Seliani hospital (ALMC), huduma hafifu

Seliani hospital (ALMC), huduma hafifu

aikacharity

Senior Member
Joined
Jan 12, 2015
Posts
109
Reaction score
68
Kwa wana JF wanaoifahamu hospitali ya Arusha Lutheran Medical Centre (ALMC) maarufu Seliani ni ukweli usiopingika kuwa hospitali hii ni mpya yenye jengo zuri, safi na ipo mahali ambapo ni rahisi kufikika kwa mtu anaehitaji huduma. Pia hospitali hii inamilikiwa na Kanisa jambo ambalo linawafanya watu waamini kuwa huduma zake zitakuwa bora kuliko hospitali za serikali. Kinyume na matarajio hospitali hii haina huduma nzuri kwa maana ya:-

-Hakuna ukarimu kuanzia mapokezi hadi kwa madaktari.

-Kuna processes kibao hadi kupata huduma utapita madirisha manne au zaidi ndio uonane na daktari hivyo wagonjwa husota muda mrefu kwenye foleni.

-Huduma zao pamoja na uhafifu wake ni very expensive. Gharama haziendani na huduma.

-Wahudumu hususani mapokezi ni wengi wamezidi badala ya kutumia wingi wao kuhudumia wagonjwa wao muda mwingi hupiga stori na kuchat huku wakihudumia kwa mapozi. Nadhani mpo wengi mnaokerwa na hospitali hizi za private kutoa huduma hafifu.
 
Zamani wakiwa kwenye jengo dogo ilikua angalau. Saivi ukienda apo kama atufaamiani na mtu utakesha mapokezi .......Pale ni jengo tu .......nadhani pia wanafanya kazi kindugu
 
pale hakuna kitu....narudia tena hakuna kitu...hospitality ni ziro..better uende maount meru ijulikne moja kuliko hao wanojiita serian...majitu weengi lakini haipnekani impact ya wingi wao,kila wakati wanapiga soga tu...
 
Ni kweli kabisa Selian ALMC huduma zao zina utata mno. kwanza kabisa hao watu wote unaowaona reception hawana ujuzi wowote wa mambo ya afya kwa maana nyingine they ar not trained kuhudumia. Mimi niliwahi kuingia kwenye mgogoro na mmoja wa hao kina dada, alinizuia kumwona doctor with no reason mpaka doctor akatoka kwenye rum yake na kuja kunichukua. nilikua mjamzito na nilikua nimekaribia kujifungua so nilikua na appointment ya kuonana na doctor kila wiki. wiki iliyofuata aliponiona tu nimefika akaenda kutafuta file langu na kulificha. nilikaa zaidi ya masaa manne nasubiri kuitwa jina. baadae ndio faili likaonekana na aliyeniambia ni mwenzake, ikabidi wamrepot ili achukuliwe hatua. sasa you can imagine ni mambo mangapi wanafanya kuwakomoa wagonjwa.
 
mh,my friend,and wife of my friend,and my sister alienda AICC wakamwambia mtoto tumboni ni mkubwa,inabidi apate operation,akienda selian wanamuambua hakuna shida na hamna haja ya operation,akaamua kwenda seliani huko huko,mimba ikapitiliza selian wakamuambia hamna shida siku anajifungua kweli mtoto alikuwa mkubwa, alifariki yule dada na kuacha mtoto, heri uende mt,meru au icc tuu,
 
Mountmeru ni salama sana kwa wajawazito pliizz msiidharau kwavile ni ya serikali. Pale majanga alikufa wifi yetu na mtoto wake wakati wa kujifungua.
 
Bora uende dispensary pale hapafai kabisa. Nimeyashuhudia kwa macho yangu nimekaa masaa 4 jamaa hajakuona dokta. Kiufupi hawaeleweki au ni yale majengo ndo yanawatia kiburi ???????? pumbavu zao kabisa bora uende Mount meru uhonge nesi 10000 mkeo atajifungua salama.
 
jamani nawapinga kwa 100%. Binafsi naikubali sana hospital ya ALMC kuliko hospital yoyote ile Arusha, kwangu mimi mimi imekuwa msaada mkubwa sana kwangu. sababu zifuatazo.
1. dada yangu alikuwa na tatizo la kutopata mimba, alianzia Mt. Meru kama mienzi 4 bila kujua tatizo, then tukaagizwa kwenda AICC kulikuwa na Dr. wa wanawake pale amehudhuria zaidi ya mwaka bila msaada, mwisho tukaagizwa kumtafuta Dr. msuya yeye alimfanyia baadhi ya vipimo (vingine tulivifanya kwa Dr.mohamed) havikuwepo pale hospital yake, mwisho alimwambia kuwa mirija yake imeziba na hawezi kupata mtoto kwa njia ya kawaida mpaka apandikizwe. tukiwa katika process ya kutaka afanyiwe hivyo tulikutana na mama mmoja ambaye alitushauri tunde ALMC, kweli tulienda, tulipewa appointment ya kumuona Dr. wa wanawake, kwa kweli alimsaidia leo ana watoto 2 bila kupandikiziwa mbegu. Hapo nilianza kuiamini ALMC sababa dadangu alitafuta mtoto wa muda mrefu sana.

2. Nilimpeleka mtoto wangu wa miaka 2 kutahiriwa pale, nikaonana na Dr. anayehusika na upasuaji wa watoto, yeye alinishauri lazima mtoto afanyiwe uchunguzi kabla ya kutahiriwa, kwanza nilipinga sababu niliona kama ni gharama za bure, baada ya Dr. kunieleza umuhimu nilikubali mtoto wangu afanyiwe check up kwanza. Yaaani ilikuwa kama bahati mwanangu alikuta na appendix, ni muda mrefu alikuwa akilalamika maumivu ya tumbo, nimeshampeleka hospital nyingi kila akipimwa hakuonekana ugonjwa ikafika wakati nikaona ni jambo la kawaida, kumbe mwanangu alikuwa na kidole tumbo (appendix) namshukuru Mungu alifanyiwa operation zote yaani tohara na kidole tumbo na sasa ni mzima wa afya.

3. Binamu yangu alipata ajali mwaka jana, akavunjika miguu yote miwili, alilazwa Mt. meru, Dr pale alisema mguu mmoja unafaa kuwekwa POP ila huo mwingine lazima ukatwe, tulipopata hiyo taarifa ilitusikitisha sana sababu ni kijana wa miaka 20 tu tena yatima, nilikumbuka ALMC hospital nikashauri familia tujichange akajaribu huko, jamani sijui nimrudishie Mungu nini kwa ajili yake. Dr wa mfupa pale alishangaa sana kusikia kuu mguu ule ulitakiwa kukatwa, hakuamini, alituambia mguu ule ni wa kuwekewa chuma na mgonjwa atakuwa na uwezo wa kutembea kama zamani baada ya muda. Mungu mkubwa kijana sasa ni mzima na anaendelea na masomo yake.

4. Mwaka jana nafikiri mwenzi wa 8 or 9, nilikwenda kumsalimia ndugu yangu. kufika kwake nilimkuta jirani yake ana mtoto mgonjwa. alikuwa na miaka 4, katika kuongea nae alinieleza jinsi mtoto wake anavyoumwa, ni kama vile mwanangu alivyokuwa anaumwa na tumbo, alikuwa anahudhuria kwa Dr mariamu na yeye alisema mtoto ana UTI, kila mara alimrudisha hospital Pale AICC na kupewa dawa ila tumbo liliendelea kuuma na mwisho mtoto alianza kunya damu ila docta, tena specialist hakujua tatizo la mtoto, nilimshauri aende seliani (ALMC) kweli kesho yake alienda pale, mtoto alijulikana ana appendix, alifanyiwa operation na sasa ni mzima. mtoto huyu alianza kuuwa akiwa na miaka 2 pasipo kujulikana tatizo.

Sipendi uswahili, kiukweli naipenda sana ile hospital, nawaamini madaktari wake, wanajituma, wanaweza na wana moyo. Kwangu ndiyo changuo langu ninapofikiria swala la matibabu, sasa nikuulize wewe mtoa mada hivi kweli umewai kutibiwa ALMC???????????????????????? Hayo madirisha manne uliyopita kabla ya kumuona Dr. ni yapi????????????????????????????? me najua unaanzia reception, cashier, nurce. na kila kimoja kina umuhimu wake
1. Reception - lazima ukatoe namba ya file ili utafutiwe file or kama ni mara ya kwanza uandikishwe, bila kupitia reception sidhani kama kuna mtu ataona kuwa kuna mtu amefika na anahitaji huduma, labda mganga wa kienyeji.

2. Cashier - ukalipe ela, hiyo ni kawaida kwa hospital zote kulipa ela ya kumuona docta hakuna private hospital hata moja duniani utaingia kwa Dr. bila kulipa consulatation fees, kama huwezi nenda govement hospital, unafiriki gharama za kulipa wafanyakazi utalipa kwa maneno???????????????????

3. Nurce - yaani hapo me ndio napapenda huwezi nipeleka kwa docta bila kujua uzito wangu na pressure, napenda sana jinsi ALMC wanavyozingatia huu utaratibu.

Nimalize kwa kusema, naipenda sana ALMC, nafurahi huduma zake, ingawa mimi siyo mlutheran, nawapongeza sana KKKT kwa kufungua hospital kama hiyo ambayo imekuwa mkombozi wa wakazi wa Arusha.
 
Hiyo hospital Bomu kabisa Kuna Mtoto wa Jiran alingatwa na Mbwa wakampeleka hapo akatibiww wakamtibu baadae aliporuhusiwa akarejea nyumban baada ya kama Wiki moja akaanzwa tena wakamkimbiza Nairobi cz hali ya Mtoto ilibadilika na kuwa mbaya sana kumbe walikua hawajamchoma sindano ya Kuzuia Sum ya yule Mbwa matokeo yake Ikasambaaa had kwny Ubongo matokeo yake yule Mtoto alifariki!
 
Mm Binafsi baungana na ww Wale jamaa ile Ni Hotel sio Hospital ile garama ni balaa haiwezekani Kulala kwa siku 60000 hapo nje na matibabu.
 
Sina hamu na hiyo hospital,huduma mbovu za kukera,manesi wako very slow,dharau zimewajaa,haina la maana.
 
Kingine ni kuwa mgonjwa wako akilazwa umletee chakula usimleteee bili ya chakula utalipa tu.isitoshe chakula chenyewe ss kibaya kama nn shame on them
 
Mimi nilipata huduma nzuri tu kujifungua..japo gharama kwa siku moja tuaana nilienda saa tano nikajifungua saa 9 na kesho yake mchana nikaruhusiwa nilisaini form ya laki sita na nusu....ilikuwa ni normal delivery...kwenye fomu ya bima wakaandika seazure laki tatu kuuliza wanasema ni nyuzi moja niliyoshonwa wakati najifungua...hapo ndo nilichoka..nikabeba kichanga changu nikasepa..watajuana na Bima

Sent using Jamii Forums mobile app
 
jamani nawapinga kwa 100%. Binafsi naikubali sana hospital ya ALMC kuliko hospital yoyote ile Arusha, kwangu mimi mimi imekuwa msaada mkubwa sana kwangu. sababu zifuatazo.
1. dada yangu alikuwa na tatizo la kutopata mimba, alianzia Mt. Meru kama mienzi 4 bila kujua tatizo, then tukaagizwa kwenda AICC kulikuwa na Dr. wa wanawake pale amehudhuria zaidi ya mwaka bila msaada, mwisho tukaagizwa kumtafuta Dr. msuya yeye alimfanyia baadhi ya vipimo (vingine tulivifanya kwa Dr.mohamed) havikuwepo pale hospital yake, mwisho alimwambia kuwa mirija yake imeziba na hawezi kupata mtoto kwa njia ya kawaida mpaka apandikizwe. tukiwa katika process ya kutaka afanyiwe hivyo tulikutana na mama mmoja ambaye alitushauri tunde ALMC, kweli tulienda, tulipewa appointment ya kumuona Dr. wa wanawake, kwa kweli alimsaidia leo ana watoto 2 bila kupandikiziwa mbegu. Hapo nilianza kuiamini ALMC sababa dadangu alitafuta mtoto wa muda mrefu sana.

2. Nilimpeleka mtoto wangu wa miaka 2 kutahiriwa pale, nikaonana na Dr. anayehusika na upasuaji wa watoto, yeye alinishauri lazima mtoto afanyiwe uchunguzi kabla ya kutahiriwa, kwanza nilipinga sababu niliona kama ni gharama za bure, baada ya Dr. kunieleza umuhimu nilikubali mtoto wangu afanyiwe check up kwanza. Yaaani ilikuwa kama bahati mwanangu alikuta na appendix, ni muda mrefu alikuwa akilalamika maumivu ya tumbo, nimeshampeleka hospital nyingi kila akipimwa hakuonekana ugonjwa ikafika wakati nikaona ni jambo la kawaida, kumbe mwanangu alikuwa na kidole tumbo (appendix) namshukuru Mungu alifanyiwa operation zote yaani tohara na kidole tumbo na sasa ni mzima wa afya.

3. Binamu yangu alipata ajali mwaka jana, akavunjika miguu yote miwili, alilazwa Mt. meru, Dr pale alisema mguu mmoja unafaa kuwekwa POP ila huo mwingine lazima ukatwe, tulipopata hiyo taarifa ilitusikitisha sana sababu ni kijana wa miaka 20 tu tena yatima, nilikumbuka ALMC hospital nikashauri familia tujichange akajaribu huko, jamani sijui nimrudishie Mungu nini kwa ajili yake. Dr wa mfupa pale alishangaa sana kusikia kuu mguu ule ulitakiwa kukatwa, hakuamini, alituambia mguu ule ni wa kuwekewa chuma na mgonjwa atakuwa na uwezo wa kutembea kama zamani baada ya muda. Mungu mkubwa kijana sasa ni mzima na anaendelea na masomo yake.

4. Mwaka jana nafikiri mwenzi wa 8 or 9, nilikwenda kumsalimia ndugu yangu. kufika kwake nilimkuta jirani yake ana mtoto mgonjwa. alikuwa na miaka 4, katika kuongea nae alinieleza jinsi mtoto wake anavyoumwa, ni kama vile mwanangu alivyokuwa anaumwa na tumbo, alikuwa anahudhuria kwa Dr mariamu na yeye alisema mtoto ana UTI, kila mara alimrudisha hospital Pale AICC na kupewa dawa ila tumbo liliendelea kuuma na mwisho mtoto alianza kunya damu ila docta, tena specialist hakujua tatizo la mtoto, nilimshauri aende seliani (ALMC) kweli kesho yake alienda pale, mtoto alijulikana ana appendix, alifanyiwa operation na sasa ni mzima. mtoto huyu alianza kuuwa akiwa na miaka 2 pasipo kujulikana tatizo.

Sipendi uswahili, kiukweli naipenda sana ile hospital, nawaamini madaktari wake, wanajituma, wanaweza na wana moyo. Kwangu ndiyo changuo langu ninapofikiria swala la matibabu, sasa nikuulize wewe mtoa mada hivi kweli umewai kutibiwa ALMC???????????????????????? Hayo madirisha manne uliyopita kabla ya kumuona Dr. ni yapi????????????????????????????? me najua unaanzia reception, cashier, nurce. na kila kimoja kina umuhimu wake
1. Reception - lazima ukatoe namba ya file ili utafutiwe file or kama ni mara ya kwanza uandikishwe, bila kupitia reception sidhani kama kuna mtu ataona kuwa kuna mtu amefika na anahitaji huduma, labda mganga wa kienyeji.

2. Cashier - ukalipe ela, hiyo ni kawaida kwa hospital zote kulipa ela ya kumuona docta hakuna private hospital hata moja duniani utaingia kwa Dr. bila kulipa consulatation fees, kama huwezi nenda govement hospital, unafiriki gharama za kulipa wafanyakazi utalipa kwa maneno???????????????????

3. Nurce - yaani hapo me ndio napapenda huwezi nipeleka kwa docta bila kujua uzito wangu na pressure, napenda sana jinsi ALMC wanavyozingatia huu utaratibu.

Nimalize kwa kusema, naipenda sana ALMC, nafurahi huduma zake, ingawa mimi siyo mlutheran, nawapongeza sana KKKT kwa kufungua hospital kama hiyo ambayo imekuwa mkombozi wa wakazi wa Arusha.
Halafu kwa nini wanakuuliza dini na dhehebu?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ni kweli kabisa Selian ALMC huduma zao zina utata mno. kwanza kabisa hao watu wote unaowaona reception hawana ujuzi wowote wa mambo ya afya kwa maana nyingine they ar not trained kuhudumia. Mimi niliwahi kuingia kwenye mgogoro na mmoja wa hao kina dada, alinizuia kumwona doctor with no reason mpaka doctor akatoka kwenye rum yake na kuja kunichukua. nilikua mjamzito na nilikua nimekaribia kujifungua so nilikua na appointment ya kuonana na doctor kila wiki. wiki iliyofuata aliponiona tu nimefika akaenda kutafuta file langu na kulificha. nilikaa zaidi ya masaa manne nasubiri kuitwa jina. baadae ndio faili likaonekana na aliyeniambia ni mwenzake, ikabidi wamrepot ili achukuliwe hatua. sasa you can imagine ni mambo mangapi wanafanya kuwakomoa wagonjwa.
Daah pole Sana dada , yaani anaficha file lako hili iweje ? So sad indeed
 
Mimi nilipata huduma nzuri tu kujifungua..japo gharama kwa siku moja tuaana nilienda saa tano nikajifungua saa 9 na kesho yake mchana nikaruhusiwa nilisaini form ya laki sita na nusu....ilikuwa ni normal delivery...kwenye fomu ya bima wakaandika seazure laki tatu kuuliza wanasema ni nyuzi moja niliyoshonwa wakati najifungua...hapo ndo nilichoka..nikabeba kichanga changu nikasepa..watajuana na Bima

Sent using Jamii Forums mobile app
Hahahahahaaa hila umelipa pesa nyingi kiasi , lakini hiyo tofauti itakuwa wameipiga
 
Back
Top Bottom