na mabomu ya machozi, maji yanayowasha, na wapo tayari kufa kwa ajili ya haki au kufungwa kwa uonevu kwa kutetea haki yao.
Mungu Ibariki Tanzania ya watu waliostaarabika, wapole, wanyenyekevu, wakarimu, wenye huruma, lakini siyo wanyonge.
Mawaziri kwa upande wao inaonekana wameitunishia misuli serikali, kwamba hawako tayari kuwajibika.
Inaonekana pia madudu yote yaliyofanyika yanaonekana ni ngeni mbele ya bunge, lakini siyo ngeni mbele ya Rais na serikali yake.
Kilichoonyeshwa na waziri mkuu ambaye ni kiongozi wa shughuli za serikali kwa kutokuchukua hatua ni udhaifu mkubwa mbele ya watanzania. Ni katika mazingira haya ambayo kila mtanzania mzalendo aliyekereka na wizi mkubwa uliofanywa na watendaji wa serikali kuachwa mdomo wazi baada ya waziri mkuu kushindwa kuwajibika.
Sote tunafahamu kuwa waziri mkuu hana madaraka ya kumwondoa mteule wa rais. Lakini kama kweli waziri wetu mkuu kama mbunge na kama waziri mkuu naye ameguswa na wizi mkubwa namna hii, alitakiwa kufanya kile ambacho kiko kwenye uwezo wake, ambayo ni kuachia ngazi badala ya kulialia mbele ya wabunge.
Waziri mkuu amewatega wabunge pamoja na wananchi waliokereka na huu ujambazi uliofanywa na watendaji wa serikali.
Serikali imetega wabunge waliokereka kwa kutochukua hatua za dhati za uwajibikaji, kuona nini kitatokea endapo kama haitachukua hatua. Serikali ilichokifanya ni kuweka ahadi feki kusema kuwa waziri mkuu atatoa tamko la maamuzi ya serikali dhidi ya tuhuma zilizotolewa kwa mawaziri wake.
Ninachokiona ni kwamba hii game ya serikali itachezwa bila mtu kuwajibishwa, kutokana na baadhi ya mawaziri waliotuhumiwa kusema wao wakimwaga mboga na sisi tunamwaga ugali.
Hatari kwa afya ya Tanzania
Hatari kwa afya ya wazalendo
Imefikia wakati ambao watanzania hawatakuwa na uwoga na mabomu ya machozi, maji yanayowasha, na wapo tayari kufa kwa ajili ya haki au kufungwa kwa uonevu kwa kutetea haki yao.
Mungu Ibariki Tanzania ya watu waliostaarabika, wapole, wanyenyekevu, wakarimu, wenye huruma, lakini siyo wanyonge.