Midas Touch
Senior Member
- Jan 23, 2008
- 191
- 203
WAZIRI WA ELIMU PAMOJA NA MKURUGENZI WA TAASISI YA ELIMU WAMESHINDWA KUSIMAMIA SYLLABUS NA MIHULA YA SHULE: SHULE BINAFSI ZINA MIHULA NA LIKIZO ZAO TOFAUTI
Katika suala hili msomaji zingatia haya:
Taasisi ya Elimu Tanzania (TET) ina jukumu la kutafsiri kwa vitendo Sera za Serikali kuhusu Elimu kwa kubuni mitaala na Programu za elimu zitakazowezesha utoaji wa elimu bora katika ngazi ya Elimu ya awali, Msingi, Sekondari na Elimu ya Ualimu. Kazi hii hufanywa na Taasisi ya Elimu chini ya miongozo ya Waziri wa Elimu, kwa sasa kufikia May 2025 waziri wa elimu ni Prof. Adolf Mkenda na Mkurugenzi wa Taasisi ya Elimu Tanzania ni Dr. Aneth Komba.
Kwa mujibu wa Programu za elimu zitakazowezesha utoaji wa elimu bora, silabasi (syllabus) inatumiaka kama muongozo wa vipindi, muda, mihula na upimaji (mitihani). Silabasi ni hati inayoangazia taarifa muhimu kwa ajili ya kozi, ikijumuisha mada zinazoshughulikiwa, kazi, tarehe za kukamilisha na sera za uwekaji alama. Inatumika kama mwongozo kwa waalimu na wanafunzi, ikifafanua matarajio na majukumu.
Shule ya wasichana ya St. Clara pale Same mkoani Kilimanjaro ni mfano halisi ikiwakilisha shule nyinginezo nyingi. Shule ilifunguliwa tarehe 11/1/2025 na likizo imepangwa kufanyika kwa kidato cha II na kidato cha IV kati ya tarehe 24/6/2025 hadi 5/7/2025 sawa na siku 11 kati ya miezi 6 (siku 182). Kidato cha kwanza na Kidato cha tatu wenyewe watakuwa likizoni kati ya tarehe June 7 na July 5 2025. Kidato cha pili na kidato cha nne watabaki shuleni kwa siku 17 wakipatiwa ELIMU YA KIKASUKU kwa siku 17 wakilipia Tsh 100,000/= nje ya ada ya kawaida. HII NI KWA KISINGIZIO HAFIFU, ETI NI MADARASA YA MITIHANI YA KITAIFA 2025!
Mh. Adolf Mkenda, waziri wa elimu kunako mwezi Aprili 2025 alikaririwa na baadhi ya vyombo vya habari akisisitiza kuhusu shule zote kuzingatia na kuheshimu mihula, mitaala na likizo za wanafunzi kwa mujibu wa miongozo ya Taasisi ya Elimu Tanzania. Lakini hali imekuwa tofauti kabisa baada ya wamiliki wa shule binafsi kutumia nguvu ya pesa/rushwa hadi kupata vibali vya kuongeza mida na ada nyakati za likizo ya mwezi June 2025. Kwa mujibu wa vyanzo vya habari, vibali vya kuminya likizo za mwezi wa nne na mwezi wa sita vinatolewa na viongozi wa elimu wilayani na mikoani. Haiwezekani na si MPANGO watoto wa miaka 12,13,14,15 kubaki shuleni kwa siku 182 bila likizo kwa mujibu wa miongozo ya elimu na hata mashariano na wazazi.
KWA MAELEZO HAYA, MH. WAZIRI WA ELIMU TUNAOMBA UTOE TAMKO RASMI NA KALI KUELEKEA LIKIZO NDEFU ZA NUSU MWAKA, JUNE 2025 WAKATI BAJETI YA WIZARA YA ELIMU IKIJADILIWA BUNGENI WIKI HII.
Katika suala hili msomaji zingatia haya:
Taasisi ya Elimu Tanzania (TET) ina jukumu la kutafsiri kwa vitendo Sera za Serikali kuhusu Elimu kwa kubuni mitaala na Programu za elimu zitakazowezesha utoaji wa elimu bora katika ngazi ya Elimu ya awali, Msingi, Sekondari na Elimu ya Ualimu. Kazi hii hufanywa na Taasisi ya Elimu chini ya miongozo ya Waziri wa Elimu, kwa sasa kufikia May 2025 waziri wa elimu ni Prof. Adolf Mkenda na Mkurugenzi wa Taasisi ya Elimu Tanzania ni Dr. Aneth Komba.
Kwa mujibu wa Programu za elimu zitakazowezesha utoaji wa elimu bora, silabasi (syllabus) inatumiaka kama muongozo wa vipindi, muda, mihula na upimaji (mitihani). Silabasi ni hati inayoangazia taarifa muhimu kwa ajili ya kozi, ikijumuisha mada zinazoshughulikiwa, kazi, tarehe za kukamilisha na sera za uwekaji alama. Inatumika kama mwongozo kwa waalimu na wanafunzi, ikifafanua matarajio na majukumu.
- Sifa Muhimu za Silabasi:
- Maelezo ya Kozi: Hutoa muhtasari mfupi wa somo na malengo ya kujifunza.
- Masomo Yanayohitajika: Huorodhesha vitabu vya kiada, nakala, au nyenzo zingine ambazo wanafunzi wanahitaji kusoma.
- Ratiba ya Kozi: Inabainisha mada zitakazoshughulikiwa kila wiki au kipindi, pamoja na tarehe za kukamilisha kazi na mitihani.
- Sera za Kozi: Inabainisha sheria na taratibu kuhusu mahudhurio, ushiriki, na uadilifu kitaaluma.
Shule ya wasichana ya St. Clara pale Same mkoani Kilimanjaro ni mfano halisi ikiwakilisha shule nyinginezo nyingi. Shule ilifunguliwa tarehe 11/1/2025 na likizo imepangwa kufanyika kwa kidato cha II na kidato cha IV kati ya tarehe 24/6/2025 hadi 5/7/2025 sawa na siku 11 kati ya miezi 6 (siku 182). Kidato cha kwanza na Kidato cha tatu wenyewe watakuwa likizoni kati ya tarehe June 7 na July 5 2025. Kidato cha pili na kidato cha nne watabaki shuleni kwa siku 17 wakipatiwa ELIMU YA KIKASUKU kwa siku 17 wakilipia Tsh 100,000/= nje ya ada ya kawaida. HII NI KWA KISINGIZIO HAFIFU, ETI NI MADARASA YA MITIHANI YA KITAIFA 2025!
Likizo fupi na ndefu ni muhimu sana kwa wanafunzi kama mitaala na silabasi za Taasisi ya Elimu Tanzania zinavoelekeza. Swali ni kwa sababu zipi waziri wa elimu na timu yake pamoja na Taasisi ya Elimu Tanzania hawafuatilii kwa karibu mienendo ya elimu, mihula na utendaji mashuleni? Wakaguzi wa elimu wako wapi?
WAZIRI WA ELIMU ATOA AGIZO POLE (SOFT ORDER) MWEZI APRILI 2025Mh. Adolf Mkenda, waziri wa elimu kunako mwezi Aprili 2025 alikaririwa na baadhi ya vyombo vya habari akisisitiza kuhusu shule zote kuzingatia na kuheshimu mihula, mitaala na likizo za wanafunzi kwa mujibu wa miongozo ya Taasisi ya Elimu Tanzania. Lakini hali imekuwa tofauti kabisa baada ya wamiliki wa shule binafsi kutumia nguvu ya pesa/rushwa hadi kupata vibali vya kuongeza mida na ada nyakati za likizo ya mwezi June 2025. Kwa mujibu wa vyanzo vya habari, vibali vya kuminya likizo za mwezi wa nne na mwezi wa sita vinatolewa na viongozi wa elimu wilayani na mikoani. Haiwezekani na si MPANGO watoto wa miaka 12,13,14,15 kubaki shuleni kwa siku 182 bila likizo kwa mujibu wa miongozo ya elimu na hata mashariano na wazazi.
KWA MAELEZO HAYA, MH. WAZIRI WA ELIMU TUNAOMBA UTOE TAMKO RASMI NA KALI KUELEKEA LIKIZO NDEFU ZA NUSU MWAKA, JUNE 2025 WAKATI BAJETI YA WIZARA YA ELIMU IKIJADILIWA BUNGENI WIKI HII.