tpaul
Platinum Member
- Feb 3, 2008
- 25,950
- 25,327
Mfumo wa serikali 3 hauepukiki hata kidogo. Nawashangaa sana wale wanafiki wachache wanaokataa uwepo wa serikali huku wakijua kwamba wazanzibar wao wana serikali yao kamili--wana rais, jeshi, benki kuu, wimbo wa taifa, bunge, mahakama, na bendera ya nchi yao.
Hakuna mtanganyika anayeruhusiwa kumiliki hata futi moja ya eneo la ardhi nchini zanzibar lakini wao wakija huku bara wanamiliki ardhi kadri wapendavyo. Sasa huu ni muungano wa aina gani ambao upande mmoja unakubali kunyonywa na unafurahia unyonyaji huo?
Aidha, wazanzibar (wanyonyaji) wao wako tayari kuwepo kwa serikali 3 hata kuanzia leo lakini eti watanganyika (wanyonywaji) hatutaki. Haya mbona ni mambo ya ajabu sana?
Wazanzibar tayari wao wana serikali yao ila wanatuunga mkono watanganyika ili nasi tupate serikali yetu. Sasa kwa nini tunawakatisha tamaa wakati wao wanatusaidia ili nasi tuwe na serikali yetu?
Jamani, watanganyika tuache unafiki ndugu zangu. Mfumo wa serikali 3 hauepukiki katu.
Hakuna mtanganyika anayeruhusiwa kumiliki hata futi moja ya eneo la ardhi nchini zanzibar lakini wao wakija huku bara wanamiliki ardhi kadri wapendavyo. Sasa huu ni muungano wa aina gani ambao upande mmoja unakubali kunyonywa na unafurahia unyonyaji huo?
Aidha, wazanzibar (wanyonyaji) wao wako tayari kuwepo kwa serikali 3 hata kuanzia leo lakini eti watanganyika (wanyonywaji) hatutaki. Haya mbona ni mambo ya ajabu sana?
Wazanzibar tayari wao wana serikali yao ila wanatuunga mkono watanganyika ili nasi tupate serikali yetu. Sasa kwa nini tunawakatisha tamaa wakati wao wanatusaidia ili nasi tuwe na serikali yetu?
Jamani, watanganyika tuache unafiki ndugu zangu. Mfumo wa serikali 3 hauepukiki katu.