Sera ya kupiga Picha inapokuwa Bora Kuliko ya utekelezaji

August

JF-Expert Member
Jun 18, 2007
8,398
4,057
Kuelekea uchaguzi na hata hapo nyuma tumeona kuwepo kwa mgombea mooja ambaye sera yake ya kuwa saidia watu wa chini au ulemavu ni kupiga nao picha au kutoa hela zake (za mfukoni/ikulu) na kumsaidia huyo mtu mwenye shida, sasa mimi ninajiuliza kilicho bora ni kutoa msaada wa namna hiyo au ni kuweka mfumo ambao utasaidia huyo mwenye shida kuweza hususani na serikali, kwa sababu ni jukumu la serikali kufanya hivyo.
na kuna hili jingine la mwanafunzi kumpenda mwl wake wakati wa uchaguzi,
suala la kujiuliza huyu mwanafunzi alikuwa wapi siku nzote kumtembelea mwalimu wake mpaka wakati wa kampeni? na baada ya hapo kutoa picha zake kwenye magazeti chapishi/waraka umeme nk, na zaidi ya hapo mwanafunzi mwenyewe akiwa ni mtu mwenye uwezo, wa kuongea na baba akaweka sera zilizo bora ili huyo mwl maisha yake ya kawa bora, kwa kuongezewa kipato, kupata mikopo mfano ya ujenzi wa nyumba, badala ya kumtumia mtu kama huyu kama mtaji wa kisiasa.
naomba kuwakilisha au kuelemwishwa, maana wenzetu wanatuambia bora kumfundisha mtu kuvua samaki badala ya kumpa samaki, sasa tatizo hapa sijui nini, huyu mtu haelewi? au , maana ukisema kisomo kidogo itakuwa si sawa kuna watu hawakwenda shule lakini wanauelewa wa jinsi ya kumuongoza mtu au kumfundisha mtoto awe mtu bora .
 
Back
Top Bottom