Kifurukutu
JF-Expert Member
- Aug 29, 2013
- 4,685
- 6,768
Wakuu
Katika hali ya kushangaza na kustaajabisha, mpaka sasa serikali haijajihusisha na utoaji wa misaada ya kibinadamu kwa wahanga wa mafuriko kwa Tanzania Dar es salaam na huko Zanzibar.
Misaada inayozungumziwa hapa ni ile inayohusu malazi na chakula, kiukweli sijapata kuona wala kusikia serikali ikilifikiria swala hili ambalo ni muhimu kuliko vyote
Ni kweli wanaopatwa na janga hili walikwisha amuliwa hapo awali wahame mabondeni lakini ndio hali ya watanzania hivyo serikali inatakiwa ithamini wananchi wake
Au mpaka UN ilete maturubai na msosi ndio nshituke?
Mafuriko ni janga kama majanga mengine, serikali mliangalie hili hata kwa kugeukia kwa mfuko wenu wa maafa.
Katika hali ya kushangaza na kustaajabisha, mpaka sasa serikali haijajihusisha na utoaji wa misaada ya kibinadamu kwa wahanga wa mafuriko kwa Tanzania Dar es salaam na huko Zanzibar.
Misaada inayozungumziwa hapa ni ile inayohusu malazi na chakula, kiukweli sijapata kuona wala kusikia serikali ikilifikiria swala hili ambalo ni muhimu kuliko vyote
Ni kweli wanaopatwa na janga hili walikwisha amuliwa hapo awali wahame mabondeni lakini ndio hali ya watanzania hivyo serikali inatakiwa ithamini wananchi wake
Au mpaka UN ilete maturubai na msosi ndio nshituke?
Mafuriko ni janga kama majanga mengine, serikali mliangalie hili hata kwa kugeukia kwa mfuko wenu wa maafa.